visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 26 Novemba 2014

WANYAMA AIBIWA


Maafisa wa polisi wanachunguza kisa kimoja ambapo wezi walivunja na kuingia katika nyumba ya mchezaji wa kilabu ya Southampton Victor Mugubi Wanyama nchini Uingereza na kumuibia mali yake usiku wa jumatatu.

Shati moja la kiungo wa kati wa timu ya Barcelona Andres Iniesta ,pamoja na nguo za wanamitindo kadhaa pamoja na jozi 20 za viatu ni miongoni ya vitu vilivyoibwa.

Wezi hao pia waliiba gari la mchezaji huyo aina ya Land Rover lenye thamani ya shilingi millioni 8.4 fedha za kenya,fanicha,Runinga pamoja na vifaa vyengine vya kielektroniki .

Mkenya huyo mwenye umri wa miaka 23 anaishi katika nyumba ndogo na polisi wameshangazwa kwamba majirani zake hawakuamshwa na kelele za uvunjaji huo.

Kikosi cha timu yake ya Southamptom kilikuwa kimesafiri hadi Villa ambapo bao la dakika za mwisho liliifanya mechi hiyo kuwa na sare ya 1-1.

Wanyama ameshiriki katika mechi 14 msimu huu na kufunga mabao matatu huku Southampton ikiendelea kupigania nafasi ya kufuzu katika mechi za UEFA.

Ni mchezaji aliyeuzwa kwa kitata cha juu kutoka Uskochi baada ya Celtic kumuuza kwa pauni 12.5 mnamo mwaka 2013
BBC

DADA WA ASHANTI AWATUKANA WALINZI WA AFRIKA



Kakatika picha hiyo aliyyoiweka kwenye mtandao dada huyo wa mwanamuziki Ashant alliandika maneno hayo yanayoonekana hapo chini ya picha akiiashiria kuwa walinzi hao wa mwili maarufu kama bodyguards ni wazuri lakini wanatoa harufu mbaya ukiwasogelea.

Wadau wengi wameichukulia kauli hiyo kama ni kauli ya kibaguzi ingawa mwenyewe hakujibu chochote kuhusiana na tuhuma hizo.

Ijumaa, 21 Novemba 2014

WANAWAKE WANAONYONYESHA WATOTO KULIPWA


Matokeo ya awali ya mpango wa kulipa wanawake ili kuwashawishi kunyonyesha watoto umeonesha matokeo mazuri, watafiti wameeleza.

Wakina mama katika maeneo matatu ya Derbyshire,South Yorkshire ambapo kiwango cha unyonyehsaji kiko chini kati ya asilimia 21 mpaka 29 waliahidiwa kulipwa mpaka pauni 200.

Kati ya wanawake 108 walio katika mpango huu,wanawake 37 sawa na asilimia 34 tayari wamelipwa katika kipindi cha wiki sita mpaka nane.

Wakosoaji wakiwemo madaktari wanasema mradi huu unachochea uwepo wa vitendo vya rushwa.

Mpango mwingine utafuata ambao utakua mkubwa zaidi utakaowahusisha wanawake 4,000

Tayari Wanawake 58 wamejiandikisha.

Nchini Uingereza, asilimia 51 ya wanawake kwa kipindi cha wiki sita mpaka nane, scotland kwa asilimia 38.

Takwimu ziko chini zaidi kwenye maeneo yaliyo masikini mpka kwa kiasi cha asilimia 12.

Wataalamu wa afya wanasema watoto wanatakiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita, ili kuwalinda watoto dhidi ya maradhi.

Halikadhalika tafiti zinasema kuwa kunyonyesha mtoto kunamuepusha mzazi kupata maradhi ya saratani ya matiti na Ovari.

lakini hali haiko hivyo nchini Uingereza ikilinganishwa na nchi nyingine, asilimia moja tu ya watoto nchini humo hunyonya maziwa ya mama zao kwa miezi sita