visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumamosi, 10 Mei 2014

TUWE NA FIKRA SAHIHI KATIKA BIASHARA.

UKOSEFU WA MAWAZO HUUA BIASHARA
KILA siku mamilioni ya watu wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali katika dunia hii tunayoishi.
Mbali na misukosuko katika ndoa au mahusiano ya mwanamke na mwanamme, hali inayochangia kutokuelewana, msongo wa mawazo, ugonjwa, wengine hufikia hatua ya kujinyonga.
Kadhia nyingine kubwa ni kuhusu kushindwa au kufilisika kwa biashara aliyonayo.
Kutokufanikiwa kwa biashara hizo kunatokana na mipango katika biashara, masoko na suala la kifedha.
Pia inakuwa si rahisi kujua kwa undani ni kwanini biashara ndogo zinakufa. Haitoshi kusema kuwa ni kutokana na ushindani wa kibiashara uliopo, ama mabadiliko ya teknolojia, madeni, mauzo madogo, ama huduma mbaya kwa wateja.
Yote hayo ni ugonjwa unaosababishwa na usimamizi mbovu katika biashara husika.
Mbali na hayo, ujuzi binafsi, elimu, kujituma na ari ya kazi ndivyo vinavyohitajika katika utawala wa biashara.
Biashara nyingi hushindwa kuendelea kutokana na ukosefu wa mawazo mazuri. Zinaweza kufa kutokana na muundo mbaya wa uwekezaji katika biashara.
Mara zote kumbuka kuwa, mpango mzuri wa biashara ni muongozo wa kufikia malengo ya kibiashara unayoyatarajia, hata kama kutakuwepo na baadhi ya vikwazo katika biashara ile unayoifanya.
Kumbuka kama huna mpango mzuri katika biashara uliyonayo, ni sawa na kuwa na silaha ambayo huwezi kuitumia wakati wa mapambano.
Jambo la kuelewa ni kwamba, kama hauna ujuzi wa kuendesha biashara yako, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kushindwa kuiendesha sio kwa sababu biashara hiyo haina faida, bali ni kwa kuwa unashindwa kuisimamia katika misingi inayotakiwa, kwa kuona ufahari kuwa na biashara ambayo haisongi mbele.
Jambo muhimu unapochagua kufanya biashara ni vema ukachagua ile ambayo una ujuzi nayo pia unaielewa kwa undani.
Unaweza kuwatumia wale watu wenye vipaji ama wenye uaminifu katika biashara ambao wataweza kukusaidia kwa kile unachotaka kukifanya.
Wape nafasi ya kukuongoza na kukufanyia tathmini au kukueleza kuwa hawakubaliani nawe pale unapokwenda tofauti katika biashara.
Ikumbukwe kuwa biashara nyingi zinaanza vizuri, lakini mwisho wake unakuwa mbaya, kwa kuwa biashara inaendelea kukua na wale wasimamizi wake wanashindwa kuisimamia vizuri kutokana na mahitaji yaliyopo kwa wakati huo au kutokuweka wafanyakazi wazuri wanaoweza kuleta ushindani kwenye soko.
Mfano mzuri katika hili, ni pale mfanyabiashara mdogo anapoanzisha chuo na baadaye kinakuwa chuo kikuu.
Hapa utaona kuwa wale wafanyakazi aliokuwa nao katika chuo kile akiwemo yeye mwenyewe, hawawezi kuwa na ushindani katika kuendesha chuo kikuu.
Kwa kuwa chuo kikuu kinafanikiwa kwa kuweka watu wenye uzoefu na ujuzi, ambao kiwango chao cha elimu kinaridhisha.
Hata mfanyabiashara mkubwa, Bill Gate ambaye ni mwanzilishi wa Microsoft, amefikia hapo alipo kutokana na kuwa na timu imara ya watu wanaomzunguka.
Kama mwanzilishi wa biashara yako inakubidi kujua ni wakati gani wa kuchukua watendaji wenye ujuzi katika biashara unayoifanya.
Kwa upande mwingine katika siku za leo, suala la masoko linaonekana kuwa muhimu kuliko bidhaa husika. Mlaji analundikiwa bidhaa nyingi zenye matumizi yanayofanana.
Hivyo inabidi kuwe na kampeni kubwa kwenye timu ya masoko ili kuweza kuuza bidhaa hizo.
Kumbuka kipindi kile ambacho bidhaa zilikuwa zikijiuza zenyewe kimekwishapita. Hivyo wajasiriamali wengi wanashindwa kujua ukweli huu katika kipindi hiki cha ushindani.
Wafanyabiashara hao wamekuwa wakifanya jitihada kubwa na kutumia muda mwingi kutengeneza bidhaa bora na kuziweka sokoni bila kujihangaisha kuhusu kutafuta masoko.
Matokeo yake, hutumia pesa nyingi kwenye kuendeleza bidhaa na pesa kidogo kwenye kutafuta masoko ya bidhaa hizo, mwisho wa siku, mapato hupungua na wanafilisika na kuondolewa sokoni na wapinzani wao ambao wanajua mikakati ya kupata masoko kwenye biashara walizonazo.
Lucy ngowi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni