visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 26 Novemba 2014

WANYAMA AIBIWA


Maafisa wa polisi wanachunguza kisa kimoja ambapo wezi walivunja na kuingia katika nyumba ya mchezaji wa kilabu ya Southampton Victor Mugubi Wanyama nchini Uingereza na kumuibia mali yake usiku wa jumatatu.

Shati moja la kiungo wa kati wa timu ya Barcelona Andres Iniesta ,pamoja na nguo za wanamitindo kadhaa pamoja na jozi 20 za viatu ni miongoni ya vitu vilivyoibwa.

Wezi hao pia waliiba gari la mchezaji huyo aina ya Land Rover lenye thamani ya shilingi millioni 8.4 fedha za kenya,fanicha,Runinga pamoja na vifaa vyengine vya kielektroniki .

Mkenya huyo mwenye umri wa miaka 23 anaishi katika nyumba ndogo na polisi wameshangazwa kwamba majirani zake hawakuamshwa na kelele za uvunjaji huo.

Kikosi cha timu yake ya Southamptom kilikuwa kimesafiri hadi Villa ambapo bao la dakika za mwisho liliifanya mechi hiyo kuwa na sare ya 1-1.

Wanyama ameshiriki katika mechi 14 msimu huu na kufunga mabao matatu huku Southampton ikiendelea kupigania nafasi ya kufuzu katika mechi za UEFA.

Ni mchezaji aliyeuzwa kwa kitata cha juu kutoka Uskochi baada ya Celtic kumuuza kwa pauni 12.5 mnamo mwaka 2013
BBC

DADA WA ASHANTI AWATUKANA WALINZI WA AFRIKA



Kakatika picha hiyo aliyyoiweka kwenye mtandao dada huyo wa mwanamuziki Ashant alliandika maneno hayo yanayoonekana hapo chini ya picha akiiashiria kuwa walinzi hao wa mwili maarufu kama bodyguards ni wazuri lakini wanatoa harufu mbaya ukiwasogelea.

Wadau wengi wameichukulia kauli hiyo kama ni kauli ya kibaguzi ingawa mwenyewe hakujibu chochote kuhusiana na tuhuma hizo.

Ijumaa, 21 Novemba 2014

WANAWAKE WANAONYONYESHA WATOTO KULIPWA


Matokeo ya awali ya mpango wa kulipa wanawake ili kuwashawishi kunyonyesha watoto umeonesha matokeo mazuri, watafiti wameeleza.

Wakina mama katika maeneo matatu ya Derbyshire,South Yorkshire ambapo kiwango cha unyonyehsaji kiko chini kati ya asilimia 21 mpaka 29 waliahidiwa kulipwa mpaka pauni 200.

Kati ya wanawake 108 walio katika mpango huu,wanawake 37 sawa na asilimia 34 tayari wamelipwa katika kipindi cha wiki sita mpaka nane.

Wakosoaji wakiwemo madaktari wanasema mradi huu unachochea uwepo wa vitendo vya rushwa.

Mpango mwingine utafuata ambao utakua mkubwa zaidi utakaowahusisha wanawake 4,000

Tayari Wanawake 58 wamejiandikisha.

Nchini Uingereza, asilimia 51 ya wanawake kwa kipindi cha wiki sita mpaka nane, scotland kwa asilimia 38.

Takwimu ziko chini zaidi kwenye maeneo yaliyo masikini mpka kwa kiasi cha asilimia 12.

Wataalamu wa afya wanasema watoto wanatakiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita, ili kuwalinda watoto dhidi ya maradhi.

Halikadhalika tafiti zinasema kuwa kunyonyesha mtoto kunamuepusha mzazi kupata maradhi ya saratani ya matiti na Ovari.

lakini hali haiko hivyo nchini Uingereza ikilinganishwa na nchi nyingine, asilimia moja tu ya watoto nchini humo hunyonya maziwa ya mama zao kwa miezi sita

Ijumaa, 31 Oktoba 2014

HUKU Dk. Damas Ndumbaro, akiwa amekata rufaa kupinga adhabu ya kifungo cha miaka saba kujihusisha na soka ndani na nje ya nchi iliyotolewa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), amesema ataendelea kufanya kazi zake za kuwawakilisha wadau wa soka watakaohitaji huduma yake ya uwakili.
Akizungumza leo mjini Dar es Salaam, Ndumbaro alisema kuwa TFF na Kamati zake hazina mamlaka ya kumfungia kufanya kazi za uwakili, isipokuwa Jaji Mkuu wa Tanzania na serikali.
Dk Ndumbaro akiwaonyesha Waandishi wa Habari hati iliyosainiwa na klabu
Ndumbaro alisema kuwa anashangaa kuona amehukumiwa na Kamati ya Nidhamu kwa kosa la maadili na kuongeza kwamba kamati hiyo haikupaswa kusikiliza tuhuma zilizokuwa zinamkabili.
Alisema kuwa adhabu hiyo aliyopewa ni dalili za wazi za 'chuki' dhidi yake kwa sababu yeye alichokizungumza ilikuwa ni maamuzi ya klabu 12 za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambazo zilikubaliana na kumteua yeye kupitia Kampuni yake ya Uwakili ya Maleta & Ndumbaro ya jijini.
"Sikuzungumza kwa niaba yangu, nilikuwa na ridhaa ya klabu 12, isipokuwa Stand United na Coastal Union, Kamati hii inatumiwa na Jamal Malinzi, ndio kamati iliyoipa ushindi Stand United kupanda Ligi Kuu," alisema Ndumbaro.
Wakili huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba alisema kuwa alianza kuonekana ni adui mara baada ya kukataa kushiriki katika ufujaji wa fedha ambapo kwa vipindi vitatu tofauti alikataa kusaini hundi za fedha ambazo TFF iliomba kutoka kwenye Bodi ya Ligi Kuu (TPL).
Alisema kwamba kwa sasa shirikisho hilo linakabiliwa na ukata baada ya kutumia kiasi cha Dola za Marekani 696,823 bila ya kupata kibali cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambao wamezitoa kwa ajili ya udhamini wake wa timu ya Taifa (Taifa Stars).
Mbali na matumizi hayo, pia Jamal Malinzi anadaiwa kujilipa binafsi Dola za Marekani 159,140 ndio maana sasa wanaamua kufidia fedha hizo katika gharama nyingine ikiwamo makato ya Sh.1,000 kwa kila tiketi," alisema Ndumbaro.
Aliongeza kuwa anashangaa kuona TFF inaendelea kukata Sh. 1,000 katika kila tiketi za mashabiki wanaoingia uwanjani kushuhudia mechi za Ligi Kuu Bara na kutaja kiasi kilichokatwa hadi kufikia jana ni Sh. milioni 193.2 zilizotokana na mashabiki 193,257 walioingia viwanjani kushuhudia michezo ya ligi iliyoanza Septemba 20 mwaka huu.
Alisema pia anashangaa kuona rufaa yake aliyokata tangu Oktoba 21 mwaka huu haijapangiwa siku ya kusikilizwa lakini kikao cha Kamati ya Nidhamu kilichokutana kumjadili kilichukua siku mbili.
Aliongeza kuwa leo Oktoba 31 mwaka huu siku ya 10 na hakuna dalili za kusikilizwa, tutaendelea kuhesabu, mambo mengi yako katika rufaa.
Alisema kwamba yeye hajawahi kutoa siri za shirikisho na kueleza kuwa kanuni za ligi na mikataba inayoingiwa si siri.

Alhamisi, 30 Oktoba 2014

DU!!MKE AMUANDALIA MUMEWE MKOROFI CHAKULA CHA KONDOMU



Watu wangu makini mmeisikia hii kutoka BBC ya mama alieamua kummuandalia mume wake mkrofi chakula cha mipira inayotumiwa wakati wa kufanya ngono!isome hapa:

Mwanamke mmoja mwenye watoto watatu katika wilaya ya Kole nchini Uganda alimuandalia mumewe mlo wa mipira ya kondomu kufuatia ugomvi usiokwisha kati yao.

Mwanamke huyo ambaye ni mkaazi wa eneo la Arao aliripotiwa kununua paketi tatu za kondomu aina ya "Trust" kutoka duka jirani kabla ya kuzipika na kumuandalia mumewe kama chakula baada ya kurudi nyumbani akiwa amelewa chakari.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la nchini Uganda, mwanamke huyo aliikata kata mipira hiyo ya kondomu ambayo ilikuwa haijatumika katika vipande vidogo vidogo na kuvichemsha kwa muda kabla ya kuvikaanga kwa mafuta ya kupikia na viungo vingine.

Wakati mumewe alipowasili kutoka kubugia pombe katika eneo jirani la kibiashara la Odede,aliandaliwa mlo huo katika sahani tofauti moja ikiwa na mipira hiyo kama mboga na nyingine ikiwa na mkaa.

Lakini jamaa huyo alibaini njama za mkewe baada ya kuonja mlo huo na kugundua ulikuwa na ladha tofauti.

Hatua hiyo ilikuwa ikilenga kumfunza mume huyo ambaye amedaiwa kuzua ugomvi na mkewe kila anapolewa na kurudi nyumbani.

CREDIT; HABARI NA PICHA KUTOKA BBC

HII NI KALI NYINGINE!!KUFANYA MAPENZI NA WANAWAKE WENGI TIBA YA CANCER!!



Kulala na wanawake wengi kunapunguza hatari ya kupatikana na ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo,kulingana na utafiti.

Katika utafiti uliochapishwa katika jarida la saratani,Watafiti kutoka chuo kikuu cha Montreal wamebaini kwamba ikilinganishwa na wanaume walio na mpenzi mmoja katika maisha yao yote,kulala na zaidi ya wanawake 20 kunapunguza uwezekano wa kupatikana na ugonjwa huo kwa asilimia 28.

Wanaume 3,208 walishiriki katika utafiti huo ambapo kati yao Wanaume 1,590 walipatikana na ugonjwa huo kati ya Septemba mwaka 2005 na Agosti mwaka 2009.

Kwa jumla watafiti hao walibaini kwamba wanaume wenye saratani ya kibofu cha mkojo kuna uwezekano mara mbili kwa wao kuwa na watu wa familia zao wenye saratani.

Hatahivyo ushahidi unaonyesha kwamba idadi kubwa ya wapenzi wa kike miongoni mwa wanaume inapunguza tishio la ugonjwa huo.

Mwanamume anapojamiana na zaidi ya wanawake 20 katika maisha yake,tisho la kupata ugonjwa huo linapoungua kwa asilimia 28 mbali na asilimia 19 kwa aina yoyote ya ugonjwa wa saratani.

Utafiti huo pia umebaini kwamba mmoja kati ya wanaume wanne wa kiafrika hupatikana na saratani

CREDIT:PICHA NA HABARI KUTOKA BBC.

HII NAYO KALI!!MKURUGENZI WA KAMPUNI YA APPLE INAYOTENGENEZA SIMU ZA IPHONE AJITANGAZA KUWA SHOGA


Tim cook,
Mkurugenzi wa kampuni kubwa ya simu duniani ya APPLE inayotengeneza simu za IPHONE bwana TIM COOK leo ameishangaza dunia baada ya kujitangaza hadharani kuwa ni shoga.

Cook amesema kuwa amekuwa akiwaambia wafanyakazi wenzake kuhusiana na hali yake hiyo ya kimahusiano lakini hajawahi kuwa wazi hadharani na sasa ameamua kuuambia ulimwengu kuwa yeye nia shoga.

''Nimekuwa nikiwaambia wafanyakazi wenzangu na wote wanajua hali yangu ya kimahusiano lakini sijawahi kuliweka swala hili hadharani lakini naomba kuitumia nafasi hii kusema kuwa mimi ni shoga na najivunia kuwa hivyo na kumshukuru MUNGU kwa zawadi hii kubwa aliyonipa'',alisema bwana cook!! Ajabu ee!.

Jumanne, 28 Oktoba 2014

KUHUSU FEDHA ZA MUIMBAJI HARRYSONG INSTAGRAM


Muimbaji Harrisong ameesema kuwa fedha alizozionesha katika mtandao wa instagram ni za kwake na sio za kuazima kama watu wengi wanavyoendelea kusambaza uzushi huo.

Muimbaji huyo alisema kuwa kamwe hawezi kufanya ujinga wa kuazima pesa na kupiga nazo picha kwa kuwa kitendo hicho hakitakuwa na maana yoyote kwake.

AUSTRALIA YAPIGA MARUFUKU NDEGE KUTOKA NCHI ZA AFRIKA MAGHARIBI


Nchi ya Ausralia imepiga marufuku ndege zote kutoka Afrika magharibi kuingia nchini humo katika harakati za kupambana na ugonjwa hatari wa Ebola.

Akizungumza na vyombo vya habari,waziri anaehusika na maswala ya uhamiaji bwana Scott Morrison amesema kuwa hakutakuwa na visa mpya zitakazotolewa kwa wasafiri wa nchi hizo na zile ambazo ziko kwenye mchakato zitazuiwa.

Nchi ambazo zimepigwa marufuku ni pamoja na sierra leone,guinea pamoja na Liberia.

OZIL AONESHA PICHA ANAVYOENDELEA VIZURI NA MATIBABU


Mchezaji wa timu ya Arsenal Mesut Ozilleo ameonesha kuwa anaendelea vizuri na matibabu na kuonesha shukrani zake kwa timu ya Arsenal.

Hayo yamethibitika baada ya kuandika maneno haya katika ukurasa wake wa face book;
''best team! Thanks for your great support to enable my quick recovery''

HAPPY BIRTHDAY ELMINIA CREDO


Hongera sana kwa siku yako hii ya kuzaliwa na tunashukuru kwa ujumbe wako huu uliotuandikia na kuonesha shukrani zako kwetu;


''Namshukuru Mungu kwaajili ya siku yangu yakuzaliwa Siku hii ya Leo,nawashukuru wazazi na walezi Wang kwa malezi waliyonipatia,nawashukuru ndugu,jamaa na marafiki kwa upendo,faraja na ushirikiano ninaopata kutoka kwenu,Mungu awabariki;Love u all!!!!!''

PICHA ZA WATU WALIOPONA EBOLA


Hizi ni picha za baadhi ya watu ambao wameugua ebola na wakapona kabisa.

Jumapili, 26 Oktoba 2014

SALE YA TANO MFULULIZO YAMLIZA OKWI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Anord Okwi na kipa chupukizi Manyika Peter Jr, jana walimwaga machozi baada ya timu yao ya Simba kutoka sare ya bao 1-1 na Tanzania Prisons katika Uwanja wa Sokoine, mjini hapa.
Nyota hao walifanya hivyo baada ya mwamuzi wa mechi hiyo, Athumani Lazi kutoka mkoani Morogoro kupuliza filimbi ya mwisho kumaliza pambano hilo namba 33.
Kilichowaliza Okwi na Manyika Jr katika mechi hiyo, ni kuona timu yao ikiambulia sare kwa mara ya tano licha ya hiyo jana kuwa mbele katika kwa dakika 78, baada ya wao kupata bao kuongoza dakika ya nane.
Bao hilo lilifungwa na Okwi kwa mpira uliotokana na na adhabu ndogo na kwenda moja kwa moja wavuni na kumwacha kipa Mohamed Yusuph akiwa hana la kufanya.
Licha ya maafande wa Tanzania Prisons chini ya Kocha David Mwamwaja kupambana kusawazisha bao hilo, Simba walikuwa makini na kwenda mapumziko wakiwa mbele.
Kipindi cha pili maafande wa Prisons walionekana kuimarika wakifanya mashambulizi ya uhakika na kujilinda vizuri na kupata bao dakika ya 86, likifungwa na Hamis Maingo aliyeingia kipindi cha pili akiubetua mpira kwa juu wakati huo kipa Manyika Jr akiwa ametoka langoni.
Baada ya filimbi ya mwisho, ndipo Okwi alikaa chini na kuanza kulia hadi aliposaidia na wachezaji wenzake kwa kumnyanyua kama ilivyokuwa kwa Manyika Jr ambaye alifarijiwa na kipa namba moja wa timu hiyo, Ivo Mapunda.
Tangu kuanza kwa ligi hiyo msimu huu, ni sare ya tano kwa Simba kwani jana walishuka dimbani wakitoka kuvuna matokeo ya aina hiyo kwa Coastal Union, Polisi Moro, Stand Utd na Yanga.
Matokeo hayo yameifanya Simba kufikisha pointi tano katika mechi tano tangu kuanza kwa ligi hiyo Septemba 20 huku Tanzania Prisons nao wakifikisha pointi kama hizo.
Wakati Simba ikizidi kuchechemea, watani wao Yanga jana wakicheza katika Uwanja wa Kambarage, mkoani Shinyanga, jana walivuna pointi tatu katika mbio za ligi hiyo baada ya kuinyoa Stand Utd mabao 3-0, anaripoti Mwandishi Wetu Stella Ibengwe.
Yanga chini ya Mbrazil Marcio Maximo, walipata bao la kwanza dakika ya 13, likifungwa na Jaja na kudumu hadi filimbi ya mapumziko.
Kipindi cha pili, kiliendelea kuwa cha mashambulizi makali ambapo wakati Yanga wakipambana kuongeza mabao, wenyeji Stand Utd nao walikuwa wakitaka kusawazisha bao hilo.
Lakini, mtokea benchi Jerrison Tegete aliyeingia kuchukua nafasi ya Jaja, aliifungia bao la pili katika dakika ya 79 na kuamsha umati wa wapenzi na mashabiki wa Yanga waliokuwa wamejitokeza kushuhudia mechi hiyo.
Dakika ya 90, Tegete kwa mara ya pili alirejea katika nyavu za Stand Utd na kuifungia timu yake bao la tatu, hivyo kufikisha pointi 10 katika mechi tano tangu kuanza kwa ligi hiyo.
Wakati Yanga wakifikisha pointyi hizo, Stand United moja ya timu ngeni katika ligi hiyo ikicheza kwa mara ya kwanza, wameendelea kupotea katika ligi hiyo wakiambulia pointi tano katika mechi tano.
Nayo Azam FC ikicheza katika Uwanja wake wa Azam Complex, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, jana walichapwa bao 1-0 na maafande wa JKT Ruvu ya Pwani, anaripoti Mwandishi Wetu Salum Mkandemba.
Bao la JKT Ruvu chini ya kocha wake Fred Felix Minziro, lilifungwa dakika ya 45 na mtokea benchi, Samuel Kamuntu akichukua nafasi ya Idd Mbaga aliyeumia na kuwainua mashabiki wa timu yake iliyoshuka dimbani ikitoka kuwafunga Tanzania Prisons katika mechi iliyopita.
Kamuntu alifunga bao hilo akiunganisha krosi murua ya Najimu Magulu kutoka wingi ya kulia, maafande hao wakisawazisha makosa ya dakika ya 40, waliposhindwa kuitumia vizuri nafasi baada ya Magulu kushindwa kuitendea haki pasi ya Ally Bilali.
Kipindi cha kwanza kilikuwa cha soka ya nguvu huku pengo la Kipre Tchetche kwa upande wa Azam FC, likionekana bayana kwa upande wa Azam FC kwani Didier Kavumbagu alionekana mara nyingi kukosa sapoti.
Katika kipindi cha pili, Azam waliongeza kasi kwa lengo la kusawazisha bao hilo, lakini maafande wa JKT Ruvu nao wakipambana kulinda na kushambulia na hadi mwisho, JKT Ruvu walifanikiwa kuondoka na ushindi wa bao 1-0.
Kwa ushindi huo, JKT Ruvu wamefikisha pointi saba baada ya kucheza mechi tano huku mabingwa watetezi, Azam FC wakibaki na pointi zao 10. Kwa upande mwingine, ni kipigo cha kwanza kwa Azam katika Ligi Kuu Tanzania bara, baada ya mechi 37 zilizopita.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa mechi kadhaa kwa timu kuzidi kupigania pointi kujiongezea mtaji katika kuuwania ubingwa wa ligi hiyo unaoshikiliwa na Azam tangu April 19, 2014.

TANZANIA DAIMA

Jumamosi, 25 Oktoba 2014

HALMASHAURI YA WILAYA YA BAGAMOYO TABIA HII INASABABISHA WANAFUNZI KUFELI

Wilaya ya Bagamoyo ni moja kati ya wilaya za mkoa wa pwani zinazofanya vibaya katika matokeo ya kidato cha nne na hivyo kusababisha wanafunzi kutangatanga na wengine kuishia kupata ujauzito na kuolewa.

Zimekuwa zikisemwa sababu nyingi zinazochangia wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao na nyingi ya sababu hizo zimekuwa ni lawama kwa upande wa serikali kuu na walimu huku sababu ndogondogo ambazo zinahusiana moja kwa moja na wanafunzi wenyewe na wazazi zikiachwa na hivyo kuendelea kurudisha nyuma ufanisi wa wanafunzi.

Moja kati ya sababu hizo ni hii inayofanywa na serikali ya halmashauri ya wilaya ya bagamoyo ya kutoa vibali kwa watu kufanya sherehe zao za harusi au nyingine usiku katikati ya makazi ya watu huku ukipigwa muziki mzito ambao husababisha kelele na kero kwa majirani.

Mbaya zaidi ni kwamba wanafunzi wamekuwa wakitoka katika nyumba zao na kwenda kucheza rusha roho katika sherehe hizo na kuacha jukumu lao la kujisomea na hasa ukizingatia kuwa hawawezi tena kusoma kutokana na kelele zinazoendelea.

Kama hiyo haitoshi sherehe hizo zinakuwa ni fulsa kwa vijana waharibifu kuwarubuni wanafunzi wa kike na kuwaingiza katika vitendo vya kufanya mapenzi wakiwa bado wanafunzi.

Kinachokera zaidi ni kwamba mbali na Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo kutokukemea tabia hizo imekuwa namba moja kutoa vibari vya kuruhusu watu kufanya sherehe hizo katika makazi ya watu huku wakijua fika kuwa kuna kumbi maalum kwaajiri ya kufanyia sherehe hizo na sio katika makazi ya watu.

Ombi langu kwa serikali ya Halmashauri ya Bagamoyo na serikali za halmashauri zote nchini ni kuwa tusishirikiane kuendelea kulitengeneza bomu hili ambalo tunaona kabisa kuwa mwisho wake sio mzuri.

Hawa tunaowaita sasa hivi watoto wa uswahilini tukumbuke kuwa ni wengi sana na miaka kadhaa ijayo tutakuwa tumezalisha kundi kubwa sana la watu wasiokuwa na elimu na ambalo bado litakuwa na mahitaji na hivyo kusababisha vitendo vya wizi na ujambazi kuongezeka.

Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo mnapaswa kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake mbadilike na kutimiza majukumu yenu ipasavyo bila kutengeneza mbonu za kujikinga huku mkijua fika kuwa kizazi hiki na vijavyo vinategemea sana busara na fikra sahihi za ki uongozi kutoka kwenu.

Matumaini yangu ni kuwa wahusika mala baada ya kuwakumbusha hapa mtachukua hatua stahiki badala ya kuanza kuwa na mawazo hasi ya kutafuta mchawi.

MIGIRO AKIRI SERIKALI HAIWEZI KUWAPA AJIRA VIJANA

Dar es Salaam.Wakati Serikali ikitupiwa lawama kwa kushindwa kumaliza tatizo la ajira kwa vijana nchini, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha-Rose Migiro amekiri kuwa Serikali haina uwezo wa kutoa ajira kwa vijana wote wanaohitimu masomo nchini.
Dk Migiro aliyasema hayo jana wakati alipofanya ziara katika Shule ya Sheria iliyopo jijini hapa na kuwataka vijana wanaomaliza vyuo kuweka kuweka mawazo kwenye upande wa pili wa ajira.
“Uchumi wa nchi yetu unajengwa na sekta binafsi katika maeneo mbalimbali…linaweza kuwa eneo la uchumi, biashara au taaluma kwa hivyo nategemea kwamba baadhi yenu mtaweka macho kwenye sekta binafsi…ni jambo zuri kwa sababu hivi sasa Serikali yetu, tofauti na sisi tuliyokuwa tunasoma haina uwezo wa kutoa ajira kwa wahitimu wote,” alikiri Dk Migiro.
Aliongeza: “Lakini wakati mtakapo kuwa kwenye sekta binafsi lazima mkumbuke kurejesha sehemu ya taaluma mnayopata hapa kwa jamii inayotuzunguka kwa kutoa huduma za kisheria pale zinapohitajika”
Alisema kuwa, serikali inategemea shule hiyo itazalisha makada wenye malezi bora na wenye ufanisi mzuri wa taaluma ya sheria ambao wataweza kumudu ushindani uliyopo kwenye fani hiyo kutoka kwa wanasheria wenzao wanaotoka nje ya nchi.
“Tunaamini kwamba mafunzo kwa vitendo wanayopata wanafunzi hawa kwa kipindi cha mwaka mmoja baada ya kuhitimu shahada ya sheria katika vyuo mbalimbali nchini yatawajengea uwezo mzuri na ufanisi wa kuwa mawakili wazuri,”alisema Dk Migiro.
Akizungumzia changamoto ya gharama za mafunzo, waziri huyo alisema kuwa serikali imekwisha peleka mswada bungeni ili sheria inayoruhusu wanafunzi wa elimu ya juu kunufaika na mkopo iweze kuongezwa sehemu ya wanafunzi wa shule ya sheria pia.
“Muswada ukifanyiwa kazi tunategemea ndani ya miaka miwili wanafunzi wanaosoma shule ya sheria nao wataanza kupata mikopo. Nimesikia kuna baadhi wanashindwa kuendelea na shule ya sheria kutokana na changamoto za kifedha hivyo tunashughulikia hilo tatizo,”alisema na kuongeza
“Licha ya kuwa mkopo huo unaweza usitosheleze kwa asilimia mia, lakini utasadia…wazazi na walezi nao ningeomba wajitahidi kupunguza gharama za matumizi yasiyo na manufaa kwa watoto wao na badala yake wajitahidi kuwekeza zaidi kwenye elimu.”
MWANANCHI

Ijumaa, 24 Oktoba 2014

CHID BENZI AKAMATWA NA POLISI AKIWANA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE DAR ES SALAAM

Msanii wa muziki wa kizazi kipya anaefahamika kwa jina maarufu la CHID BENZ amekamatwa na polisi baada ya kukutwa na madawa ya kulevya katika mfuko wa shati lake alipokuwa anataka kupanda ndege kuelekea jijini mbeya kwaajiri ya Instagram party.

Kwa mujibu wa taarifa za kipolisi Chid alikamatwa wakati anafanyiwa ukaguzi wa maungo yake kabla ya kusafiri katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Taarifa hizo zinadai kuwa Chid amekutwa na kete 14 za madawa ya kulevya ambayo bado yanafanyiwa uchunguzi kubaini ni aina gani ya madawa na misokoto miwili ya bange ambayo mwenyewe Chid amekiri kuwa ni yake na kusema kuwa ni kweli anatumia madawa hayo na anashangaa kwa nini aliyaweka katika mfuko wa shati.

Pamoja na madawa hayo Chid pia amekamatwa na vifaa mbalimbali vinavyotumika katika uvutaji wa dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na kigae na kijiko kilichokatwa.

Taarifa zinadokeza kuwa Chid anaendelea kufanyiwa uchunguzi na utakapokamilika basi atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazomkabiri.

Katika safari hiyo Chid alikuwa na msanii mwenzake Shetta ambaye amefanikiwa kusafiri kuelekea katika tamasha hilo la istagram party wakate mwenzake Chid akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi.

KIKWETE ATAMANI MUDA WA KUSTAAFU URAIS UFIKE

RAIS Jakaya Kikwete amesema mfumo unaotumika Tanzania ambako Rais anatumikia nafasi ya uongozi kwa muhula wa miaka mitano na si zaidi ya miaka 10 ni mzuri na unaovutia kwa sababu unaiwezesha nchi kupata fikra na mawazo mapya.
Aidha, Rais Kikwete amesema, anaamini Tanzania itapata Rais bora zaidi kuliko yeye, atayeiwezesha Tanzania kusonga mbele kwa kasi kubwa zaidi.
Rais Kikwete pia amesema, ana hamu kumaliza muda wake wa uongozi ili arudi kijijini kushughulika na wajukuu wake na mifugo yake. Rais Kikwete ametoa kauli hiyo mjini Beijing, China, wakati akizungumza na mabalozi wa Afrika wanaoziwakilisha nchi zao katika China.
Mkutano huo uliofanyika kwenye Nyumba ya Kufikia Wageni wa Serikali ya China ya Diaoyutai, ulikuwa shughuli ya kwanza ya Rais Kikwete katika ziara yake rasmi ya siku sita ya Jamhuri ya Watu wa China ambako amealikwa na Rais Xi Jinping.
Wakati wa maswali na majibu, Balozi Sola Onadipe, Naibu Balozi wa Nigeria katika China, alishangazwa na kauli ya Rais Kikwete kuwa anatamani amalize muda wake wa uongozi ili astaafu na kusema kuwa lingekuwa jambo la maana kwa Afrika kama viongozi wengine wangekuwa na mawazo ya namna hiyo ya kuheshimu Katiba za nchi zao na kung’atuka kwenye uongozi muda wao unapowadia.
Rais Kikwete amemwambia Balozi huyo:”Ni kweli naona kama muda hauendi kwa kasi ya kutosha ili niweze kuwa raia wa kawaida na nipate muda wa kuchunga ng’ombe na mbuzi wangu na nilime mananasi yangu kwa nafasi ya kutosha. Lakini Mheshimiwa Balozi usishangazwe na utayari wangu kuondoka katika uongozi.”
“Kwanza utaratibu huu wa miaka mitano ama miaka 10 ni utaratibu wa Kikatiba, ni jambo lililoko katika Katiba yetu na hatuna kishawishi cha kulibadilisha. Pili, kazi hii ya Urais ni kazi ngumu sana. Kwa hakika, binafsi nawaonea gele sana wenye nguvu na ubavu wa kutaka kubakia kwenye kazi hii kwa miaka mingi. Pengine wana nguvu zaidi kuliko mimi,”amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“ Lakini pia kuna uzuri katika mfumo huu wa kwetu kwa sababu kila baada ya miaka mitano na hata kama ni baada ya kila miaka kumi, anaingia mtu mwingine madarakani akiwa na fikra mpya na mawazo mapya.”
“Mfumo huu ni mfumo unaoniridhisha sana na wala hakuna kinachonishawishi nibakie katika madaraka zaidi ya muda wangu kikatiba. Nina hakika, nchi yetu itapata kiongozi mwingine, bora kuliko hata mimi, kuongoza vizuri nchi yetu.”
Rais Kikwete pia amesema kuwa si busara pia kwa kiongozi kuwasikiliza wale wanaoshauri wakisema kuwa akiondoka madarakani nchi itavurugika.
“Kwa hakika, hawa wanatetea maslahi yao tu wakisema kuwa ukiondoka wewe madarakani, wao hawatakuwa tena mabalozi ama mawaziri ama nafasi nyingine yoyote.”
mwananchi

Jumatano, 22 Oktoba 2014

MWANAFALSAFA ASEMA MUZIKI ANAOFANYA DIAMOND NI WA KIKI KWAHIYO NI KAWAIDA KUZOMEWA

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya maarufu kama Mwana Falsafa amesema kuwa Muziki aliozoea kuufanya Diamond ni muziki wa kiki kwahiyo ajue kuwa kuna kiki nzuri na kiki mbaya na kumtaka kuwa tayari kwa pande zote mbili kwakuwa ndio aina ya muziki aliouchagua.

Mwanafalsafa aliyasema hayo wakati akihojiwa kwenye kipindi cha xxl cha clouds fm na kutakiwa kuliongelea tukio lililompata msanii mwenzake wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul au Diamond plantinumz kama anavyofahamika na wengi.

Akiongea kwa mifano Mwanafalsafa alisema,tukio kama hilo liliwahi kuwakuta kipindi kile kukiwa na ushindani kati ya kundi lao la EAST COAST na lile la TMK WANAUME FAMILY ambapo alisema kuwa waliwahi kuzomewa na mashabiki wa kundi hilo na yeye binafsi ilimtetemesha sana na ilimjengea woga katika kazi hiyo ya muziki.

FA aliongeza kuwa inawezekana kabisa kukawa na mipango kutoka upande wa pili wa upinzani kukodisha watu ili wamzomee au kumbooo mpinzani na hivyo kumkatisha tamaa lakini katika hali ya kawaida msanii hatakiwi kukata tamaa kutokana na matukio hayo kwasababu hutokea kama ajari tu!.

Akizungumzia swala la wasanii kuwa na bifu Mwanafalsafa alisema kuwa kama wasanii husika wanajielewa basi bifu kati yao wanaweza kuitumia kutengeneza pesa na mambo mengine ya kibiashara lakini kwa msanii asiekomaa huichukulia kama personal na kuishia kutengeneza chuki ambazo hazina tija.

MENEJA WA DIAMOND AKAMATWA SAKATA LA KUVAA SARE ZA JWTZ,NEY NAE MATATANI

Diamond Platnumz, Nay wa Mitego na wasanii wengine waliovaa sare za jeshi kwenye show ya Fiesta Jumamosi iliyopita wapo matatani. Wasanii hao wamepewa amri na jeshi la polisi kuzirudisha wao wenyewe sare hizo kwenye kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kuna taarifa kuwa meneja wa Diamond, Babutale alikuwa akishikiliwa na polisi kuanzia jana japo tayari ameshatoka.
Nay wa Mitego amesema kuwa hata yeye anashangaa kuona jinsi mambo yalivyobadilika.
“Limekuwa tatizo kubwa sana,”amesema Nay.
“Kuna watu tu wajinga wanachochea hivi vitu ilimradi tu wote wawili mimi na Diamond tumeshapewa warning, tunatakiwa polisi kurudisha zile nguo na kupeleka tu vitu vya watu, tutazipeleka.”
“Babu Tale alikamatwa tangu jana, yupo polisi, tutajua nini cha kufanya kwa sababu nimeona Diamond naye alikuwa ananipigia kwahiyo sijajua watu wamempa ushauri gani, lakini hili suala linaisha tu. Unajua hatujafanyia uhalifu, tulikuwa kazini sawa maybe inawezekana tuna makosa lakisi sio zile nguo zote zilikuwa ni za jeshi, kwahiyo tutajua tu chakufanya tutapata tu jawabu,”amesisitiza Nay.
Pia Nay alizungumzia taarifa iliyotolewa ikidai kuwa walipata kibali cha kutumia nguo za JWTZ kwenye shughuli ile.“Ndiyo maana nakwambia kuna vitu vipo katikati hapa sisi wenyewe hatuelewi ni nini kinaendelea,”amesema.

Jumanne, 21 Oktoba 2014

KUNDI LA DIAMOND LAONGELEA TUKIO LA MSANII HUYO KUZOMEWA

Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale amesema haoni kama wameathirika na kundi la watu waliomzomea msanii huyo wakati akitumbuiza Jumamosi hii kwenye show ya Serengeti Fiesta, Leaders Club jijini Dar es Salaam.
Tale amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa walikuwa na taarifa kuhusu mpango huo hata kabla ya show na hivyo walijiandaa. “Tulikuwa tumemjenga kisaikolojia, kwahiyo hiyo ni sehemu ya kazi na mashabiki ingekuwa wanapiga kelele kama tumekosea show kweli, lakini sio hivyo. Show ilikuwa sawa,” amesema Tale.
“Tunachojua sisi msanii wetu anafanya vizuri na sasa hivi nguvu zetu tumeelekeza katika tuzo. Wananchi wakaze kumpigia kula katika tuzo Channel O na MTV, sie sasa hivi tunasonga mbele, tunachojua chema chajiuza, kibaya chajitembeza.”

Jumamosi, 18 Oktoba 2014

WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAMU KUACHIWA HURU

Serikali ya Nigeria na wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, wamefikia makubaliano ya usitishaji mapigano na kuachiliwa huru wanafunzi wa kike wanaoshikiliwa na kundi hilo.
Hayo yameelezwa na mkuu wa vikosi vya jeshi la Nigeria, Meja Jenerali Alex Sabundu Badeh na Hassan Tukur, Katibu wa ikulu ya rais ya nchi hiyo na mshauri wa karibu Rais Goodluck Jonathan na kuongeza kuwa, kwa mujibu wa makubaliano hayo, kundi hilo litatakiwa kuwaachilia huru wasichana hao zaidi ya 200 liliowateka nyara tarehe 14 Februari mwaka huu huko Borno.
Inaelezwa kuwa pande hizo mbili zimefikia makubaliano hayo Ijumaa ya jana, baada ya mazungumzo yaliyofanyika nchini Saudi Arabia ambayo yalijumuisha Rais wa Chad, Idris Deby na maafisa wa ngazi ya juu kutoka Cameroon.
Wakati huo huo jeshi la Cameroon limetangaza kuua wanamgambo 107 wa Boko Haram, katika mapigano yaliyojiri kati ya pande mbili huko kaskazini mwa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo, mapigano hayo yalitokea asubuhi ya siku ya Jumatano miji ya Amchide na Limani iliyoko mpakani kati ya nchi hiyo na Nigeria.
Wizara hiyo imeongeza kuwa, katika mapigano hayo yaliyoibuka baada ya wanamgambo wa Boko Haram kuvuka mpaka na kuingia nchini Cameroon, yalipelekea kuuawa askari wanane na raia saba wa nchi hiyo.
BBC

Ijumaa, 17 Oktoba 2014

DAVIDO AZUILIWA SERENGETI FIESTA

Video: Mahakama ya Kisutu yamzuia Davido kuperform katika tamasha la Fiesta
posted4 hours ago by admin
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam imemzuia msanii kutoka Nigeria, Adedeji Adelek maarufu kama ‘Davido’ kuperform katika tamasha la Fiesta linaloandaliwa na Clouds Fm na Prime Promotion, October 18,2014.
Amri hiyo imetolewa jana (October 17) na hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu , mheshimiwa D. Kisoka kufuatia maombi ya dharura yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Times Fm Radio na Times Fm Promotion.
Times Fm Radio na Times Fm Promotion walipeleka maombi ya dharura mahakamani hapo wakiitaka mahakama kumzuia msanii huyo kuperform katika tamasha hilo kwa kuwa licha ya BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) kukataa kutoa kibali cha msanii huyo kwa maelezo kuwa tayari alikuwa ameshachukuliwa kibali cha kuperform nchini November 1 kwenye tamasha lililoandaliwa na Times Fm Radio, Clouds Fm na Prime Times Promotion waliendelea na taratibu zote bila kujali zuio hilo la BASATA.
Times Fm Radio na Times Fm Promotion waliiomba mahakama kuidhinisha madai yao dhidi ya Clouds Fm, Prime Promotion na mkurugenzi wa kampuni inayomsimamia Davido, HKN Music.
Madai hayo ni pamoja na kulipwa fidia ya gharama na usumbufu waliosababishiwa na walalamikiwa kadiri Mahakama itakavyoona inafaa.
Mahakama imetoa amri kuwa msanii huyo amezuiwa kufanya onesho hilo October 18,2014 hadi pale ufumbuzi wa kesi hiyo utakapopatikana mhakamani hapo.
Awali, Davido alisikika katika matangazo ya Times Fm Radio akieleza kuwa atakuja Tanzania November 1 kwa ajili ya kufanya onesho linaloandaliwa na kituo hicho cha radio

Times fm.

Jumatano, 15 Oktoba 2014

IDADI YA WALIOKUFA KWA EBOLA YAFIKIA 4000

Afisaa mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na janga la Ebola, anasema kuwa dunia inajikokota katika vita vyake dhidi ya Ebola huku maelfu ya watu wakiwa katika hatari ya kuambiukizwa ugonjwa huo ifikapo Disemba mwakani.
Afisaa huyo Anthony Banbury ameambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwamba kasi ya maambukizi ya Ebola ni ya kutisha na kwamba, huenda ikashindikana kudhibiti maambukizi.
Wakati huohuo, idadi ya watu waliofariki kutokana na Ebola tangu janga hilo kuanza imefika 4,447 , wengi wakiwa katika kanda ya Afrika Magharibi.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la afya duniani, WHO.
Naibu mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Bruce Aylward, pia alisema huenda watu 10,000 wakaambukizwa ugonjwa huo kila wiki kwa kipindi cha miezi miwili ikiwa juhuudi za kimataifa haziongezwa kasi kupambana na ugonjwa huo.
Lakini kiwango cha maambukizi mapya katika baadhi ya maeneo kimepungua.
Sierra Leone, Liberia na Guinea, ndizo nhi zilizoathirika zaidi kutokana na ugonjwa huo tangu kuanza kwake.
Katika matukio mengine:
Uingereza imeanza kuwakagua na kuwachunguza watu katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Heathrow
Daktari wa kikosio cha wanajeshi wa kulinda amani wa Siera Leone alipatikana na Ebola mjini Freetown.
Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa kutoka Sudan alifariki nchini Ujerumani baada ya kuambukizwa Ebola nchini Liberia.
Mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg amesema yeye na mkewe Priscilla Chan, watachanga dola milioni 25 za kusiadia vita dhidi ya Ebola.
Muuguzi mmoja wa Uhispania, alikuwa mtu wa kwanza kuugua ugonjwa huo nchini Hispania na angali yuko hali mahututi, ingawa madaktari wanasema ana dalili za hali yake kuimarika.
BBC

Jumamosi, 11 Oktoba 2014

HOW lindaikeji.blogspot.com BROKEN AND THEN RESTORED AGAIN

MUKEBEZI BLOG/(DOUBLE LL KIDS): Linda Ikeji’s blog was taken down by Google a few ...: Linda Ikeji’s blog was taken down by Google a few days ago due to claims of copyright infringement. Why were there claims against her in th...
Linda Ikeji’s blog was taken down by Google a few days ago due to claims of copyright infringement.
Why were there claims against her in the first place? It’s implied that some hackers under the direction of one Mr. Aye Dee were to blame.
Linda Ikeji and Mr. Aye Dee
According to Linda’s latest post on the matter, the real reason was very, very personal. Allegedly, the shocking reason for this whole hoopla is because of a scorned friend who got upset that he was being ignored.
It turns out that Mr. Aye Dee actually used to be Linda's confidant that she would seek advice from in matters pertaining to her blog. She knew him under a different alias as Alex of 1976AD and was just as shocked as everyone else when she found out that he was really Mr. Aye Dee.
Linda states that they've been conversing for years, but when she got extremely busy with blogging and flooded with thousands of emails it became a bit difficult to keep up with the conversation.
Text convo between Ikeji and Mr. Aye Dee
Text convo between Ikeji and Mr. Aye Dee
He claims that he reached out to her for over a year straight, but all his attempts failed.
He later on assumed that Linda had allowed all her fame and opportunities to go straight to her head. He thought she no longer cared for him. So he decided to get some buddies of his to come together to take down her blog. They were determined to get Google, who owns Blogspot, to remove her blog because of plagiarism and copyright claims.
It’s insinuated from the convo that Aye Dee realizes that Linda hadn’t been ignoring him, but was actually just busy. In his own way he apologizes for his wrong-doing and promises that she will bounce back bigger and better than ever before because of this.
Credit:lindaikeji.blogspot.com

DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA UPOFU

Watafiti nchini Australia wanadai kwamba dawa inayotumiwa kuongeza nguvu za kiume VIAGRA husababisha upofu baada ya mda mrefu.
Kulingana na Watafiti hao kutoka Australia, kiungo fulani katika dawa hiyo inayotumiwa kukabiliana na ukosefu wa nguvu za kiume,huathiri uwezo wa kuona miongoni mwa wanaume ambao wana ugonjwa wa macho.
Kulingana na gazeti la Nation nchini kenya,Madaktari nchini Australia wamebaini kwamba kiungo fulani katika dawa hiyo kinaweza kusababisha upofu miongoni mwa wanaume wenye tatizo la ugonjwa wa macho.
Vilevile inadaiwa kuwa dawa hiyo pia inaweza kuwaathiri watumiaji ambao wanaona vizuri.
Utafiti huo uliofanywa katika panya,ulibaini kwamba hata watu wasio na ugonjwa wa macho wanaweza kuathirika.
Credit:BBC

Ijumaa, 10 Oktoba 2014

BASI ALILOPANDA BABA LEVO LAPATA AJARI AKIELEKEA MPANDA

BreakingNews, stori kubwa
Baba LevoNi saa tisa kasoro mchana Msanii wa bongofleva Baba Levo anapiga simu na kuongea kwa tabu kwenye usikivu ulio mdogo na kusema kwamba amepata ajali kwenye pori karibu na eneo linaitwa Uluwila akiwa anatokea Tabora kwenda Mpanda.
Alikua kwenye Basi liitwaloAMambapo ghafla wakiwa kwenye kona ilitokea Coaster ikiwa na abiria ambayo dereva wake alikua akikwepa barabara mbovu hivyo ikabidi ahamie kwenye upande wa pili wa barabara ambako ndiko lilikua linapita basi la kina Baba Levo ambalo hakuliona sababu ni kwenye kona.
Dereva wa basi la kina Baba Levo ilibidi ahame upande wake ili ahamie kwenye upande wa magari yanayopanda ambao ndio upande sahihi wa ile Coaster kupita ambapo juhudi zake hazikufanikiwa kwani wote walikua kwenye spidi na yule dereva wa Coaster alihama kwenye ule upande baada ya kuona atagongana uso kwa uso na basi la kina Baba Levo ila bahati mbaya wakawa wote wamejikuta upande mmoja na wakagongana uso kwa uso.
Mwenye makosa anatajwa kuwa ni mwenye Coaster ambapo pamoja na Baba Levo kuumia usoni na mwilini kwa kuchanwachanwa na vioo vya mbele vilivyopasuka kwenye basi, ameweza kuona kuna baadhi ya watu wamefariki ambapo kati yao ni waliopasuka vichwa na shingo.
Dereva wa basi la kina Baba Levo hajaumia sana wala basi halijaumia sana, Coaster ndio imefumuka upande wa juu wote na kuharibika sehemu nyingine pia huku kilichosababisha Baba Levo kuumia ni kwamba alikua amekaa pale juu ya Injini ya Basi kwenye kigodoro kutokana na basi hilo kujaa.
Baba levo anajisikia vibaya kiasi na kwa sasa yuko na wenzake kama 20 pamoja na Askari mwenye silaha waliekua pamoja kwenye Basi…. wanatembea kutafuta kijiji chenye network ili kuomba msaada manake baadhi ya abiria wamebanwa kwenye hiyo Coaster na hawajatolewa.
Credit:millardayo

VITAMBULISHO VYA TAIFA VYAGEUKA KERO TANZANIA

Shughuli ya upatikanaji wa vitambulisho vya uraia nchini Tanzania imegeuka kuwa kero kwa wananchi badala ya faraja waliyoisubiri kwa hamu.
Kumekuwa na msongamano wa watu katika maeneo mbali mbali wanaoitwa kupokea vitambulisho vyao bila mafanikio.
Kwa Zaidi ya miaka miwili sasa tangu vitambulisho hivyo vianze kuandaliwa na hatimaye kutolewa, kumekuwa na changamoto upande wa uhakiki taarifa na uhaba wa vifaa walivyopewa NIDA na serikali ya Tanzania kama vitendea kazi.
Vifaa vilivyotarajiwa kwa zoezi zima la usajili na utoaji wa vitambulisho nchini Tanzania ni elfu tano lakini kwa sasa vilivyopo ni miatano tu kwa nchi nzima yenye mikoa Zaidi ya 26.
Msongamano wa raia wa Tanzania mbele ya kituo cha kupokea kadi za utambulisho wa raia,bila kujali mwanamke ama mwanaume mzee au kijana ,mjamzito ama mzazi wote mchapalo pasi na tafrija, macho mlangoni kusubiria nani atatoka wa kwanza kwenye kadhia ya kukaribiana kwa saa moja hadi saa mbili,mradi kitambulisho kitoke na maisha yaendelee.
Credit:BBC

VITAMBULISHO VYA TAIFA VYAGEUKA KERO TANZANIA


Alhamisi, 9 Oktoba 2014

NAFASI ZA KAZI MWANANCHI COMMUNICATION LTD

MWANANCHI COMMUNICATIONS LIMITED PUBLISHERS OF READING TANZANIA NEWS PAPERS, MWANANCHI, MWANASPORTI, AND THE CITIZEN ARE LOOKING FOR MOTIVATED AND HIGHLY EXPERIENCED INDIVIDUALS TO FILL THE POSITION OF:-
LEGAL AND ADMINISTRATIVE OFFICER
POSITION DESCRIPTION:
Main Responsibilities:
• Draft, interpret, advice on, review Mwananchi
performance contracts/agreements
• Advise on legal and regulatory matters.
• Liaise with the regulators to ensure compliance with regulatory matters and with external lawyers on legal and litigation
matters.
• Provide legal advice to employees on
company related issues of a legal nature.
• Handle legal administrative matters.
• Arrange and take minutes of the departmental meetings and follow up on the implementation of decisions taken therein with the respective staff and prepare action
reports .
• Liaise with insurance brokers/companies;
follow up on claims settlement and ensure
timely renewals of policies.
• Prepare and update schedules of all leases,
rents, rates, company properties contracts/ agreements and licenses and ensure their renewals and payments where necessary.
• Ensure that leases and tenancy agreements are renewed, updated, are paid for and running and that trading licenses are current.
Qualifications and Experience:
An hours bachelor’s Degree in Law (LLB)
Legal practice
Must possess a legal practicing certificate
Two years of professional experience with a. minimum of one year as an Advocate in legal practice or as an in-house counsel in a busy corporate entity.
APPLICATION INSTRUCTIONS:
Human Resources Manager Mwananchi Communications Ltd P. O. Box 19154,
Dar es Salaam
Interested and suitably qualified individuals should forward their applications enclosing a detailed CV and copies of professional certificates, and a day time telephone contact
NB: Only short listed candidates will be contacted.
SOURCE: THE GUARDIAN OF 9OCTOBER 2014

NAFASI ZA KAZI

TANZANIA NATIONAL ROADS AGENCY
08th October, 2014.
VACANC IES ANNOUNCEMENT
The Regional Manager’s Office TANROADS – SIMIYU, On behalf of Chief Executive, TANROADS, intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill vacant posts on specific duty short - term contract within the Region for Portable Weighbridge.
1.0 SHIFT INCHARGE (1POST)
A. Qualifications for shift in-charge;
· Age: Not below 35 and not above 40 years of age
· Educational minimum qualification: Holder of 1st Degree in any professional.
· Computer Literate
· Must be fluent in Kiswahili and English languages;
· Must be a Tanzanian Citizen.
B. Duties and Responsibility;
· Enforcement of Road Traffic axle Load Control by the use of Weighbridge scale devices;
· Overall supervision of shift activities.
· Carrying out activities as described in the Roads Traffic (Maximum Weigh of Vehicles) Regulations, 2001. The activities include the following:
· Record all necessary particulars regarding the motor vehicle being weighed
· Observe good customer care, dignity and integrity
· Report all matters to the Regional Manager
· Any other duties as may be assigned by Regional Manager.
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 40 years old,
ii. Applicants must attach an up-to-date Curriculum Vitae (CV) having reliable contacts, i.e postal address, e-mail and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
v. Applicants who were already working at any weighbridge station with TANROADS will not be considered
vi. FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
vii. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii. Applicants should indicate three referees with their reliable contacts.
ix. Certificates from foreign Universities should be certified by The Tanzania Commission for Universities (TCU).
x. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xi. Only short listed candidates will be informed on a date for interview
Note: Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
xii. Deadline for submission is 19th October, 2014 at 16:30 Hrs
xiii. Application letters should be handwritten in English Language
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED/E-MAILED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS ACCEPTABLE:
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
P. O. Box 389,
SIMIYU.
E-mail: tanroadssimiyu@gmail.com
Tell No: 028 2700245
Fax No: 028 2700256
==========
VACANCIES ANNOUNCEMENT
08th October, 2014.
The Regional Manager’s Office TANROADS – SIMIYU, On behalf of Chief Executive, TANROADS, intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill vacant posts on specific duty short - term contract within the Region for Portable Weighbridge.
2.0 WEIGHBRIDGE OPERATOR (2 POSTS)
A. Qualifications for Weighbridge Operator;
· Age: Not below 25 and not above 35 years of age
· Educational minimum qualification: Holder of Full Technician Certificate (FTC)/Diploma in Civil Mechanical or Electrical Engineering;
· Computer Literate (at least Certificate in Computer Applications);
· Must be fluent in Kiswahili and English languages;
· Must be a Tanzanian Citizen.
B. Duties and Responsibility;
· Enforcement of Road Traffic axle Load Control by the use of Weighbridge scale devices;
· Weigh Motor Vehicles of Gross Vehicle Weight (GVW) ≥ 3,500kg plying on our Public Roads;
· Carrying out activities as described in the Roads Traffic (Maximum Weigh of Vehicles) Regulations, 2001. The activities include the following:
· Measure physical dimensions of motor Vehicle or any load being carried on the motor vehicle, and in case of non-compliance with vehicle dimension limits, the transporter should be caused to seek for a special permit;
· Record all necessary particulars regarding the motor vehicle being weighed
· For trucks carrying abnormal load with special permit, the Weighbridge Operator shall ascertain compliance to the permit. Any discrepancy should be reported to the Weighbridge In- charge for appropriate action
· Observe good customer care, dignity and integrity
· Report all matters to the Shift in-charge
· Any other duties as may be assigned by Regional Manager.
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 40 years old,
ii. Applicants must attach an up-to-date Curriculum Vitae (CV) having reliable contacts, i.e postal address, e-mail and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
v. Applicants who were already working at any weighbridge station with TANROADS will not be considered
vi. FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
vii. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii. Applicants should indicate three referees with their reliable contacts.
ix. Certificates from foreign Universities should be certified by The Tanzania Commission for Universities (TCU).
x. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xi. Only short listed candidates will be informed on a date for interview
Note: Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
xii. Deadline for submission is 19th October, 2014 at 16:30 Hrs
xiii. Application letters should be handwritten in English Language
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED/E-MAILED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS ACCEPTABLE:
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
P. O. Box 389,
SIMIYU.
E-mail: tanroadssimiyu@gmail.com
Tell No: 028 2700245
Fax No: 028 2700256
=========
VACANCIES ANNOUNCEMENT
08th October, 2014.
The Regional Manager’s Office TANROADS – SIMIYU, On behalf of Chief Executive, TANROADS, intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill vacant posts on specific duty short - term contract within the Region for Portable Weighbridge.
3.0 WEIGHBRIDGE CASHIER (1 P0STS)
A. Qualifications for Weighbridge Cashier;
· Age: Not below 25 and not above 35 years of age
· Educational minimum qualification: Diploma in account;
· Computer Literate (at least Certificate in Computer Applications);
· Must be fluent in Kiswahili and English languages;
· Must be a Tanzanian Citizen.
B. Duties and Responsibility;
· Collecting and Banking all weigh bridge charges (fees) according to weighbridge report form;
· Seeking current USD exchange rates issued by Bank of Tanzania for case of imposing charges that are equivalent to Tanzania shillings and keep exchange rate records;
· Timely filling all necessary records timely and keep register area neat:
· Report all matters to the Shift in charge;
· Performing other duties as may be assigned from time to time by Shift in Charge and / or Regional Manager.
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 40 years old,
ii. Applicants must attach an up-to-date Curriculum Vitae (CV) having reliable contacts, i.e postal address, e-mail and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
v. Applicants who were already working at any weighbridge station with TANROADS will not be considered
vi. FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
vii. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii. Applicants should indicate three referees with their reliable contacts.
ix. Certificates from foreign Universities should be certified by The Tanzania Commission for Universities (TCU).
x. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xi. Only short listed candidates will be informed on a date for interview
Note: Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
xii. Deadline for submission is 19th October, 2014 at 16:30 Hrs
xiii. Application letters should be handwritten in English Language
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED/E-MAILED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS ACCEPTABLE:
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
P. O. Box 389,
SIMIYU.
E-mail: tanroadssimiyu@gmail.com
Tell No: 028 2700245
Fax No: 028 2700256
==========
VACANCIES ANNOUNCEMENT
08th October, 2014.
The Regional Manager’s Office TANROADS – SIMIYU, On behalf of Chief Executive, TANROADS, intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill vacant posts on specific duty short - term contract within the Region for Portable Weighbridge.
4.0 WEIGHBRIDGE ATTENDANTS (2 POSTS)
Key qualifications for the Weigh bridge Station Attendant;
· Minimum Education Qualification is Ordinary Secondary Education (Higher Qualifications will be of added Advantageous;
· Computer Literate (at least Certificate in Computer Applications);
· Must be fluent in both written and spoken Kiswahili and English languages
· Must be a Tanzanian Citizen;
· Age limit of not above 35 years.
Duties and Responsibilities:
Weighbridge Station Attendant should Observe Good Customer Care, Dignity and Integrity to Carrying out all activities as described in the Road Traffic (Maximum Weigh of Vehicles) Regulations, 2001 including the following duties:-
· Assisting weighbridge operator in weighing vehicle;
· Direct vehicle to the weighing scale
· Performing such other related duties as may be assigned by senior staff.
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 40 years old,
ii. Applicants must attach an up-to-date Curriculum Vitae (CV) having reliable contacts, i.e postal address, e-mail and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
v. Applicants who were already working at any weighbridge station with TANROADS will not be considered
vi. FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
vii. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii. Applicants should indicate three referees with their reliable contacts.
ix. Certificates from foreign Universities should be certified by The Tanzania Commission for Universities (TCU).
x. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xi. Only short listed candidates will be informed on a date for interview
Note: Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
xii. Deadline for submission is 19th October, 2014 at 16:30 Hrs
xiii. Application letters should be handwritten in English Language
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED/E-MAILED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS ACCEPTABLE:
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
P. O. Box 389,
SIMIYU.
E-mail: tanroadssimiyu@gmail.com
Tell No: 028 2700245
Fax No: 028 2700256
==========
VACANCIES ANNOUNCEMENT
08th October, 2014.
The Regional Manager’s Office TANROADS – SIMIYU, On behalf of Chief Executive, TANROADS, intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill vacant posts on specific duty short - term contract within the Region for Portable Weighbridge.
5.0 DRIVER ( 1 post)
A. Qualifications for Driver;
· Age: Not below 25 and not above 35 years of age
· Educational minimum qualification: Ordinary Secondary Education; High qualification will have additional advantages;
· Must have driving licence CLASS D
· Must be fluent in Kiswahili and English languages;
· Must be a Tanzanian Citizen.
B. Duties and Responsibility;
· To ensure that the vehicle is in good condition in mechanical and cleanness;
· To preserve vehicle safety
· To check and report the maintenance requirement;
· Observe good customer care, dignity and integrity
· Report all matters to the Shift in - charge
NB: GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 40 years old,
ii. Applicants must attach an up-to-date Curriculum Vitae (CV) having reliable contacts, i.e postal address, e-mail and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
v. Applicants who were already working at any weighbridge station with TANROADS will not be considered
vi. FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
vii. Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii. Applicants should indicate three referees with their reliable contacts.
ix. Certificates from foreign Universities should be certified by The Tanzania Commission for Universities (TCU).
x. Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xi. Only short listed candidates will be informed on a date for interview
Note: Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
xii. Deadline for submission is 19th October, 2014 at 16:30 Hrs
xiii. Application letters should be handwritten in English Language
APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED/E-MAILED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS ACCEPTABLE:
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
P. O. Box 389,
SIMIYU.
E-mail: tanroadssimiyu@gmail.com
Tell No: 028 2700245
Fax No: 028 2700256
==========

Jumatano, 8 Oktoba 2014

BABA AMCHINJA MWANAE NA KUMTOBOA TUMBO SENGEREMA

Baba mzazi mkazi wa Sengerema anadaiwa kumuua mwanaye wa miaka minne kwa kumchinja koromeo na kumchoma kwa kisu kwenye kitovu na utumbo kutoka nje.
Mzazi huyo anadaiwa kufanya mauaji hayo juzi alfajiri baada ya kumchinja aliuchoma kwa kisu mwili wa mtoto huyo sehemu mbalimbali ikiwemo masikioni na kifuani.
Gazeti la MWANANCHI ambalo lilikua shuhuda limedai baada ya kufanya kitendo hicho alianza kufukuza wananchi waliokusanyika eneo hilo kwa kuwatishia kuwachoma na kisu.
Hata hivyo mtuhumiwa huyo alizidiwa nguvu na wananchi na kuanza kumshambuliwa kwa kipigo hadi alipookolewa na Mwenyekiti wa mtaa.
Mama mzazi wa watoto hao alisema kabla ya kutengana na mumewe huyo alizaa nae watoto watatu na kwamba ameshangazwa kupata taarifa za mwanaye kuuawa na baba yake.
Jeshi la Polisi linamshikilia kwa uchunguzi huku likisubiri taarifa ya hospitali kuhusu utimamu wa akili yake.

ETI WANAUME WAFUPI WANAFAA ZAIDI KWENYE NDOA KULIKO WAREFU

Wanaume ambao ni wafupi kwa kimo mara nyingi wanasifika kuwa waume bora kuliko wanaume warefu.
Pia inaarifiwa huwa na busara zaidi kufidia kimo chao, amekiri Adam Gopnik, mwanamme mmoja wenye umbo dogo.
Wiki kadhaa zilizopita, wana soshologia wawili kutoka Chuo Kikuu cha New York, walichapisha waraka mrefu ulioangalizia maisha ya watu wafupi.
Utafiti wao ulizua mjadala mkali kutoka kwa kile kinachoweza kusemekana kuwa jamii ya wanaume wenye kimo kifupi.
Waandishi wa waraka huo wa maswala ya kijamii unaashiria kwamba wanaume wenye haiba ya kuvutia mara nyingi hupendelewa katika maisha yao hivyo wanaripotiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na zaidi ya mpenzi mmoja.
Hata hivyo, hitimisho la waraka huo, pindi mtu anapoupitia, unashangaza. Ni kwamba, watu wafupi wana ndoa za kudumu zaidi.
Wanafanya hayo, katika mazingira magumu wakiwa katika umri tofauti na kipato tofauti, na wanayafanya hayo wakiwa na wanawake wafupi ambao wanawaoa, na wakati mwengine na hata wanawake warefu wanaokutana nao.
Wanaume wafupi wanaoa kuchelewa, lakini pindi wanapooa, wanadumu katika ndoa kwa muda mrefu, na kwa kiwango cha sayansi ya kijamii, angalau wanakuwa na furaha.
Kuna sababu zinazoonyesha kwa nini wanaume wafupi wanadumu kwenye ndoa.
Nazo ni, wanaume wafupi wanaonyesha kukata tamaa. Wanaume wafupi wanaishi katika ulimwengu wa wanaume warefu na wanajua kila fursa inayopatikana, ni bora kuidhibiti.
Hali ya kukata tamaa ndio inayowafanya wanaume wafupi kuwa wanaume bora kwa wake zao. Watafiti hao pia walisema kuwa wanaume wafupi hukimbilia kufanya kila kitu kuwafurahisha wapendwa wao wakati wanume warefu hilo halliwajalishi.
Moja wapo ya ufumbuzi wa ripoti hiyo pia ni kwamba wanaume wafupi wanafanya kazi chache za nyumbani wanapokuwa kwenye ndoa kuliko wanaume warefu, ingawa utafiti pia unaonyesha kwa wanaume wenye kimo kirefu, aina ya kazi zao za nyumbani inatofautiana.
Kwa maana nyengine, wanaume wafupi hawafiki juu ya makabati. Wanaume wafupi hawadumu kwenye ndoa kwa sababu ya kutaka kuridhisha, bali wanadumu kwenye ndoa kwa sababu wanataka kuonekana.
Utafitio huu kama ulivyosoma hapo awali umeua mjadala mkali lakini pindi mtu anaposoma utafiti wao kinachojitokeza zaidi ni kuwa wanaume wafupi wanakuwa na ndoa za kudumu.
Hii ni licha ya mazingira magumu wanayokabiliwa nayo katika ndoa zao na hufanya hivyo na wake wafupi waliowaoa lakini pia na wanawake warefu wanaokuwa wamewaoa.
Utafiti huo unahitimika kwa kusema wanaume wafupi hawana kasi ya kuoa lakini wanapooa wao hudumu katika ndoa zao.
Chanzo: BBC

FILAMU ILIYOKUWA INADHALILISHA UKATOLIKI IMETIA HASARA YA 30 MIL

Muigizaji wa filamu Blandina Chagula aka Johari amesema pamoja na kusikitishwa kutokana na bodi ya filamu nchini kuizua filamu ya ‘Sister Marry’ isitoke, amekula hasara kubwa.
Johari amesema kuwa maandalizi ya filamu hiyo yalighalimu shilingi milioni 30.
“Unajua inauma sana, tumeshindwa kutetea filamu ya ‘Sister Marry’ kutokana na madai eti tumedhalilisha dini. Ina maana hawataki tuzungumzie maisha halisi kwenye filamu zetu?
"Mimi binafsi imeniumiza sana. Ile filamu imegharimu zaidi ya milioni 30, hebu angalia, Halafu inafungiwa ili isitoke kabisa!
"Kinachonisikitisha ni kwamba serikali yetu inashindwa kuangalia sisi tunavumbua baadhi ya maovu ya watu ambayo wanayafanya ili kuelimisha jamii.
"Kwahiyo imefungiwa na kukatazwa isitoke kabisa kwa sababu kuna mambo ya ukweli ambayo tumeyaonyesha.
"Tumefanya kila njia mpaka sasa hivi tumeshindwa, kwahiyo filamu ya Sister Marry haitatoka tena,”amesema Johari.

MISS TANZANIA YARUHUSIWA KUENDELEA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu,jijini Dar es Salaam, jana iliamuru mashindano ya urembo Tanzania yaliyopangwa kufanyika Oktoba 11, mwaka huu kuendelea baada ya kutupilia mbali maombi ya dharura yaliyowasilishwa na Prashant Patel dhidi ya Hashimu Lundenga ya kuzuia kuendelea kuendesha kinyang'anyiro hicho kwa madai ya kukiuka mkataba wa makubaliano yao.
Kadhalika mahakama hiyo imesema maombi ya hati ya dharura yaliyowasilishwa na Patel hayana mashiko ya kisheria na kwamba kuzuia kufanyika mashindano hayo ambayo wadhamini mbalimbali wamewekeza fedha zao itasababisha mgongano wa kimaslahi.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi Frank Moshi baada ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili kuhusu maombi hayo ya dharura ya kuzuia mashindano hayo kufanyika Oktoba 11, mwaka huu.
Hakimu Moshi alisema mlalamikaji amefungua kesi mahakamani hapo pamoja na maombi ya hati ya dharura akiitaka mahakama yake kuzuia mashindano kufanyika kutokana na mlalamikiwa kuvunja haki dhidi ya mwanzilishi mwenzake Patel.
Alisema Patel kupitia hoja za maombi yake, amedai kuwa Lundenga alivunja mkataba huo kwa kufanya mawasiliano moja kwa moja na mawakala bila kumshirikisha.
Hata hivyo, mahakama bila kuacha shaka imeona hakuna sababu za msingi katika hati hiyo ya kusababisha mashindano hayo yasifanyike na kwamba hayawezi kuathiri kesi ya msingi iliyofunguliwa na mlalamikaji huyo.
“Mahakama imeona hakuna sababu ya kuzuia mashindano hayo kwa sababu wadhamini na washiriki wametumia gharama zao na kwamba kwa kufanya hivyo kutasababisha mgongano wa kimaslahi” alisema Hakimu Moshi wakati akitupilia mbali hati hiyo ya dharula.
Akifafanua zaidi alisema hati ya dharura ya mlalamikaji haina mashiko kisheria kwa sababu kesi yake ya msingi ipo mahakamani na kwamba haina uhusiano na mashindano yatakayofanyika Oktoba 11, mwaka huu.
Mapema juzi, mahakama hiyo ilitupilia mbali pingamizi la awali la Lundenga lililotaka hati hiyo ya dharura kutupilia mbali.

HALIMA MDEE APATA DHAMANA

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na wenzake 8 leo wamepata dhamana katika Mahakama ya Kisutu, Dar. Kesi yao kutajwa tena Oktoba 21, 2014.
Siku ya jana washtakiwa hao walipanda kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Kaluyenda na kusomewa mashtaka mawili na Wakili wa Serikali Mkuu, Kangola aliwataja washtakiwa kuwa ni Mbunge wa Kawe, Mdee, Rose Moshi, Penina Peter, Anna Linjewile, Mwanne Kassim, Sophia Fanuel, Edward Julius, Martha Mtiko na Beatus Mmari.
Mdee na wenzake hao wanashitakiwa kwa makosa mawili la kwanza washtakiwa wote wanadaiwa Oktoba 4 mwaka huu, Mtaa wa Ufipa wilayani Kinondoni, walikaidi amri ya Ofisa wa Polisi SP Emmanuel Tillf iliyowataka watawanyike.
Shtaka la pili washtakiwa wote wanadaiwa Oktoba 4, mwaka huu, maeneo ya mtaa wa ufipa jijini Dar es Salaam wakiwa na lengo moja walikusanyika kinyume na sheria wakitaka kwenda ofisi ya rais.

WATUMISHI MAFIA WAHUKUMIWA KWA UFISADI

Mafia. Mahakama ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani imewatia hatiani na kuwahukumu kifungo cha miaka minne jela au faini ya Sh3 milioni watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia baada ya kuridhika wametenda kosa la ubadhirifu wa Sh7.5 milioni zilizokusudiwa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Watumishi hao watatu ni William Kimaro aliyekuwa ofisa utumishi, Geofrey Kiwelu (mweka hazina) na Hatibu Kwao Amanzi aliyekuwa mtunza fedha.
Kila mmoja alitakiwa kulipa fedha hizo au kutumikia adhabu hiyo.
Akisoma hukumu hiyo, hakimu mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mafia, Hassan Makube alimtia hatiani Geofrey Kiwelu kwa kosa jingine la kuharibu nyaraka kinyume na kifungu cha 109 cha sheria ya kanuni za adhabu na kumhukumu kwenda jela miaka mitatu au faini ya Sh1 milioni.
Hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa na makosa 12, iliwaona hawana hatia na kuwaachia huru watumishi wengine watatu ambao ni William Zakaria Shimwela, Lusasi na ofisa mipango, Brenden Oswin Kachenje.
Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, John Sang’wa aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa waliotiwa hatiani ili iwe fundisho kwa watumishi wengine.
Mwananchi.

Jumatatu, 6 Oktoba 2014

MWALIMU APEWA UJAUZITO NA MWANAFUNZI WAKE

WAKATI ikiwa imezoeleka kuwa baadhi ya walimu wa kiume huwarubuni wanafunzi wao wa kike na hata kuwaharibia kabisa ndoto zao za kielimu kutokana na kuwapa ujauzito, hali imekuwa tofauti mkoani Rukwa ambako mwanafunzi wa Kidato cha Pili anadaiwa kumzalisha mwalimu wake.
Mwanafunzi huyo aliyemzalisha mwalimu wake ana umri wa miaka 17, wakati mwalimu huyo anayefundisha katika Shule ya Sekondari ya Umma ya Nkasi, iliyopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, Rukwa, ana umri wa miaka 25.
Tukio hilo linalotajwa kuwa la kwanza kutokea wilayani hapa, limekuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Nkasi na wilaya jirani.
Hata hivyo, kwa wanafunzi, wamekuwa wakimpongeza mwenzao kwa kujaliwa kupata mtoto katika umri wake huo mdogo, huku mzazi mwenzake akiwa na uhakika wa maisha kutokana na kuwa ni mtumishi serikalini.
Imeelezwa kuwa licha ya tukio hilo, mwalimu huyo aliyezaa na mwanafunzi wake bado anaendelea na masomo shuleni hapo, huku `mzazi’ huyo wa kiume akifundishwa na mzazi mwenzake.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Namanyere hivi karibuni, Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkasi mjini Namanyere ambayo ni ya mchanganyiko ya umma, Amiamie Nanga alisema mwalimu huyo alianza kazi shuleni hapo ikiwa ni mara yake ya kwanza kufundisha baada ya kuhitimu mafunzo ya ualimu chuoni.
“Yameshatokea, lakini haileti picha nzuri sana, lakini mimi nina uzoefu mkubwa na wakazi wa mwambao wa Ziwa Tanganyika, kwao si ajabu kuwa na uhusiano na watu waliowazidi umri, iwe kwa mtoto wa kike au wa kiume, wote ni sawa tu…
“Lakini katika kisa hiki, inaonesha walimu sasa wanapoteza haiba ya ualimu. Hii kazi ina miiko na maadili yake …kwa mwalimu huyu hii ni ajira yake ya kwanza, nikimaanisha ni kituo chake cha kwanza cha kazi tangu ahitimu masomo yake…”alisema.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema hakuna kosa kwa mwalimu huyo wa kike kwa kuwa tayari ni mtu mzima.
“Isitoshe katika kisa hiki ni nadra kumpata mlalamikaji … Mwalimu mwenyewe huyu wa kike hawezi kuwa tayari kujidhalilisha kuwa amebakwa, yalikuwa maamuzi yake.”
Aliongeza kuwa, kwa mwalimu huyo kupata ujauzito wa mwanafunzi wake hakuwezi kuathiri ajira yake, tofauti na mwalimu wa kiume akimpatia ujauzito mwanafunzi wake wa kike ambaye huathirika kwa kukatisha masomo.
Jitihada za kumpata mwalimu huyo wa kike na mwanafunzi huyo zimegonga mwamba baada ya watu wao wa karibu kumweleza mwandishi kuwa hawako tayari kuuzungumzia mkasa huo.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliohojiwa na mwandishi wa habari hizi kwa masharti ya kutoandikwa majina yao kwa hofu ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu shuleni hapo, pamoja na kukiri kutambua uhusiano baina ya mwanafunzi mwenzao na mwalimu wao, lakini walisema hivi sasa mwalimu huyo amesitisha uhusiano na mwenzao na kuanzisha uhusiano mpya na mwalimu mwenzao.
Walisema pamoja na mambo mengine ni kama mwanafunzi mwenzao ameathirika kisaikolojia baada ya ‘kupinduliwa’ na mwalimu wake wa kiume ambaye kwa sasa ndiye baba mlezi wa mtoto.
“Huyu mwalimu wa kike sisi sasa tunamwita shemeji yetu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwenzetu… penzi lao lilikolea hadi sasa ameweza kumzalia mtoto huyo…, lakini kwa sasa inavyoelezwa ni kwamba penzi limehamia kwa mwalimu mwenzake,“alisema mmoja wao.
Baadhi ya watu wa karibu na mwanafunzi huyo wanakiri kuwa mwanafunzi huyo hana uwezo wa kifedha kumudu kumpatia malezi stahiki mtoto wake huyo, hivyo hata mzazi mwenzake alipoanza uhusiano na mwalimu mwenzake hakuwa na jinsi, bali kukubaliana na matokeo.
“Usiniandike jina, sisi tunashauri mwalimu huyo wa kike na mpenzi wake huyo wa kiume ambaye ni mwalimu mwenzake wahamishiwe shule nyingine kwa sababu kama kioo katika jamii wameteleza kwa kiasi kikubwa na watashindwa kuwajenga na kuwalea wanafunzi wao kimaadili.
“Isitoshe tunajiuliza sheria hapa inasemaje maana kama angekuwa ni mwalimu wa kiume amempatia mwanafunzi wake wa kike ujauzito angeshitakiwa na kufikishwa mahakamani na pengine kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka 30 jela, sasa kwa hili sheria inasemaje?”Alihoji.
Baadhi ya wazazi mkoani hapa waliohojiwa na mwandishi kwa nyakati tofauti wameelezea kushangazwa na tukio hilo, na hasa kwa jinsi mwalimu alivyoshindwa kujizuia `kujiachia’ kimapenzi kwa mwanafunzi wake.
Credit: Habarileo

HOUSE GIRL AIBA MILION 2 NA LAKI 6 NA KUTOROKA

MSICHANA anayefanya kazi za ndani katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, anadaiwa kuiba Sh milioni 2.6 mali ya mwajiri wake.
Inadaiwa kuwa siku ya tukio msichana huyo baada ya kuiba fedha hizo, aliruka ukuta wa nyumba na kutokomea kusikojulikana.
Mwajiri wa mfanyakazi huyo, Shujaa Baruti alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 2, mwaka huu saa 3 asubuhi, kwenye Mtaa wa Zaire, Kata ya Endiamtu.
Baruti alimtaja mfanyakazi huyo wa ndani kuwa ni Jacquelin Kimario (18) mwenyeji wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, ambaye aliiba fedha hizo na kuruka ukuta wa nyumba na kukimbia na fedha hizo.
Alisema msichana huyo alipoiba fedha hizo alitoroka kwa kupanda pikipiki ili akapande gari aina ya Toyota DCM kuelekea jijini Arusha, lakini baadhi ya watu walimkamata na kumkuta akiwa na fedha hizo.
“Mimi nimemsamehe na siwezi kumchukulia hatua yoyote huyu msichana baada ya kuniibia fedha zangu ila nafanya utaratibu wa kumrudisha nyumbani kwao Rombo, kwani siwezi kuishi na mtu mwenye tabia hii,”alisema Baruti.
Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo balozi wa nyumba 10, Maulid Kimolo alisema ni jambo la kushangaza kwa msichana kuiba Sh milioni 2.6 na wametaka jamii kuwa makini na wafanyakazi wa ndani.
Naye msichana huyo Jacquelin alikiri kuiba fedha hizo na kusema alipitiwa na shetani na kwamba alitarajia kuishi vizuri na familia hiyo hivyo anaomba msamaha kwa kufanya tukio hilo.

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA BIASHARA

1. Thaminisha bidhaa unazo uza
Iwe biashara ndogo au kubwa bidha unazouza ni muhimu ziwe zenye ubora na muonekano mzuri utakaomvutia mteja.Watu hupenda vitu vizuri, bora na vinavyodumu hivyo ni vema utengeneze bidha zenye ubora na thamani“A good businessman serves quality products to his customers.’’
2. Fanya biashara ya kipekee
Fikiri na kuwa mbunifu katika kubuni na kuibua biashara mpya. Mfano kama mahali unapotaka kufanya biashara kuna M-PESA, AIRTEL MONEY, maduka ya nguo, show room ya vitu vya makazini na majumbani au biashara nyingine maarufu. Ikiwa mahali pa biashara kuna mzunguko wa watu wengi na kuna mazingira ya kupata faida nzuri unaweza kufanya biashara kama wanazofanya wengine lakini bado una kila sababu ya kuongeza biashara nyingine kwa kubuni na kuibua biashara mpya tofauti na za wafanyabiashara wengine. Kufanya hivyo utaweza kuwa mfanyabiashara wa kipekee kwa kuwa na huduma nyingi ambazo watu huhitaji kuhudumiwa. Moja ya siri ya kuongeza wateja katika biashara yako ni kuwa na huduma nyingi anazohitaji mteja. Kuwa mjanja kwa kujua wateja wako wanataka nini ili uweze kuwasogezea huduma karibu.
3. Pata ushauri kwa watu waliofanikiwa kibiashara
Unapokuwa katika wakati mgumu wa kutatua matatizo yako ya kibiashara au unapokuwa na utata katika kufanya maamuzi sahihi ya namna ya kuanza biashara ni vizuri utafute ushauri kutoka kwa watu ambao tayari wamefanikiwa katika biashara kama yako. Pia unaweza kutafuta watu wa kukufundisha jinsi ya kufanya biashara yani“Business Mentors”ambao watakusaidia kupata ujuzi sahihi na kukupatia maarifa kuhusu biashara yako.
4. Uza bidhaa zako kwa bei inayokubalika na wengi
Wateja hupenda kununua vitu kwaBEI POA!hivyo ni muhimu kujua utauza bidha zako kwa bei kiasi gani. Hapa si maanishi uuze bidha kwa bei rahisi bali uzingatie bei ambayo wateja wengi wanaweza kukidhi.
Mfano; Unataka kufanya biashara ya kuuza keki, gharama ulizotumia kutengeneza na kuandaa keki ni shilingi 8,500/= kwa keki moja badala ya kutaka faida kubwa kwa kuuza shilingi 20,000/= unaweza kuuza kwa shilingi 13,500/= ambayo utapata faida ya shilingi 5,000/= mathalan vilevile utapata wateja wengi na kuuza keki nyingi kuliko kuuza kwa bei kubwa ambayo utapata wateja kidogo.
5. Tangaza biashara yako
Biashara ni matangazo hivyo ukitaka biashara yako ikue kwa kupata wateja wengi huna budi kuitangaza ili watu waifahamu. Siku hizi kuna njia nyingi za kutangaza biashara ikiwemo kupitia wavuti (website / blog) , radio, runinga au hata mabango. Kumbuka tumia maneno mazuri ya kuvutia na kushawishi wateja.
6. Jiamini na usikate tamaa katika biashara
Kuna wakati unapoanza biashara mambo huwa mabaya hivyo ni vema ujiamini na utafakari ni wapi umekosea au ni nini cha kufanya ili uboreshe biashara yako. Wakati mwingine unapoanzisha biashara inachukua muda watu kujua unauza nini hivyo swala la muda wa watu kujua biashara yako nalo ni jambo la kuzingatia. Hakuna mafanikio ya haraka hivyo uvumilivu na ukakamavu wako ni muhimu sana katika kukuza biashara yako. Kumbuka usikae na kusubiri sana watu waifahamu biashara yako, weka na zako bidii katika kuongeza na kupanua mtandao wa wateja wako.
7. Fanya biashara uipendayo
Inaaminika kuwa ikiwa mtu atafanya kazi aipendayo basi ataifanya kwa uhodari na utashi wake kuweza kupata mafanikio makubwa, swala hili ni muhimu katika kuamua ni biashara gani unapenda kuifanya. Mfano kama wewe umesomea fani ya uhandisi wa majengo ni vema ukafanya biashara kwa kuanzisha biashara yako ya mambo ya ujenzi. Kama unapenda kupika fungua mgahawa au fanya kazi inayohusiana na fani unayopenda. Maendeleo na mafanikio makubwa ya kazi yeyote ile huletwa kwa kufanya kazi unayoiridhia na kuipenda.
Hayo ni mambo machache na ya kawaida ya kuzingatia katika biashara yako, kuwa na ndoto kubwa ya kufanikiwa kibiashara ni vizuri lakini pia penda kujua mengi kuhusu mahusiano ya biashara yako na wateja wako kwani biashara ni watu hivyo kuwa makini kwa kila hatua unayopiga kibiashara ili kuepuka hasara.

Jumapili, 5 Oktoba 2014

AJIUA KWA MOTO KISA WIVU WA MAPENZI

MKAZI mmoja wa kijiji cha Malolwa wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Ndikile Sunguli (38) amejichoma ndani ya nyumba hadi kufa baada ya kumjeruhi mke wake katika ugomvi unaoaminika ni wa mapenzi.
Tukio hilo la kutisha lilitokea Septemba 29, 2014 majira ya saa tano usiku katika kijiji cha Mlolwa.
Imeelezwa kuwa Sunguli alirudi kutoka matembezini akiwa amelewa huku akipiga makelele, alipofika nyumbani kwake alianza malumbano na mke wake huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kufanya mapenzi nje ya ndoa.
Kamanda wa polisi mkoani Rukwa Jacob Mwaluanda alisema kuwa wakati ugomvi ukiendelea Sunguli alichukua kisu na kumchoma mkewe wake ubavuni na kumjeruhi.
Kamanda alisema kuwa katika harakati za kujiokoa mama huyo alianguka nje ya nyumba yao na kuzirai, hali inayodhaniwa ilisababisha mume kudhani ameua na kujifungia ndani na kuwasha moto akiwa ndani.
Alisema kutokana na nyumba hiyo kuezekwa kwa nyasi ilishika moto kwa kasi na juhudi za majirani kumuokoa ziligonga mwamba kutokana na kujifungia.
Kamanda Mwaluvanda alisema hali ya majeruhi inaendelea vizuri kwani alikimbizwa kituo cha afya Mpui baada ya tukio hilo.

Ijumaa, 3 Oktoba 2014

WANAJESHI NA POLISI WATWANGANA RISASI TARIME

Watu 12 wamejeruhiwa wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi baina ya askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Kikosi 128 KJ cha Nyandoto na Polisi wa Kituo cha Stendi wilayani Tarime mkoani Mara.
Hatua hiyo imekuja wakati wanajeshi hao walipokuwa wakijaribu kumchukua askari mwenzao aliyekamatwa na Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani kwa kuendesha pikipiki bila kuwa na kofia ngumu.
Mashambulizi hayo ya kurushiana risasi na kutwangana ngumi na mateke yalitokea juzi saa 12 jioni katika Kituo cha Polisi Stendi.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime, Bernard Makonyo alisema amepokea majeruhi 10, kati ya hao wawili ni askari wa JWTZ, polisi saba na raia mmoja. Alisema majeruhi tisa wameruhusiwa na mwingine kupelekwa Hospitali ya Shirati kwa matibabu zaidi.
Dk Makonyo aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Aloyce Filbert (24) aliyepigwa risasi mguu wa kulia, Deodatus Dominic (26) aliyejeruhiwa puani na wote ni askari wa JWTZ.
Wengine ni askari polisi saba ambao ni Makoye Katula (26), Sylvester Michael (31), Salum Omary (44), Abdallah Halifa (24), Joel Msabila (25), Ally Juma (27) na Deogratius Tryphon (32) na raia Hamza Jumanne (33) aliyepigwa risasi mguu wa kushoto ambaye alipelekwa Hospitali ya Shitari, Rorya kwa matibabu.
Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Ndalama Salumu anadaiwa kujeruhiwa kwa kupigwa katika vurumai hizo huku mwananchi mwingine, David Kisaro (20) akijeruhiwa kwa bomu jichoni. Alitibiwa katika Zahanati ya Tarime.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Benedict Mambosasa alisema mwanajeshi aliyekamatwa alifanya makosa kwani baada ya kukamatwa na kuombwa kwenda kituo cha polisi, alikaidi.
Mambosasa alisema mwanajeshi huyo licha ya kukiuka taratibu, aliwatolea lugha za matusi polisi jambo lililowalazimu kumkamata kwa nguvu, ndipo wanajeshi wenzake walipoingilia kati na kusababisha kutokea kwa majibishano ya risasi za moto. Hata hivyo, alisema hakuna aliyejeruhiwa.
Alisema wanajeshi watatu ambao hawakutajwa majina, wamekamatwa na polisi kwa kuvunja utaratibu wa usalama.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, amelaani kitendo hicho cha kurushiana risasi za moto hewani akisema ni cha utovu wa nidhamu na maadili ya kazi ya jeshi na kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema wananchi Tarime wameshangazwa kwa kitendo kilichofanywa na walinda usalama hao, wakisema si cha kinidhamu huku wakisema kilikwamisha shughuli zao kwa muda kwa kuhofia usalama wa maisha yao.
Mkazi wa Tarime, Joseph Samson amesema kitendo hicho kimewashangaza sana wananchi.

ASKARI ALIYETOROSHA MWANAFUNZI ASHTAKIWA

Na Girdon Kalulunga
Taarifa kutoka mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, zinaarifu kuwa jeshi la polisi nchini limemkamata na kumfikisha katika mahakama ya kijeshi askari wake Pc.Godlisen anayetuhumiwa kumtumikisha katika vitendo vya ngono mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari Okaoni iliyopo wilaya ya Moshi.
Habari zinasema kuwa, askari huyo ambaye Septemba 21 mwaka huu alimfungia kwenye nyumba ya kulala wageni mjini moshi mwanafunzi huyo na baadaye wawili hao kupata ajali mbaya ya pikipiki wakijaribu kutoroka, aliumia kwenye moja ya bega lake na hivyo kushindwa kupelekwa kwenye mahakama ya kijeshi.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita, pamoja na kukiri kuwa wameanzisha uchunguzi kuhusiana na tuhuma hizo, alikataa kuweka wazi kama askari huyo amefunguliwa mashitaka ya kijeshi.
Kamanda Koka aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, jeshi la polisi linafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo na kwamba kama itabainika, askari huyo atachukuliwa hatua za kinidhamu kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.
Pamoja na jeshi hilo kumfungulia mashitaka ya kijeshi askari huyo, taarifa kutoka kwa mmoja wa wazazi wa mwanafunzi huyo zinadai kuwa, kuna juhudi za makusudi zinafanywa na askari wa jeshi hilo kutaka kukwamisha mashitaka ya kijeshi dhidi ya askari huyo.
Taarifa zinadai kuwa, polisi wa kituo kikuu cha polisi mjini Moshi, wanajenga ushawishi kwa wazazi wa mwanafunzi huyo kutaka kulimaliza suala hilo kienyeji.

SHEREHE YA KUZALIWA YA DIAMOND IMEGHARIMU 28MILION

Diamond Platnumz ni msanii ambaye yuko kwenye level za juu kwenye kila kitu kwa sasa, upande wa muziki na hata aina ya maisha anayoishi. Hilo linaweza kuthibitishwa na gharama zilizotumika kufanikisha sherehe yake ya kutimiza miaka 25 iliyofanyika jana October 2, pamoja na zawadi aliyopewa na uongozi wake.
Meneja wa Diamond, Babu Tale amesema party hiyo iligharimu shilingi milioni 28 na kuwataja waliohusika kuigharamia.
“Event tumefanya wenyewe lakini mwisho wa siku Diamond yupo karibu na watu wengi na makampuni mengi”.Tale ameiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm.“Coca cola kama Coca Cola ndio walichukua nafasi kubwa kuifanya ile event sababu wao ni balozi wao….ilikuwa gharama inagharimu milioni 28 kwa sisi wenyewe watoto wa paka tusingeweza kuitoa kirahisi hiyo hela.”
Zawadi kubwa aliyopata Diamond kwenye birthday yake ni gari aina ya BMW X6, ambayo alipewa na uongozi wake unaoundwa na Babu Tale, Said Fela na Salam. Tale ameelezea jinsi walivyoweza kupata pesa za kununua gari hiyo.
“Sasa hivi Diamond anafanya vizuri na tulikuwa tunamwambia Diamond kwamba kuna contract tukisaini tutakupa zawadi, as in kwamba management haitachukua percent ya hiyo contract hiyo pesa itaenda kwenye kukuchukulia wewe zawadi, akasema nyie bana mlivyokuwa watata sijui kama mtakubali.”
Aliendelea,
“Tulivyotoka South Africa tukawa kuna contract tume confirm kusaini, tulivyosaini ile contract ile pesa ambayo ilitakiwa pasenti yote ije kwetu sisi mimi, Fela na Salam yote tukasema tumchukulie zawadi….ni shilingi ya kitanzania milioni 90”.

Alhamisi, 2 Oktoba 2014

UHUSIANO WA KIMAPENZI NA NGURUWE WAMFANYA KIJANA KUACHA SHULE

UNAWEZA kudhani ni Hekaya za Kusadikika! Lakini ni kisa cha kweli kwamba mama mzazi amemshitaki polisi mwanawe wa kiume, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16, kwa kile anachodai amechoshwa na tabia ya mwanawe ya kufanya mapenzi na nguruwe wao jike mara kwa mara na hata kujikuta akiacha shule.
Amelalamika akidai kuwa kijana huyo amenogewa `penzi’ la mnyama huyo maarufu hapa kama “kitimoto au noah”, kiasi cha kumfanya aache masomo na kuwa mtoro sugu shuleni.
Nguruwe huyo jike, inadaiwa anafugwa na familia ya mwanafunzi huyo anayesoma katika shule moja ya umma ya sekondari katika Manispaa ya Sumbawanga.
Hayo yalithibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Polisi Jamii mkoani Rukwa, Sixmund Kibassa aliyemweleza mwandishi wa habari hizi jana kuwa mama mzazi wa mtoto, ameripoti tukio hilo katika jeshi polisi.
Kibassa alisifu uamuzi huo, akisema ni mafanikio makubwa yanayotokana na Mpango Shirikishi wa Kitengo hicho wa kuwarejesha shuleni watoto, ambao ni watoro sugu.
Alisema mwanafunzi huyo (jina limehifadhiwa) ni miongoni mwa watoro sugu 70 kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari katika Manispaa ya Sumbawanga, waliorejeshwa hivi karibuni kupitia mpango huo shirikishi wa kuwarejesha watoro shuleni, unaotekelezwa na Kitengo cha Polisi Jamii mkoani humo.
Kibassa alisema wazazi na walezi wenyewe wanafika katika kitengo hicho cha polisi jamii na kuripoti kuhusu watoto wao ambao wamekatiza masomo.
Alisema wazazi na walezi hao, wanafichua kwamba watoto wao hao licha ya kutokwenda shuleni, pia nyumbani hawaonekani na kwamba baadhi yao wamebainika kutumia muda wao mwingi kunywa pombe vilabuni badala ya kusoma.
“Ni juzi tu mama mmoja alinifuata na kuripoti kisa cha mwanawe wa kiume anayesoma Kidato cha Pili katika shule moja ya sekondari, kwamba licha ya kuwa mtoro sugu shuleni, lakini pia amekuwa na tabia chafu ya kufanya mapenzi na nguruwe wao jike mara kwa mara…Nilipomhoji kijana huyo alikiri kufanya hivyo …basi tulimnasihi,“alieleza.
Kwa mujibu wa Kibassa, baada ya kumsihi mwanafunzi huyo, alikubali kuendelea na masomo, ambapo alirejeshwa shuleni kwake na kupokewa na walimu na wanafunzi wenzake kwa furaha.
Akizungumzia tukio hilo, Daktari wa Tiba ya Binadamu, Dk Paulo Maiga alisema mwanadamu kufanya mapenzi na mnyama, kuna madhara makubwa, ikiwemo kuambukizwa virusi ambavyo vikiingia katika mwiliwa binadamu, kuna uwezekano mkubwa visiweze kutibiwa.
“Hili ni tatizo kubwa, madhara yake ni makubwa, huyu nguruwe anaweza kuwa ameshambuliwa na virusi vya ugonjwa ambao ukiingia na kumshambulia mwanafunzi huyo, upo uwezekanao mkubwa kusiwepo na tiba,“alisisitiza Dk Maiga.

THELUTHI MBILI YA RASIMU YA KATIBA YAPATIKANA DODOMA

Bunge maalumu la Katiba limepitisha rasimu ya katiba iliyopendekezwa. Hatua hiyo imefikiwa baada ya kura za ndio zilizopigwa na wajumbe kufikia kiwango kinachostahili.
Ili katiba hiyo iliyopendekezwa ipite ilitakiwa kuungwa mkono na kura za ndio theluthi mbili( 2/3) kutoka Tanzania bara na theluthi mbili (2/3) za ndio kutoka Zanzibar.
Jumla ya wajumbe wote wa bunge hilo la Katiba ni 629, huku 419 wakitoka Tanzania bara na 210 kutoka Zanzibar.
Zoezi hilo la upigaji kura ambalo lilianza Septemba 29 mpaka Oktoba 2, siku matokeo yalipotangazwa, lilisusiwa na wabunge wa upinzani waliounda umoja wao uitwao UKAWA, kwa madai kuwa baadhi ya vipengele vya awali vilivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyopewa kazi ya kukusanya maoni kutoka kwa mwananchi, vilikuwa vimeondolewa.
Kabla ya kupitishwa kwa rasimu hiyo, bunge hilo maalum la katiba lilikaa kama kamati kujadili mapendekezo katika Rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na tume hiyo ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya uongozi wa Jaji Joseph Warioba.
Baada ya kamati hizo za bunge hilo kutoa mapendekezo yao, kamati ya uandishi ilikuwa na jukumu la kuandika upya Ibara za Sura za Rasimu ya Katiba zilizojadiliwa na Bunge Maalum na hatimaye kutoa taarifa kwa Mwenyekiti baada ya kukamilisha kazi hiyo.
Hivyo, Kamati ya Uandishi ilikuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa mapendekezo ya marekebisho, maboresho au mabadiliko katika Rasimu ya Katiba yanakidhi matakwa na masharti ya Kanuni za Bunge Maalum za Mwaka 2014.
Hatma ya katiba hiyo itahitimishwa kwa kura ya maoni inayotarajiwa kupigwa na wananchi.

Jumamosi, 27 Septemba 2014

WABUNGE WA TANZANIA SIO HALALI BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ), jana imesema uchaguzi wa wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki ni batili kutokana na kukiuka ibara ya 50 ya mkataba wa kuanzishwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Jaji Kiongozi, Jean Bosco-Butasi akiwa na majaji wengine wa mahakama hiyo, Isaac Lenaola na Jaji Faustine Ntezilyayo, walitoa uamuzi huo katika hukumu ya kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mmoja wa wagombea ubunge wa Eala kutoka Tanzania, Anthony Komu (Chadema).
Jaji Faustine Ntezilyayo, walitoa uamuzi huo katika hukumu ya kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mmoja wa wagombea ubunge wa Eala kutoka Tanzania, Anthony Komu (Chadema).
Katika hukumu hiyo ya kurasa 38, mahakama hiyo, imempa ushindi Komu katika hoja zake zote tatu na kutupilia mbali pingamizi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kesi hiyo na hivyo, kuitaka Serikali kulipa gharama za kesi hiyo.
Katika shauri hilo namba saba la mwaka 2012, katika madai yake ya msingi Komu alikuwa anapinga utaratibu uliotumika kupata wagombea wa Bunge la Eala kutoka Tanzania akidai ulikiuka Ibara ya 50 ya mkataba wa kuanzishwa kwa EAC inayoelekeza wabunge wapatikane kwa uwiano.
Ibara hiyo inaeleza kuwa, Bunge la Taifa kutoka kila nchi mwanachama litachagua wabunge tisa kutoka nje ya wabunge wa bunge husika kuwa wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuzingatia uwiano wa vyama vya siasa, jinsia na makundi mengine.
Komu pia alikuwa akitaka tafsiri ya kisheria kama taratibu zilikiukwa Spika kumpitisha, John Chipaka kutoka chama cha Tadea kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki, hali ya kuwa chama chake hakina mbunge hata mmoja.
Pia Komu alitaka kujua kama ni halali chama ambacho ndiyo kikuu cha upinzani nchini, kinachounda baraza kivuli la mawaziri, kukosa uwakilishi katika Bunge la Afrika Mashariki.
Katika uamuzi wa majaji wa mahakama hiyo, wameamua kuwa uchaguzi huo ulikiuka ibara ya 50 ya kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na upatikanaji wa wabunge wa Bunge hilo.
Uamuzi huo, ulieleza kuwa kanuni za Bunge la Jamhuri, ibara ya tano kifungu kidogo cha tano na cha 12 vilivyotumika katika uchaguzi huo, pia vinapingana na Ibara ya 50 na hivyo kusababisha kutopatikana kihalali wagombea wote wa uchaguzi huo.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji alisema kwa mkataba wa Jumuiya hiyo, wabunge wa Bunge hilo, wanapaswa kuchaguliwa kutokana na uwiano wa wabunge katika Bunge la nchi husika na pia kushirikisha makundi mengine ambayo siyo ya vyama vya siasa.
Hata hivyo, mahakama hiyo ilieleza haina mamlaka ya kutangaza kutengua ubunge wa wabunge wa Tanzania kwa kuwa shauri hilo, sasa linatakiwa kutolewa uamuzi na Mahakama Kuu hapa nchini.
Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hukumu hiyo, Komu na Wakili wake John Mallya ambaye alikuwa akimwakilisha wakili, Damas Mbogoro, walisema kutokana na uamuzi huo, sasa watapeleka uamuzi huo Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.
Wakili Mallya alisema shauri hilo, ambalo tayari lilikuwa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, linatarajiwa kutajwa Novemba 27 mwaka huu ili kupangiwa siku ya kuanza kusikilizwa.
“Tuna imani Mahakama Kuu itafuata tafsiri za kisheria zilizotolewa na majaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki ili kutangaza rasmi kutengua uchaguzi wa wabunge wa Tanzania,”alisema Mallya.
Hata hivyo, alifafanua kuwa hukumu hiyo, pia imeeleza fursa za Watanzania wengine bila kupitia vyama vya siasa wanaweza kujitokeza kugombea kwa kupitia makundi ya kijamii.