visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumamosi, 22 Februari 2014

SHULE 10 ZILIZOSHIKA MKIA KATIKA MATOKEA YA KIDATO CHA NNE


Siku zote katika maisha kuna wa kwanza na wa mwisho ,kauli hii inajidhirisha mara baada ya NECTA kutangaza matokeo ya kidato cha nne nchini huku kukiwa na shule zilizoshika nafasi za juu na zile za zilizoshika mkia.
Kwa upande wa shule 10 za mwisho kwenye kundi la shule zenye watahiniwa zaidi ya 40, shule ya kwanza ni Kisima ya Pwani, Kitongoni ya Kigoma na Tongoni ya Tanga.
Nyingine ni Njechele ya Dar es Salaam, Lumemo ya Morogoro, Mvuti ya Dar es Salaam, Tambani ya Pwani, Nasibugani ya Pwani, Ungulu ya Morogoro na Kitonga ya Dar es Salaam.
Shule za mwisho kwenye kundi lenye watahiniwa chini ya 40 ni Singisa ya Morogoro, Hurui ya Dodoma, Barabarani ya Ruvuma, Nandanga ya Lindi na Vihokolo ya Mtwara.
Nyingine ni Chongoleani ya Tanga, Likawage ya Lindi, Ngwandi ya Dodoma, Rungwa ya Singida na Uchindile ya Morogoro

Jumanne, 11 Februari 2014

TUWAHESHIMU VIONGOZI WETU WA NCHI.


KUTOKA KWA MHARIRI.
Deonidas Mukebezi;Mhariri wa blog hii.


Katika katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 18 kifungu kidogo cha 1 kinampa kila mtu ambae ni raia wa Tanzania uhuru wa kutoa maoni bila kubughudhiwa na mtu.Ibara hiyo pia inampa mtu uhuru wa kusambaza,kupokea au kutoa taarifa zozote kupitia chombo chochote cha kusambaza na kupokea habari.Kama hiyo haitoshi ibara hiyo pia inampa mtu uhuru wa kutokuingiliwa katika taarifa zake binafsi.

Hata hivyo katika katiba hiyohiyo ya jamhuru ya muungano wa Tanzania ibara ya 30(1) inasema kuwa haki na uhuru hautatumiwa na mtu katika misingi kwamba zinaingilia haki na uhuru wa mtu mwingine.Pia kifungu cha pili cha ibara hiyo kinasema kuwa provission zinazotengeneza na kufanya hakina uhuru,havizuii utekelezwaji wa sheria za nchi au kuzuia sheria mpya zilizotungwa kufanya kazi.

Nimeanza na kidokezo hicho cha katiba kwasababu watu wengi wamekuwa wakijisahau na kutamka au kuposti mambo ambayo ni kinyume kabisa na malengo ya uhuru wa kujieleza.Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la picha nyingi za viongozi zikitumwa katika mitandao mbalimbali,facebook,instagram, na mingine ambazo zinawaonesha viongozi hao wakiwa katika hali ambazo hazikubaliki kimaadili.Baadhi ya picha zimekuwa na ujumbe unaomuonesha kiongozi husika akihamasisha watu kutokufanya kazi.Hii ni hatari sana.Tunapaswa kujua kuwa mtu anapoachwa kuwa huru kufanya chochote akitakacho maana yake anajitambua na pia anajua kujicontrol

Tuwaheshimu viongozi wa nchi kwa kuwa kuna watu wanaheshimu sana kile anachosema kiongozi,hii ina maana kuwa mambo mengine yanakuwa na adhari moja kwa moja kwa jamii.

HIZI HAPA NI BAADHI YA PICHA AMBAZO ZIIMETUMWA KATIKA MITANDAO MBALIMBALI.TUACHE TABIA HII.


Jumanne, 4 Februari 2014

KUFUNGIWA VIDEO YA SNURA 'NIMEVURUGWA'KUMEONDOA TATIZO??


Hivi karibuni taarifa zilizagaa katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu kufungiwa kwa video ya wimbo wa msanii snura wa Nimevurugwa kwa kile kilichoonekana kuwa ni video ambayo haiendani na maadili ya kitanzania.

Inawezekana ikawa ni kweli haiendani na maadili ya kitanzania na hivyo jamii ya kitanzania itakapoangalia inaweza kupotoka hususani watoto wadogo na wanafunzi wa shule.

Lakini najaribu kujiuliza,na pengine hata msomaji wangu utakuwa unajiuliza maswali mengi,swali mojawapo likiwa,Hii BASATA inakuwaga wapi mpaka video inatoka na kusambaa mitaani na wao kukurupuka huko waliko na kusema video imefungiwa ikiwa tayari iko katika mitandao,ma CD pamoja na maeneo mbalimbali.

Kingine cha kujiuliza,ni kweli ni kwasababu ya maadili au kuna sababu nyingine,kwani nakumbuka kuna video nyingi tu ambazo wanacheza katika mitindo hiyo ya snura na hazifungiwi,mfano mzuri ni video ya IT bata,au hata Besta kuna wimbo alikuwa katika mazingira hayo hayo na hakufungiwa!

Au kwasababu ya kile kipande cha wimbo alichoponda nchi kuyumbayumba?mtazamo tu jamani,naruhusiwa na katiba kutoa maoni yangu katika ibara ya 18(1).

PICHA ZA SNURA AKIWA KATIKA POZI MBALIMBALI

ARSENAL YAPANDA KWA MGONGO WA CHELSEA


Timu ya soka ya ligi kuu ya uingereza Arsenal maarufu kama the gunners,jana ilijikuta ikibaki kileleni mwa ligi hiyo kwa tofauti ya point mbili mbele ya manchester city na chelsea baada ya hapo jana chelsea kuifunga manchester city kwa goli moja kwa sifuri katika uwanja wa Etihad.

Gori hilo pekee la chelsea lilifungwa na mshambuliaji wake Ivanovic katika dakika ya 32 na kudumu kwa kipindi chote cha mchezo huo ambao kila timu ilitaka kushinda ili kujiwekea mazingira mazuri katika ligi hiyo ambayo imeonekana kuwa ngumu kuliko ligi zote hasa msimu huu ambapo timu hizo zimepishana kwa pengo la poit chache sana na hivyo kila timu kujitahidi kuongeza mbinu za ushindi

Katika msimamo wa ligi hiyo kwa sasa Arsenal inaongoza ikiwa na point 55,ikifuatiwa na manchester city yenye point 53 na iliyoizidi chelsea kwa magori lakini timu hizo mbili zikiwa na point sawa.

Bahati mbaya ipo kwa mabingwa watetezi wa ligi hiyo ambao wako nyuma ya vinala kwa point 15 hasa mala baada ya kupoteza mechi mwishoni mwa wiki.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA YA MECHI YA MANCHESTER CITY VS CHELSEA

NAVAS AKIJITAHIDI KUMKIMBIA MCHEZAJI WA CHELSEA


JOE KATIKA HARAKATI


GAME NGUMU YAYA TOURE




Jumatatu, 3 Februari 2014

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM KITENGO CHA HABARI WACHANGANYWA NA MITIHANI.

Wanafunzi wa chuo kikuu Dar es salaam shule ya habari na mawasiliano(SJMC)wapo katika wakati mgumu kwa sasa hasa mala baada ya kuanza kwa mitihani ya semister ya kwanza katika chuo hicho.
.
Wakizungumza na muandishi wa habari hii kwa nyakati tofauti wanafunzi wa chuo hicho walisema kuwa kila mmoja kwa sasa yuko bisy na mitihani ili kuhakikisha kuwa anajiweka katika nafasi nzuri ya kutokurudia mitihani mwezi wa tisa na kutengeneza ufaulu mzuri utakaompa unafuu katika soko la ajira hapo baadae.

Mmoja kati ya wanafunzi chuoni hapo ambae anasoma kitengo cha habari(journalism) bwana YUSUF NURU alionekana kuhangaika huku na huko katika makundi mbalimbali yaliyokuwa yanahaha kujadili somo ambalo lilitarajiwa kufanyika leo saa tano asubuhi.

Moja kati ya vitu ambavyo wanafunzi huviogopa sana ni mitihani hiyo ikifuatiwa na matokeo ya majaribio mbalimbali darasani ambayo hujumlishwa na kupata matokeo ambyo mwisho wa semister huchanganywa na matokeo ya mtihani wa mwisho na mwanafunzi anakuwa amevuna alichopanda kwa semister nzima.

Blog hii inawatakia wanafunzi hao mtihani mwema na wenye mafanikio na mwisho wa siku chuo hicho kitengeneze waandishi wazuri watakaokuwa tegemeo kwa taifa hili changa.

PICHA;WANAFUNZI WAKIWA WAMEJUMUIKA KWA UPENDO.


PICHA HII NI MOJA KATI YA PICHA ZA WHATSAPP AMBAZO WANAFUNZI WAMETUMIANA KATIKA KUNDI LAO KAMA MOJA YA UTANI NA KUPEANA MOYO.

KIKWETE ATEMBELEA MAJENGO YA BUNGE LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jakaya Mlisho Kikwete leo ametembelea na kukagua majengo ya bunge la jamhuri ambayo ujenzi wake unaendelea.

Mheshimiwa Kikwete ametembelea majengo hayo mala baada ya kutoka katika sherehe za CCM zilizofanyika mjini Mbeya jana

Majengo hayo ya bunge yanajengwa na kufanyiwa ukarabati kwaajili ya wajumbe wa Bunge la katiba linalotarajiwa kuanza hivi karibuni kwaajiri ya kujadiri rasimu ya katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Zifuatazo ni picha mbalimbali zikimuonesha rais katika ukaguzi wa majengo hayo leo;


PICHA KWA HISAN YA OTHMAN.

MWIKO WA MBEYA CITY WAVUNJWA NA YANGA

Ule mwiko wa timu iliyoko ligi kuu ya Tanzania Bara Mbeya city umevunjwa wa kutokufungwa toka kuanza kwa ligi kuu Tanzania Bara umevunjwa jana baada ya kukubali kichapo cha bao moja kwa bila kutoka kwa wapinzani wao timu ya Yanga uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Bao hilo la pekee la Yanga lilifungwa na mshambuliaji mahili Mrisho khalfan Ngasa katika dakika za mwanzoni za kipindi cha kwanza na bao hilo kudumu katika muda wote ambao mchezo huo ulifanyika.

Wakizungumza kwa furaha na muandishi wa habari hii mashabiki wa timi ya Yanga waliokuwa wamefurika uwanjani hapo walijigamba kuwa swala la Mbeya city kufungwa lilikuwa la lazima ili kujihakikishia nafasi nzuri katika kinyanganyiro hiki cha ligi kuu Tanzania Bara.

Kwa upande wao mashabiki wa Mbeya City walisema kuwa matokeo yaliyopatikana ni matokeo ya mpira wa miguu na kama inavyofahamika katika mchezo huo kuna kufungwa kutoa droo au kushinda kwa hiyo wao hawakati tamaa na wanajipanga kwa mchezo mwingine unaofuata kwakuwa matumaini yao ni kunyakua ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara.

ZIFUATAZO NI PICHA ZINAZOONESHA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA MTANANGE HUO.

PICHA ZOTE KWA HISAN YA OTHMAN