visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 8 Julai 2015

MWANAUME MWENYE UMRI MKUBWA ZAIDI DUNIANI AFARIKI DUNIA

Mwanaume mzee zaidi duniani anaefahamika kwa jina la Sakari Momoi ameaga dunia mjini Tokyo Japan akiwa na umri wa miaka 112.
bonyeza hapa kusoma zaidi...

Ijumaa, 26 Juni 2015

MTU MMOJA AUAWA UFARANSA

Mtu mmoja amechinjwa na mwingine kujeruhiwa nchini Ufaransa na mvamizi mmoja aliekuwa akipeperusha kibendera cha kiislamu katika eneo lililofahamika kwa jina la Saint-Quentin-Fallavier.

Alhamisi, 25 Juni 2015

AAGA DUNIA SIKU TATU BAADA YA HARUSI




null

Kijana  mmoja aliefahamika kwa jina la Omar Al Shaikh (16) ameaga dunia ndani ya siku tatu kwa ugonjwa wa saratani ya damu unaofahamika kwa jina la Leukemi baada ya ndoa na mchumba.Kijana huyo alimuoa mpenzi wake aliefahamika kwa jina la Amie Cresswell (16) katika wodi ya hospital ya Malkia Elizabeth iliyoko Birmigham Uingereza.

Jumanne, 23 Juni 2015

MTU MBAYA KULIKO WOTE UGANDA APATA MTOTO

 
Godfrey Baguma, 47, mwanaume ambae anadaiwa kuwa ndio mwenye sura mbaya kuliko wote nchini Uganda amejipatia mtoto wake wa nane na mke wake wa pili anaefahamika kwa jina la, Kate Namanda mwenye umri wa miaka 30.Jamaa huyo amejipatia mtoto wa kike mapema wiki hii na ameonekana kufurahia sana ujio huo wa mtoto wake.

Jumanne, 16 Juni 2015

MORSE AHUKUMIWA KIFO

Mahakama ya juu ya Misri imehakiki hukumu ya mahakama ya chini ya kumnyonga rais wa zamani Muhammad Morsi kwa makosa ya kupanga njama ya kuwatorosha wafungwa katika kipindi cha maandamano ya kumng'oa madarakani rais aliyekuwepo Hosni Mubarak mwaka wa 2011.
Hukumu hiyo inafuatia majadiliano baina ya majaji wa mahakama kuu na kiongozi wa kidini Mufti.
Awali mahakama ya chini ilikuwa imemhukumu kifungo cha maisha Morsi, kwa kosa la kufanyia ujasusi kundi la Kipalestina la Hamas, kundi la wapiganaji la Hezbolah na Iran.
Viongozi wengine 16 wa vuguvugu la Muslim Brotherhood , akiwemo kiongozi wao Khairat el Shater,walihukumiwa kifo.
Bwana Morsi pia anakabiliwa na hukumu tofauti ya kifo baada ya kupatikana na kosa la kushiriki katika kupanga njama ya kutoroka gerezani zaidi ya miaka minne iliyopita, wakati mtangulizi wake Hosni Mubarak alipopinduliwa.
Morsi tayari amehukumiwa kunyongwa
Mahakama inatarajiwa kutoa hukumu ya mwisho juu ya kesi hiyo baada ya mapumziko mafupi.
Mahakama imekuwa ikisubiri ushauri maalumu kutoka kwa kiongozi Mkuu wa Kidini nchini humo Mufti.
Kundi la Muslim Brotherhood lilitaja hukumu hiyo kama upuzi mtupu

Jumanne, 9 Juni 2015

KARDASHIAN FAMILY

Tazama hii picha ya baba na mama Kim Kardashian hajulikani mwanaume nani na mwanamke nani!!!halafu unasema Kim ni role model wako!

Jumatano, 3 Juni 2015

BOKO HARAMU WATOA ONYO JIPYA


Wanamgambo wa Boko haram wamekuwa tishio kaskazini mwa Nigeria
Wanamgambo wa kiislamu nchini Nigeria wametoa picha mpya za video lakini Kiongozi wa Boko Haram ambaye huwa anaonekana kwenye video zao, Abubakar Shekau hakuonekana kwenye picha hizo za video.
kutoonekana kwa Shekau kwenye Video hiyo kumeleta hali ya wasiwasi kuhusu kuwepo kwa hali ya mgawanyiko ndani ya kundi hilo.
Takriban watu 13 wameuawa siku ya jumanne katika shambulio la bomu katika Soko la Ng'ombe mjini Maiduguri, mji ambao uliwahi kuwa ngome ya Boko Haram, Kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Katika picha ya video ya dakika 10, msemaji huyo amekanusha taarifa zilizotolewa na Jeshi la Serikali kuwa linadhibiti miji yote kutoka mikononi mwa wanamgambo.
Ameonyesha vitambulisho vya wanajeshi akisema kuwa wameuawa, na kuonyesha mabaki ambayo amedai ya ndege ya kijeshi waliyoidungua.
Msemaji aliyekuwa amebeba bunduki na huku uso wake ukiwa umefunikwa, amesema video hiyo ilirekodiwa sambisa, msitu unaozunguka hifadhi.
Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari,amesema kuwa vikosi vya kijeshi viko kwenye doria mjini Maiduguri na kuhakikisha kuwaondoa wanamgambo hao katika eneo hilo.
Baadae wiki hii, Buhari atakutana na Viongozi wenzie wa nchi jirani kwa ajili ya kuzungumzia mikakati ya kijeshi dhidi ya wanamgambo wa kiislamu.
Takriban watu milioni moja na nusu wamekimbia makazi yao, na mamia zaidi wametekwa tangu kuanza kwa harakati za kundi hilo mwaka 2009.
Zaidi ya Watu 15,500 wameuawa katika mapigano.
 
Shared directly from BBC SWAHILI.

Alhamisi, 28 Mei 2015

JINSI YA KUTAMBUA KIPAJI CHA MTOTO WAKO NA KUKIENDELEZA.

 
 
Hujambo mpenzi msomaji na karibu sana katika mfululizo wa mafunzo kwa njia ya mtandao yanayoletwa na mimi muandishi wako Deonidas Mukebezi.Mafunzo haya pia yanapatikana kwa njia ya sauti kwenye mtandao wa watsapp ambapo yanatumika kufanya utafiti kuona kama ujumbe mmoja unaweza kuwafikia karibia watanzania wote na wasio waTanzania wanaotumia mtandao wa watsapp ili kuanzaisha kitu ambacho kitakuwa ni faida kubwa sana kwa watumiaji wa mtandao.Unachotakiwa kufanya ndugu msomaji unapopata ujumbe wa aina hii kwa njia ya sauti,ni kushare na wengine ili nao waweze kushare hatimae uwafikie waTanzania wote.
 
Tukirudi kwenye mada yetu kwanza tutaanza kuangalia maana ya neon kipaji;Huu ni uwezo anaokuwa nao mtu wa kufanya jambo Fulani bila hata kwenda kujifunza shuleni.Mala nyingi mtu huzaliwa na uwezo huo na anapokwenda shule kuuendeleza zaidi basi hulifanya jambo hilo kwa ufanisi sana.Sasa wewe kama mzazi unawezaje kutambua kipaji cha mwanao na kukiendeleza,fuatilia yafuatayo;
 
Kama motto wako anaongea kupita kiasi;Kuna watoto ambao huongea kwa spidi sana na huwa hawachoki kuongea.Watoto hawa huongea mpaka anapokwenda kulala na wengine huwa wanaongea mpaka usingizini.Huwa na tabia ya kusimulia visa mbalimbali au kukueleza mzazi yote yaliyotokea mchana pengine wakati wewe umeenda kazini au kwenye shughuli zako.Mpangilio wa maneno yao na sentensi huwa ni mzuri sana.Hii ni dalili nzuri sana kwa watoto hawa kama kipaji chao kitaendelezwa kwasababu fani zao mala nyingi huwa ni sharia,uandishi wa habari,uanasiasa pamoja na Mc wa majukwaani.
 
Jinsi ya kuwasaidia watoto wa aina hii;
1.Epuka kuwakatisha tama kwa yale wanayoongea na kama yanakera mfundishe kuongea yanayofurahisha.
 
2.Unaweza kumwambia akusimulie visa mbalimbali wakati wewe ukimrekodi na baada usikilize pamoja nae.Hii humjengea kujiamini na kuona kuwa anachofanya kinadhaminiwa.
 
3.Msaidie pia aweze kuwa msikilizaji mzuri kwa wewe kumsimulia wakati yeye akikusikiliza ana kumwambia arudie ulichosema.
 
4.Mtengenezee tabia ya kujiamini kwa kuepuka kumfokea au kumpiga mala kwa mala hususani kutokana na kosa la yeye kuongea sana.
 
Asante sana mpenzi msomaji wakati mwingine tutaangalia kipaji cha motto ambae kila jambo antaka kulifanya yeye tunawaita ''vimbelembele''.
Unaweza kuwasiliana na mimi kwenye namba yangu ya watsapp 0654627227 na tafadhali tuma ujumbe,hii ni kwa watsapp tu.

KANISA KATOLIKI LAJITOA KWENYE UCHAGUZI BURUNDI.

Kanisa Katoliki nchini Burundi limejiondoa katika mchakato mzima wa uchunguzi na uongozi wa aina yoyote katika uchaguzi huo.
Uamuzi huo umekuja wakati ikisalia wiki moja tu uchaguzi wa wabunge na madiwani ufanyike nchini humo
Kanisa katoliki ni kiungo muhimu katika suala la amani na demokrasia nchini Burundi tokea kuanzishwa mazungumzo ya amani ya Arusha mnamo miaka ya tisini.
EU inasema kuwa uamuzi wao umeafikiwa kwa sababu ya sheria kali dhidi ya vyombo vya habari na waandamanaji
Haya yamearifiwa wakati maandamano dhidi muhula wa tatu wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza yanaendelea kufanyika katika mitaa kadhaa ya mji mkuu Bujumbura kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Wakati huohuo, Jumuia ya bara ulaya imesimamisha ujumbe wake uliokuwa usimamie uchaguzi mkuu nchini Burundi.
EU inasema kuwa uamuzi huo umeafikiwa kwa sababu ya sheria kali dhidi ya vyombo vya habari, matumizi ya nguvu dhidi ya waandamanaji, na mazingara mabaya ya vitisho kwa vyama vya upinzani.
Rais Nkurunziza anapania kuwania tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yanasema kuwa zaidi ya watu 20 wamefariki wakati wa ghasia za maandamano,
tangu rais Pierre Nkurunziza alipotangaza mwezi uliopita kuwa anapania kuwania tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu, kinyume na katiba ya Burundi.
Uchaguzi wa urais umepangiwa kufanyika Juni tarehe tano, huku ule wa urais ukiwa mwishoni mwa mwezi huo wa Juni.
SHARED DIRECT FROM BBC SWAHILI

MWANAFUNZI ALAZIMISHWA KULA MATAPISHI YAKE .


Walimu wawili wamefukuzwa kazi baada ya kumlazimisha mwanafunzi kula matapishi yake baada ya kutapika wakati akipokea kipigo kutoka kwa walimu hao.

Walimu hao ambao walikuwa wanafundisha katika shule moja ya watoto wenye matatiza ya kihisia walitenda kosa hilo lililosababisha vibarua vyao kuota nyasi katika huko Suffolk county council.

Shule hiyo ambayo jina lake halikutajwa kwa sababu maalum imekuwa ikikumbwa na kashfa mbalimbali za kunyanyasa wanafunzi wake ambapo sasa matukio hayo yanafikia 100.

Kaisome The trent.

VIRUSI VYA KIMETA VYATUMWA KWENYE KAMBI ZA KIJESHI MAREKANI


Maafisa wakuu katika idara ya ulinzi ya Marekani wamekiri kuwa chembechembehai za ugonjwa hatari wa Kimeta zilitumwa kimakosa kwa kambi 9 za kijeshi nchini Marekani na moja nchini Korea Kusini.
Kulingana na makao makuu ya ulinzi nchini Marekani sampuli za chembechembehai za Kimeta zilidhaniwa kuwa zimekufa na hivyo zikatumwa kutumia njia ya usafirishaji mizigo ya umma kimakosa.
Chembechembe hizo za kimeta zilikuwa zimenuiwa kutumika katika mazoezi ya shambulizi la zana za kibaiolojia zakijeshi katika kambi za mazoezi.
Wandani wa maswala ya zana za kibayolojia wanasema kuwa kungetokea maafa makubwa iwapo chembechembe hizo za kimeta zingeachiliwa nje ya maabara maalum ya kibayolojia.
Maafisa wa serikali ya Marekani walioko Korea Kusini wameripoti kuwa takriban watu 22 waliogusana na zana hiyo katika kambi ya kijeshi ya Osnan wanachunguzwa.
Hadi sasa hakuna kati yao aliyeonesha dalili za maambukizi ya ugonjwa huo hatari.
Wakati ukweli ulipobainika mahabara na vituo vya kijeshi vilifungwa.
Kimeta ni hatari ikinuswa au ikiliwa.
Ni silaha inayoweza kutumiwa wakati wa vita vya kemikali.
Makao makuu ya kijeshi ya Pentagon yanasema kuwa haijulikani ni watu wangapi wanaokabiliwa na hatari hiyo nchini Marekani.
Hadi uchunguzi ukamilike, hakuna bacteria zozote za kimeta zinaweza kusafirishwa kutoka Marekani.
Kambi za kijeshi zilizoathirika ni Texas, Maryland, Wisconsin, Delaware, New Jersey, Tennessee, New York, California na Virginia.
Kufikia sasa watu wanne pekee wanachunguzwa nchini Marekan
Shared directly from BBC SWAHILI.

JINSI YA KUTENGENEZA AIR FRESH


Tumekuwa mala nyingi na utaratibu wa kununua Air fresh na bidhaa nyingine kutoka nchi za nje kwa vigezo kuwa hatuwezi kutengeneza wenyewe au bidhaa zetu sio bora.Hapa nakuletea jinsi ambavyo unaweza kujitengenezea Air fresh yako mwenyewe na kuifanya nyumba yako kuwa na harufu nzuri tu.

Ili bidhaa yako ikamilike unahitaji baadhi ya vitu kama mvuke ambao umepoa.Hapa nina maanisha kuwa mvuke unapopoa untengeneza maji kwahiyo tunatakiwa kuwa na maji lakini lazima maji hayo yatokane na mvuke.

Unaweza kutengeneza maji hayo kwa kuchemsha maji kutunia pipa moja lililofungwa pande zote na kuwa na mrija au mpira unaotoka katika pipa hilo kuelekea kwenye pipa lingine ambalo liko pembeni.

Kwa mfumo huo maana yake ni kuwa mvuke kutoka pipa A unaotokana na kuchemka kwa maji utaelekea pipa B.Hakikisha unapata maji ya kutosha.

Uache mvuke katika pipa B upoe halafu anza kutengeneza kwa kuchukua maji lita ishirini uchanganye na harufu vijiko vinne vya chakula na ukoroge kwa dakika zisizopungua ishirini na tano.Ongeza tena maji lita kumi na ukoroge kwa dakika tano.Hapo Airfresh yako itakuwa tayari na weka kwenye containers kwaajili ya matumizi.

JINSI YA KUTENGENEZA DAWA YA KUSAFISHA VIOO


Dawa hii hutengenezwa kwa kutumia malighafi tatu ikiwemo sabuni ya maji, maji yenyewe pamoja na vinegar.

Alhamisi, 21 Mei 2015

WAWILI WAJITOA UCHAGUZI WA FIFA

Wagombea wawili kati ya wanne waliojitokeza kuwania nafasi ya urais wa shirikisho la vyama vya soka Duniani FIFA wamejitoka katika kinyang'ang'anyiro hicho.
Nyota wa zamani wa soka huko Ureno , Luis Figo ambaye ni mmoja wa waliojitoa kuwania nafasi hiyo,amelalamikia mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi huo na kuiita kuwa ni wakinafiki.
Amesisitiza kuwa kwa mtazamo wake anaona kuwa taratibu zilizowekwa zililenga kumnufaisha mgombea mmoja tu na si kuelta usawa wa wote waliojitokeza kuwania nafasi hiyo,ambapo inaonekana kuwa ni mpango uliowekwa kumpatia nafasi ya ushindi Rais wa sasa Sepp Blatter ambaye anawania nafasi hiyo kwa kipindi cha tano.
Hata hivyo Rais wa chama cha soka huko Uholanzi , Michael van Praag , akijitoa. Huku wapinzani waliosalia ni Bw Blatter ambaye ni Jordan Prince Ali Al Hussein ambaye ni mwanachama wa kamati ya utendaji ya FIFA.
Mgombea mwingine aliyejitoa pia ni Rais wa chama cha soka cha Uholanzi Michael van Praag na hivyo kuwaacha Blatter na mtu anayedaiwa kuwa mpinzani wake wa karibu Prince Ali Al Hussein ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA

BBC SWAHILI.

Jumatano, 22 Aprili 2015

BIASHARA YA MAZAO YA CHAKULA




Na Charles Msuluzya Nazi
17. Mazao ya chakula
Biashara ya kununua na kuuza mazao ya chakula ni biashara nzuri ambayo ina faida kubwa na pia soko lake ni la uhakika kwa sababu kila mtu anahitaji chakula. Bei za mazao huwa zinabadilika mara kwa mara kufuatana na msimu. Kwa mfano; wakati wa mavuno mazao huwa na bei ndogo na kupatikana kwa wingi ubunifu ni kuhamisha kutoka huko kwenye wingi na kuyauza kwenye uhaba kwa faida kubwa. Au unaweza kununua kwa wingi na kuhifadhi hadi msimu wa uhaba nawe ukauza kwa faida kubwa. Biashara hii inahitaji uwe na mtaji pia na maghala ya kutunzia mazao hayo. Unapaswa kujifunza mbinu za kuhifadhi mazao kama vile kuweka dawa za kuua wadudu ili mazao yasiharibike. Unaweza ukaamua kuwa mkulima wa mazao, kuyalima na kuyauza au kununua mazao na kuyauza. Ni muhimu kufanya utafiti wa soko la mazao yako kabla ya kufanya biashara hii ili usije ukashindwa kuyauza.

18. Huduma za kitaalamu.
Biashara ya kutoa huduma za kitaalamu ni nzuri sana na ina mapato mazuri, inaweza kuleta utajiri na maisha bora. Ili ufanye biashara hii unapaswa kwanza kusomea taaluma husika kwa kiwango kinachohitajika na wahitaji au masoko. Taaluma ambazo zina malipo mazuri ni ufundi, ualimu, uanasheria, udaktari ufamasia, uhasibu na ufundi wa vifaa vya elektroniki. Unaweza kuanza kwa kuajiriwa kwenye ofisi inayotoa huduma ya fani yako ili upate uzoefu na siri ya biashara hiyo. Kisha tafuta kuanza taratibu kufanya kazi zako binafsi. Ukiona biashara yako inaenda vizuri acha kazi na uende kufanya biashara yako kwa juhudi na maarifa yako yote na utafanikiwa.

19. Magari ya usafirishaji.
Biashara ya usafirishaji ni biashara pana sana ambayo inajumuisha magari ya abiria na magari ya mizigo. Ni biashara yenye faida sana, inayohitaji mtaji mkubwa na usimamizi wa hali ya juu ili kudhibiti wizi wa mapato. Kwa kuwa biashara hii ni pana kila aina ya biashara tutaizungumzia hapa nchini.

(i) Kusafirisha abiria
Biashara hii ni nzuri na inayo mapato mazuri ya uhakika. Ili uweze kufanikiwa katika biashara hii unatakiwa ununue gari ambalo ni zima. Usimamie kwa karibu na kudhibiti mapato ili yasiibiwe. Gari linatakiwa lifanyiwe ukarabati mara kwa mara ili liwe katika hali nzuri ya kufanya kazi. Uweke akiba nusu ya mapato ili kukabiliana na dharura ya matengenezo makubwa. Niliwahi kuzungumza na aliyekuwa mmiliki mmoja wa magari ya kusafirishia abiria kuhusu suala hili ambapo alisimulia mkasa uliomkuta. Yeye alikuwa analetewa mapato yake katika kumbi za starehe na kutumia hizo fedha, kunywea pombe. Alikuwa haweki akiba. Siku moja gari liliharibika na lilihitaji matengenezo ya Tshs 900,000/=. Mmliki huyo wa magari ya kusafirishia abiria alikuwa hana fedha hivyo aliamua kuuza gari. Matatizo ya aina hii ya biashara ni kuwapo watu wengi wanaotegemea kuchota mapato hayo nao ni dereva, kondakta, mawakala na kadhalika. Pia kuna udanganyifu mwingi unaofanywa na dereva na kondakta kwa kusingizia kuwa gari limeharibika au limekamatwa na askari wa usalama barabarani wakati siyo kweli ili mapato wayaibe. Pia kuna wizi wa mafuta na vipuri. Ili kukabiliana na matatizo haya unaweza kumwekea kiwango maalum cha mapato anayopaswa kuwasilisha na dereva na kondakta. Kwa mfano, kwa gari la uwezo wa kubeba abiria 18 kiasi cha mapato ni Tshs 25,000/= kwa siku na gari la abiria 26 mapato ni Tshs 40,000/= kwa siku. Pia unapaswa kufuatilia nyendo za wafanyakazi hao. Unaweza kuingia mikataba na makampuni ya kusafirisha wafanyakazi au wanafunzi ili upate mapato ya uhakika pia.

(ii) Magari ya kukodi
Biashara ya taxi ni nzuri na ina faida kubwa. Tatizo lake ni gumu kudhibiti kwani soko la abiria halina uhakika kama magari ya abiria ni rahisi dereva kukuambia kwamba hajapata abiria siku nzima. Pia kuna wizi wa mafuta na udanganyifu kwa kisingizio cha kuharibika gari. Katika biashara hii unatakiwa ununue gari zima, ulifanyie ukarabati mara kwa mara ili liwe katika hali nzuri ya kufanya kazi.Umfuatilie dereva wako katika nyendo zake ili uwe karibu nae kwa msaada atakaotaka na urejeshaji mzuri wa mapato. Unaweza kudhibiti mapato kwa kumwekea dereva wa taxi kiwango cha mapato cha kuwakilisha kwa siku ambazo ni Tshs 10,000/= Unaweza kuingia mkataba wa kukodisha kwenye makampuni kusafirishia watalii au wageni na kupata mapato ya uhakika.

(iii) Magari makubwa ya abiria
Biashara hii ni nzuri. Inahitaji mtaji mkubwa kwani gari moja, linaweza kununuliwa hadi kwa Tshs 100,000,000/= Inahitaji uthibiti wa mapato kwa hali ya juu kwani kuna watu wengi ambao wanategemea kuchota mapato ya gari kama vile dereva, kondakta, mawakala, wahudumu wa magereji na kadhalika. Kuna udanganyifu mwingi unaofanywa na wafanyakazi li wakuibie, kama vile kusafirisha abiria wa njiani na mizigo. Bila kuonyesha ankara na wafanyakazi kuchukua fedha za nauli bila kuziwasilisha. Pia kuna wizi wa mafuta, kusingizia gari kuharibika wakati ni zima au kusingizia kukosa abiria ili wachukue fedha za nauli. Ili kukabiliana na matatizo hayo unapaswa: kununua gari zima na kulifanyia ukarabati mara kwa mara ili gari liwe katika hali nzuri ya kufanya kazi. Simamia gari lako kuhakikisha linajaza abiria kabla ya safari. Unaweza kuweka wakaguzi na kufanya ukaguzi wa kushitukiza njiani ili kubaini udanganyifu wa kupakia abiria wa njiani na mzigo bila kuwakatia tiketi. Weka akiba nusu ya mapato kukabiliana na gharama za matengenezo makubwa au dharura. Ajiri wafanyakazi waadilifu na pia uwalipe vizuri na uwape motisha. Ii kujipatia mapato ya uhakika, kama una magari mengi unaweza kuingia mkataba na watu binafsi au makampuni kusafirisha wafanyakazi au wanafunzi.

(iv) Magari ya mizigo
Biashara hii ni nzuri. Ina faida kubwa pia. Wingi wa mapato unategemea na ukubwa wa gari. Ili ufanikiwe katika biashara hii, unapaswa kununua gari zima kulifanyia ukarabati kila mara ili kuliweka katika hali nzuri ya kufanya kazi. Pia unatakiwa kutafuta wateja wa kukodisha gari lako kwa kungia mkataba na wafanyabishara ili kuwasafirishia mizigoyao. Unaweza kuliegesha gari lako sehemu ambayo kuna wateja wanaohitaji kusafirisha mizigo, kama vile sokoni, kwenye maduka ya jumla au viwandani. Matatizo ya biashara hii ni kuwapo kwa watu wengi wanaotegemea mapato ya gari lako ambao ni dereva, utingo, mawakala na kadhalika. Pia kuna udanganyifu unaofanywa na wafanyakazi kama vile, kubeba mizigo bila kuwasilisha fedha, wizi wa mafuta, kusingizia gari kuharibika au kukamatwa askari wa usalama wa barabara wakati sio kweli ili wakuibie fedha za usafirishaji wa mizigo. Ili kukabiliana na tatizo hili ajiri wafanyakazi waaminifu, uwape motisha na kuwalipa mshahara mzuri. Unapaswa pia kufuatilia nyendo za wafanyakazi wako.Tafuta pia wafanyabishara wakubwa au mashirika kusafirisha mizigo yao ili upate mapato ya uhakika.
CHARLES MSULUZYA NAZI
Mwandishi wa makala hii ni mshauri wa biashara na mtunzi wa kitabu cha Mbinu za biashara na maarifa ya kupata pesa na utajiri. Kwa mawasiliano piga simu namba 0755394701

MWANAFUNZI ATANDIKWA VIBOKO NA WALIMU MPAKA KUFA KITETO


Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Matui wilayani Kiteto, amefariki dunia darasani baada ya kudaiwa kuchapwa viboko na walimu watatu wa shule hiyo, kwa kile kilichodaiwa kufeli mtihani wa Kiswahili.

Polisi wilayani na mkoani Manyara, wanamshikilia mwalimu mmoja baada ya wenzake kukimbia baada ya tukio.

Akizungumza jana, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Kanali Samwel Nzoka alimtaja mwanafunzi huyo aliyepoteza maisha kuwa ni Noel Bichima (15).

Kanali Nzoka alisema tukio hilo lilitokea juzi asubuhi wakiwa darasani, wakati mwalimu huyo anayeshikiliwa na polisi alipokuwa akiwafundisha. Inadaiwa mwanafunzi huyo alichapwa viboko vinane. Haikuelezwa kama alichapwa kiganjani ama sehemu nyingine.

Nzoka alidai kuwa mwalimu huyo alimchapa marehemu baada ya kupata alama 40 katika mtihani wa somo la Kiswahili kwani walipeana mkakati wa kutofeli na kwamba mwanafunzi atakayepata chini ya alama 40 atachapwa fimbo 12.

“Mwanafunzi huyo alifariki dunia papo hapo darasani baada ya kuanguka chini alipochapwa viboko na walimu hao na mwili wake umehifadhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kiteto ukisubiri uchunguzi,” alisema Kanali Nzoka.

“Natoa wito kwa walimu wa shule za msingi na sekondari, kuangalia namna ya kutoa adhabu kwa wanafunzi wanapokosea, baadhi ya watoto afya zao siyo nzuri,” alisema Kanali Nzoka.

Diwani wa Kata ya Matui, Athumani Kidawa alisema baadhi ya wazazi wa eneo hilo waliopatwa na hasira baada ya kutokea tukio hilo, waliandamana hadi Kituo cha Polisi Matui kulalamikia kitendo hicho.
MPEKUZI

Ijumaa, 20 Februari 2015

30 WAUAWA TENA NA BOKO HARAMU CHIBOK,NIGERIA


At least 30 people were killed during an attack by Boko Haram members in Thlaimakalama and Gatamarwa villages in Borno state yesterday February 19th. Confirming the attack to AFP, the head of the Chibok Elders Forum, Pogo Bitrus said;

"From information coming in from residents of the two villages at least 30 people were killed in the attacks."