visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 29 Januari 2014

LIST YA WANAWAKE WAIGIZAJI WAZURI KULIKO WOTE DUNIANI 2013

10.PINK


9.DREW BARRYMORE

8.HARRYBELLE


7.KELLY ROWLEND


6.JENNIFER LAWLENCE




5.JANE FONDA

4.ZOOEY DESCHANEL


3.AMANDA SYFRIED

2.KERRY WASHNGTON

1.GWYNETH PALTROW.


MPENZI MSOMAJI BADO NAENDELEA KUKULETEA ORODHA HIZI ILI UZIANGALIE KWA JICHO LA TATU,KWAMBA NI KWELI KATIKA HAO WOTE HAKUNA MUAFRIKA HATA MMOJA.JE HII INADHIHIRISHA KUWA KILA KITU WAAFRIKA NI WABAYA.HIZI NI SAIKOLOJIA TU.TUAMKE,TUJIJALI NA TUJIKUBALI,KUMBUKA MABARA YOTE WATU WEUPE ISIPOKUWA NI BARA LA AFRIKA TU NDIO KUNA RANGI TOFAUTI,KWANINI HATUJIVUNII KWA HILO?


MAMA WA MBUNGE WA MAFIA AFARIKI DUNIA

Mama wa mbunge wa mafia na makamo mwenyekiti wa kamati ya ardhi,maliasili na utalii na kamishna wa tume ya utumishi wa bunge,Mheshimiwa Abdulkarim Shah,Bi Fatma Abdulkarim Mussa amefariki dunia tarehe 28 januari huko Chennai India.

Mama huyo amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda kidogo na anatarajiwa kusafirishwa kurejeshwa nchini Tanzania kwaajili ya maziko yatakayofanyika siku ya ijumaa ya tarehe 31 saa saba mchana.

Mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili ncini tarehe 30 january kwa ndege ya shirika la ndege la emirate saa 9 alasiri.

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHARI PEMA PEPONI.AMEN.

MAHAKAMA YAMUACHIA KIBANDA HURU

Na vitendo issa

Mahakama ya kisutu leo imemwachia huru mhariri mtendaji mkuu wa New Habari (2006), Absalom Kibanda na wenzake wawili, Samsoni Mwigamba, mwandishi wa gazeti la Tanzani Daima na Theophili Makunga meneja uendeshaji biashara wa kampuni ya Mwananchi Communication Limited,dhidi ya kesi iliyokuwa inawakabili.

Kibanda na wenzake walikuwa wanakabiliwa na kesi ya uchochezi dhidi ya askari wa jeshi la ulinzi kwa kuchapisha makala kwenye gazeti la Tanzania Daima yenye maneno yaliyolenga kushawishi kutowatii viongozi wao.

Waandishi mbalimbali walioudhulia kesi hiyo walionyesha kuwa wenye furaha mara baada ya ukumu hiyo kutolewa kutokana na matukio mbalimbali yaliyokuwa yanajitokeza karibuni yanayoashiria kuwa uhuru wa vyombo vya habari hauzingatiwi ipasavyo Tanzania.
PICHA MBALIMBALI ZA KIBANDA

Jumanne, 28 Januari 2014

WANAFANANA

HEBU FANANISHA PICHA HII YA KIJANA ANAEDAI KUWA NI MDOGO WAKE DIAMOND PLANTINUMZ

PICHA YA HUYO KIJANA



PICHA YA DIAMOND AKIWA NA PENNY.

TUFANYE YETU TANZANIA

MCHAGUE THE MOST BEAUTFUL GIRL KATIKA BONGO MUVIE & THE MOST HANDSOME MAN. ANDIKA JINA MOJA MFANO JOICE KWENDA NAMBA 0654627227,JINA MOJA LA KIUME NA JINA MOJA LA KIKE.


MATOKEO YATACHAPISHWA KATIKA UKURASA HUUHUU.

KWA WALE WALIOKO MIKOANI NA WANAHISI WANAHABARI ZAO WANGEPENDA ZIWAFIKIE WANANCHI UNAWEZA KUTUCHEKI KATIKA NAMBA HIYO HAPO AU KUTUMA HABARI YAKO KATIKA EMAIL mdeonidas@yahoo.com.Hakikisha habari yako ina picha za tukio za kutosha

ARSENAL WAVUTWA SHATI

Viongozi wa ligi ya uingereza timu ya soka Arsenal jana walijikuta wakipoteza point mbili baada ya kukubali kutoka sale na timu ya soka ya Southompton.

Timu hiyo ya southompton ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao kupitia mchezaji wake Jose Fonte,baada ya kuunganisha cross kali iliyotoka kwa mchezaji Luke Shaw.

Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika ubao ulikuwa unasomeka kuwa ni moja kwa sifuri.

Kipindi cha pilli kilianza kwa kasi,Arsenal wakishambulia kwa nguvu zote kuhakikisha kuwa wanarudisha gori na pengine kupata lingine la ushindi,na juhudi zao zilionekana dakika ya 48 wakati Bakari Sagna alipochonnga cross kali iliyounganishwa moja kwa moja gorini na mchezaji Olivia Giriud.

Iliwachukua tena Arsenal dakika nne tu kufunga bao la pili kupitia mchezaji wake Saint Carzola baada ya kupiga shuti lililomzidi nguvu goal keeper wa Southampton na kufanya ubao usomeke 2-1 mpaka kufikia dakika ya 52.

Sherehe ya magori katika mechi hiyo ilifungwa dakika ya 52 wakati Adam Lallana alipofunga goli la kusawazisha baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa mchezaji mwenzake Jay Rodriges na kuuvurumisha langoni mwa Arsenal na kukamilisha kalamu hiyo.

Katika mechi hiyo Arsena walijikuta wakicheza pungufu kuanzia dakika ya 80 baada ya mchezaji wao Matheau Flamin kupewa kadi nyekundu iliyotokana na kumchezea rafu ya miguu miwili mchezaji wa timu pinzani Morgan Shneiderlin


Matokei ya mechi nyingine zilizochezwa jana ni;

MANCHESTER UNITED 2-0 CARDIFF


SWANSEA 2-0 FULHAM


CRISTAL PALACE 1-0 HULL CITY

NORWICH CITY 0-0 NEWCASTLE

MAFURIKO MOROGORO YAMEIKUMBUSHA SERIKALI JUKUMU LAO

Moja katika majukumu ya serikali yaliyoorodheshwa katika katiba ni kuwapatia wananchi huduma ya chakula,Hii ni moja kati ya huduma za jamii ambazo serikali inapaswa kulitekeleza siku zote ambazo inakuwa madarakani.Cha kushangaza ni kuwa serikali huwa inasubiri majanga makubwa kama hili lililotokea juzijuzi mkoani Morogoro la mafuriko.

Shukrani kwa Rais JK kuwaagiza watumishi kuhakikisha kuwa waathirika wanapata chakura kutoka kwenye maghara ya serikali.

Lengo la kipengere hiki ni kutaka kuwakumbusha kuwa matatizo ya njaa katika jamii yapo kila siku,na ni jukumu la serikali kutafuta nani ana njaa na kuhakikisha kuwa anapata chakula.

Niwape pole sana wale walioathiriwa na mafuriko pale Morogoro na kuwapa moyo kuwa Serikali yao haijawatupa na msaada wa kutosha unatarajiwa ili kuyapunguza maumivua ambayo yalitarajiwa

.

Baadhi ya picha zikionesha tukio la mafuriko Morogoro na madhara yaliyojitokeza.

Jumatatu, 27 Januari 2014

PICHA ZA WATU AMBAO NI MOST HANDSOME DUNIANI

HUYU NI MJUKUU WA MFALME FAISAL WA SAUDIA

ZIJUE HISTORIA ZA WASANII KATIKA PICHA

MTOTO HUYU KATIKA PICHA NI HEMED (PHD)AKIWA NA MAMA YAKE ENZI HIZO

PICHA HII INAMUONESHA HEMEDI NA MAMA YAKE WALIVYO SASA

PICHA HII NI YA NYUMBA ALIYOZALIWA LADY JAYDEE.KWA MUJIBU WA YEYE MWENYEWE ALIZALIWA NDANI YA NJUMBA HII NA SIO HOSPITALI

Natumai mmefurahia.Shukrani kwa Zamaradi na Lady Jaydee kutuwezesha kupata picha hizi

ZAWADI/ GIFT

YALIYOMO

SHUKURANI……………………………………………………………………………………………………………………..I
UTANGULIZI……………………………………………………………………………………………………………………..II
DIBAJI………………………………………………………………………………………………………………………………..III





















SHUKURANI
Sitakuwa nimefanya lolote kama nisipoanza kumshukuru MWENYE ENZI MUNGU muweza wa yote ambae ameniwezesha kuwa miongoni mwa watu ambao ameamua waendelee kuishi katika hii dunia .Pamoja na kuniwezesha kuishi pia ameendelea kunisimamia katika mamba mbalimbali yanayohusiana na maisha yangu hapa duniani katika halinzuri na hali mbaya .Nashukuru kwa yote kwa kuwa mambo hayo ndio yanayofanya maisha yaitwe maisha na kila iakimoja kinasababu maalum ya kuwepo katika nafasi yake kwa hiyo kila linalotokea tunapaswa kushukuru.
Shukurani nyingine za dhati kabisa ni kwa mke wangu mpendwa ambae amekuwa na mimi bega kwa bega katika hali zote zinazohusiana na maisha.Namshukuru kwa upole na moyowake wa uvumilivupamoja na mzigo wate wa majukumu aliyonayo ya kuitunza familia.
Pamoja na wote hao nawashukuru wazazi wangu walionizaa akiwemo mama yangu mpendwa ambae sasa ametangulia mbele ya haki,Baba yangu mzee Mukebezi ambae Mungu anaendelea kumpa moyo wa subira kwa kumpoteza mke wake mpenzi,ndugu jamaa na marafiki zangu wate akiwemo kaka yangu mpendwa ambae amekuwa akinisimamia sana kwa hali na mali kw ayote ninayoyafanya.












UTANGULIZI
Hadithi hii inatokana na ukweli uliopo kwenye maisha yetu ya kila siku.Watu wengi wamekuwa wakikata tamaa katika maisha na hasa wanafunzi mashuleni kwa kisingizio kuwa maisha yao ni duni hivyo hata wakijitahidi hawawezi kufanikiwa katika maisha.Mawazo hayo ni potofu kwa kuwa hakuna binadamu yoyote aliezaliwa na pesa isipokuwa ni juhudi na maarifa za baadhi ya binadamu ndio zinazowafanya kuitwa mamilionea,mabilionea au hata kuwa na nafasi ambazo wamekuwa wakiota kuwa nazo katika maisha.
Msichana JENI ambae baadae alib adilishwa jina kuwa ZAWADI ni kiwakilishi tu cha watu ambao pamoja na yote yaliyotokea katika maisha hawakati tama na wanaendelea kupambana mpaka mwisho wa siku wanafanikiwa kupata kile wanachokusudiwa kukipata.
Pamoja na kufiwa na wazazi wake wote tena kwa kuliwa na wanyama wakali wa majini aina ya mamba Jeni chini ya mikono ya mwanamke msamalia anafanikiwa kupambana na vikwazo vyote vya maisha mpaka kufanikiwa kuwa na cheo kikubwa kabisa katika nchi ingawa kazi hiyo haikuwa rahisi.Endelea kuisoma hadithi hii ujue ni jinsi gani msichana jasiri ZAWADI ataweza kutimiza malengo yake.

MUKEBEZI,Deonidas G(2014)Muandishi wa habari
A journalist &teacher.

















MOJA 1
Walitembea kwa uangalifu kila mmoja akiwa makini kuangalia eneo zuri ambalo litafanana au litakaribia kufanana na eneo la mwanzo.Akiwa na mawazo mengi juu ya ya umaskini uliokithiri katika familia yake,juu ya jinsi ambavyo motto wake wa kike atakavyoishi bila matatizo ambae kwa wakati huo alikuwa ndio kwanza ana umli wa mwaka mmoja,Pia akiwaza kuhusiana na jinsi ya kuwakwepa polisi ambao ndio walikuwa kikwazo kikubwa katika biashara yao,mzee John aliweza kuona mto mkubwa ambao ulikuwa na maji yaliyokuwa yanateremka taratiibu kuelekea bondeni.
Alimshika mkono mke wake mama Jeni ambae wakati huo alikuwa amembeba Jeni mgongani,wakasogea karibu kabisa na mto huo ambao ulionekana kuwa mkubwa kuliko mto wa mwanzo.
Wiki moja iliyopita mzee john na wenzake walitimuliwa kutoka katika eneo lao ambalo walizoea kutengeneza pombe haramu aina ya chang’aa(gongo) na maafisa wa polisi,ambao walipewa habari ya kuwepo kwa eneo hilo na raia ambae alipita katika harakati zake na kugundua maficho hayo amayo yalikuwa na mitambo na mapipa mengi kwaajili ya kazi maalum ya kuchemsha gongo.
“Nafikiri hapa panafaa”alisema mzee John
“Sana!tena pamejificha kuliko eneo la mwanzo”mama Jeni alimuunga mkono mumewe.
Mzee John aliendelea kukagua eneo zuri ambalo lingefaa zaidi kwa kazi yao kando yam to huo.Wakati huo mama Jeni aliamua kusoge karibu na maji ili amsafishe Jeni ambae alianza kulia kwa kwa sauti kutokana na mkojo ambao ulilowanisha nguo na za mama yake.
Mama Jeni alifungua kanga ambayo aliifunga kwa utaalamu wa asili ili kumfanya motto asidondoke kutoka mgongoni,na kumshusha Jeni ambae kwa wakati huo alionekana kufurahia kutokana na kuhisi kuwa kilio chake kimesikiwa.Akiwa katika harakati za kumsafisha Jeni mala ghafla bila kutegemea aliona kitu kama kifaa cha kuchania mbao aina ya msumeno kikiubana mguu wake wa kushoto.Kabla hajatafakari dubwana lile lilianza kumvuta mzimamzima kuelekea mtoni.
“Mama weeee”

Baba Jeni aliisikia sauti ya mkewe akiwa tayari yuko mbali sana na eneo la tukio.Alijitahidi kuiamlisha miguu yake imbibe kadiri inavyoweza kuelekea mahali walipokuwa mama Jeni na motto wao Jeni.Akiwa bado yuko mbali aliweza kumuona mkeweambae alikuwa amemkumbatia motto wake Jeni kw makini sana akipambana bila mafanikio kujitoa katika ya wanyama wale ambao sasa walikuwa wawili na ambao walikuwa hawapo tayari kuliachia windo lao asubuhi ile.
Mzee John alifika na kumchukua Jeni ambae alimlaza pembeni yam to ule mbali kidogo na eneo lile.Ilikuwa kama Jeni ndio alikuwa anaongeza uzito na moyo wa kupambana kwa mama yake kwani baada ya kuondolewa kwenye mikono ya mama yake,mama Jeni nguvu zilimuishia na ikawa rahisi kwa mamba wawili wakubwa kumvutia mama Jeni mtoni.
Wakati mzee Joni anafika eneo lile ili aweze kumsaidia mke wake, alishuhudia kichwa cha mkewe kikitokeza kwenye maji ghafla na kupotea moja kwa moja.Bila kutafakari mzee John alijitosa kwenye maji ili kumtafuta mkewe.Kwa bahati mbaya mzee John hakufahamu kina cha mto ule na hakuwa na ujuzi wowote wa kuogelea.Kutokana na ukweli huo mzee John alipoingia tumoja kwa moja alijikuta anamezwa na maji ambayo hakuweza kupambana nayo.
Maji yale yalimtoa nje mala ya kwanza na mala ya pili,mala ya tatu alishukia kwenye midomo ya mamba ambao waligombania supu na minofu ya mwili wa mzee kama wana njaa ya siku tano.Mto ulibadilika na kuwa na rangi nyekundu na eneo lote lilitoa harufu ya damu.
Mtoto Jeni baada ya kusubili kwa muda,uvumilivu ulimshinda na akaanza kulia kwa sauti kali bila mafanikio.Kwa muda wa nusu saa nzima Jeni alilia mpaka sauti ilikuwa hafifu na mwisho akapitiwa na usingizi na kulala…
























MBILI 2
Bi Zainabu ambae alikuwa hana mume wala mtoto na ambae alimua kuishi maisha ya upweke msituni kutokana na matatizo ambayo alishakumbana nayo zamani,alikuwa akipitappita msituni kujiokotea kuni kwaajili ya kwenda kujipikia chakula baada ya kazi nzito. ya kulima kijishamba kidogo kilichokuwa nyuma ya kibanda chake.Hakuwa na wazo lolote juu ya atakachokiona kule alikokuwa anaelekea zaidi ya kuni.Ghafla kwa mbali aliweza kuoona kitu kama jiwe limelala kando yam to.Aliposogea zaidi alishangaa kuona mtoto mzuri mwenye afya amelala usingizi mzito.Alihisi kuwa mtoto huyo alikuwa ni mmoja kati ya watoto wa kijiji cha BOMA ambacho kipo karibu kabisa na mahali hapo alipokuwaanashi peke yake.
Mawazo mengi yalimjia kwa wakati mmoja na hakujua aanze na lipi.Aina ya maisha aliyokuwa anaishi ilikuwa ni kutokana na ukweli kuwa hakuwahi ku bahatika kupata mtoto katika maisha yake.Je!mtoto huyo alikuwa ni zawadi kutoka kwa mungu?,Au je ampeleke motto huyu kwa mwenyekiti wa kijiji na kuitupa zawadi hiyo?Kama sivyo je!amuache motto huyo mahali alipo?Mtoto Yule alikuwa ni mtu au ni shetani?Nani kamuweka mahali pale?....Kwanini?..........?.............?....................?.....................?.Maswali mengi yalikuja kichwani kwake kama umeme na hakujua aamue lipi aache lipi
Bi Zainabu alimuinamia na kumbeba mtoto kwa uangalifu mkubwa asimuamshe kutoka katika usingizi.Alimpenda sana motto Yule na kwa upendo huo tayari bi Zainabu alishapata jibu la maswali mengi yaliyokuwa yanamsumbua…
Aliamua kuacha shughuli ya kutafuta kuni na kumpeleka motto nyumabani kwake ambapo alimtengenezea mahali pazuri pa kulala.Baada ya kumlaza motto na kuhalilisha kuwa yuko salama na amelala usingizi,bi Zainabu aliwasha moto na kumtengenezea uji mtoto Yule.
Baada ya nusu saa uji ulikuwa tayari na Bi Zainabu alimuamsha mtoto na kuanza kumlisha uji ambao aliunywa bila kipingamizi kutokana na njaa aliyokuwa nayo.Wakati wote huo bi Zainabu alikuwa akiwaza kwa furaha jinsi Mungu alivyosikia kilio chake na kumpatia motto.
Zamani alipokuwa mwanafunzi kila mwanaume alitamanni kumuoa kutokana na uzuri wake wa umbo na sura.Baada ya kumaliza elimu ya msingi katika shule ya msingi pango Zainabu alichumbiwa na kijana mtanashati kutoka jijini Dar es salaam na siku zilipotimia aliolew na kuhamia jijini Dar es salaam kwa kijana Zuberi.
Kwa mwaka mzima Zuberi na Zainabu waliishi maisha ya furaha na amani wakifanya starehe za kila aina kutokana na ukwli kuwa Zuberi alikuwa anajiweza kiuchumi.Baadaya muda kupita Zuberi alianza kubadilika hasa baada ya kugundua kuwa muda mrefu ulipita bila ya Zainabu kushika ujauzito.Zuberi alianza kuchelewa kurudi nyumbani na hata alipokuwa anarudi mapema Zainabu aliambullia kipigo na matuisi.Zainabu alivumilia hali hiyo kwa muda wa miaka miwili na hatimae uzalendo ukamshinda na akaamua kurudi nyumbani kijijini Pango na kuendelea kuishi na wazazi wake kama mwanzo.
Kama wahenga wasemavyo ukisema cha nini wenzako wanawaza watakipata lini,baada ya miezi sita Zainabu aliolewa tena na mwanaume mwenye maisha ya kawaida kutokajijini Mwanza.Waliishi maisha ya upendo kama mke na mume,lakini baada ya miezi nane tumwanaume Yule hakuwa tayari kuvumilia zaidi na akaamua kumuacha Zainabu kwa kigezo kile kile cha kutokupata mtoto.Zainabu aliapa kutokuolewa tena nje ya kijiji chao.Alikaa miaka mitatu,kipindi hicho akiwa na umli wa miaka ishirini na nne na kupata mwanaume mwingine kutoka kijijini kwao Pango kama alivyo taka ambae alikuwa maskini kama yeye.Zainabu aliishi kwa rah asana na mwanume huyo kutokana na kumueleza mwanaume huyo ukweli wote kabla hata hawajaoana na akakubaliana na hali ya Zainabu ya kuto kushika ujauzito.Pia Zainabu alimueleza mwanaume huyo yote yaliyo mpata katika maisha yake yaliyopita na mwanaume huyo akamuahidi kuwa hatamuacha na ataishi nae mpaka kifo kitakapowatenganisha.
Zainabu aliishi na mwanaume huyo kwa muda wa miaka mitano na alionekana kumpenda sana bila kujali hali yake.Zainabu alijihisi yulo salama sana katika mikono ya Hamisi ambae alimuona kama ni zawadi kutoka kwa Mungu.Kazi yake kubwa aliyokuwa anafanya Hamisi ilikuwa kilimo cha maharagwe na mahindi.Kila asubuhi Hamisi na mkewe walikuwa wanaelekea shambani kwaajili ya kuendelea kufanya shughuli zao za kawaida za kilimo.
Ilikuwa ni siku ya jumatano,siku ambayo ilibadilisha kabisa maisha ya Zainabu na ni siku ambayo Zainabu hawezi kuisahau katika maisha yake.Wakiwa wametoka asubuhi kwa furaha kabisa na mume wake,na siku hiyo jua likiwa ni la wastani,wanandoa hao walipanga kuitumia siku hiyo kuchoma mabiwi kwaajili ya kupanda mbegu.Walifika mapema kabisa shamban na kuanza kazi mala moja.Hamisi aliamua kuyakusanya mabiwi kwa wingi ili ayachome kwa pamoja.Aliyasogeza mabiwi hayo karibu kabisa na mpaka ws shamba la jilani ambalo lilikuwa na miwa mingi yenye majani makvu.Bila kufikiri Hamisi alimuagiza kibiriti mkewe na kuyawasha moto mabiwi mengi sana aliyoyakusanya.
Mabiwi yale yalianza kuwaka taratibu lakini baada ya muda mfupi moto ule ulikuwa mkali na wa kutisha.Kabla hajakaa sawa moto ulikamata majani makavu yaliyokuwa kwenye shamba la jilani na kuanza kutembea kuelekea kwenye miwa ya jilani.Hamisi hakuwa na jinsi alishaiona hatari ambayo ingetokea mbeleni.Alijaribu kuuzima moto ule kwa kutumia majani ya miti lakini haikusaidia.Kwakuwa katika shamba la jirani kulikuwa na kijoto kidogo kilichokuwa kinatiriririka,aliamua kuuzima moto ule kwa kutumia maji.Maji hayakusaidia kutokana na ukavu wa majani na umbali kutoka mahali ambapo moto ulikuwa unawaka na mtoni na hivyo moto uliendelea kuwa mkali zaidi ya mwanzo.
Kwa kipindi ambacho alikuwa anahangaika kuuzima moto ule,Hamisi alitumia muda mrefu sana kiasi kwamba moto ulifika karibu kabisa na shamba la miwa la jirani yake.Aligundua kuwa hakuwa na muda tena wa kulima njia kuzuia moto usipite kuelekea kwenye miwa hiyo.Alitumia muda wa sekunde kadhaa kuwaza njia ya haraka ambayo ingemsaidia kupata suluhisho la halaka na ndipo alipokumbuka moja ya misemo ya zamani kabisa ‘Dawa ya moto nimoto’.Hilo ndilo tumaini pekee alilokuwa nalo Hamisi kwa wakati huo kwa kuwa njia zote zilishindwa.Alikumbuka siku moja wakati yuko darasa la tano mwalimu wao wa Kiswahili aliwaeleza kuwa moto unapokuwa mkubwa katika eneo lililowazi,ukiwasha moto mwingine mbele yake utavutwa kuelekea kwenye moto huo mkubwa.
Hamisi alijaribu!.Alichukua kibiriti na kuwasha moto mwingine mbele kidogo ya moto ule mkubwa ambao sasa ulikuwa unaunguruma na kutoa miali ya kutisha kama radi wakati wa msimu wa vuli.Haikuchukua muda moto mdogo aliouwsha Hamisi ulianza kushika kasi na kuwa mkubwa.Moto huo ulianza kuvutwa kuelekea ulipokuwa moto ule mkubwa uliokuwa ukiendelea kuunguruma kwa msaada wa upepo.Kutokana na hali hiyo moto mkubwa ulianza kuzunguuka na kutengeneza alama ya mwezi mchanga.Kutokana na kuchanganyikiwa Hamisi alisahau kuwa aliwasha moto mdogo akiwa yuko katikati,na alibaki anashangaa moto ule aliowasha ulivyokuwa unavutwa kwa nguvu na moto mkubwa na kufurahi moyoni kuwa amefanikiwa jaribio lake.
“Hamisiiiiiiiii” Alisikia sauti ya mkewe ikimuita na alipostuka akajikuta yuko katikati ya moto uliomzunguka pande zote.Moto ulikuwa mkubwa kiasi kwamba hakuweza kuona kundi kubwa la wanaume wa kijijini Pango walifuatana na Zainabu kwenda kumsaidia mumewe baada ya Zainabu kwenda kuomba msaada.Walijitahidi kuuzima moto ule,lakini kwa muda waliofika walishachelewa sana.Moshi ulikuwa mwingi sana kiasi cha kufanya Hamisi ashindwe hata kutoa sauti.Pumzi zilimuishia na akadondoka chini.Moto mdogo na ule mkubwa viliweza kuungana kabisa Hamisi akiwa katikati.Huo ukawa ndio mwisho wa mume kipenzi wa Zainabu,Hamisi.
Moto ulipopungua wanakijiji waliweza kuuona mwili wa Hamisi ukiwa umeiva na kuwa mwekundu kama mbuzi wa kuchoma(ndafu).Hakuna aliependa kumtazama Hamisi mala mbili!.Wanakijiji waliubeba mwli wa marehemu na kuurudisha kijijini kujiweka tayari kwaajili ya mazishi.Wakati wote huo Zainabu alishazimia na kuzinduka mala mbili nab ado alikuwa hajitambui kw auchungu mkubwa aliokuwa nao wa kuondokewa na mwanaume ambae ...........................USIKOSE KUJUA KILICHOENDELEA.

Alhamisi, 23 Januari 2014

One of the important Media Act to the constitution of United Republic of Tanzania is The Electronic and postal communication Act number 3/10 of 2010.This Act though it is very important has several impacts to the media of Tanzania. The impacts of this Act can be evaluated in accordance to its sections as follows;

The Act reduces number of media ownership especially private ownership in Tanzania. Example one of the sections which is section number10 which is dealing with Grant of license state that (2) where frequency requirements involved the applicants shall make a separate application for a radio frequency user license. This means the process of obtaining media license and radio frequency user license, the process which discourage people from starting or trying acquiring media license.

The Act also reduce media competition especially due to development of science and technology. The act has some condition which prohibit the media from transmitting or publishing some information which are named as indicent.This means media would leave some information which might be important to the audience. This might cause the audience to search for alternatives in other sources which are not limited such as internet. Example of section deals with this is section number 53 which state that a person shall not send by post any (a)indecent or obscene

printing,painting,photograph,lithograph,ingraving,book or obscene article.
Furthermore the Act goes against one of human rights which is the right to information. Due to limitation in publishment and transmission journalist escape from publishing the so called indecent information.

In addition to that the act gives too much power to the authority against media owners. For example section 22 (b) state that the authority may suspend or cancel a license if the license and authority have agreed in writing to terminate the license.

Also the license ownership is not stable for the media owners. This means any time the license can be terminated as section 21© which deals with suspension and cancellation of license state, that the license terminate up on expire of the terms and is not renewed.

Another impact is that the act relies much to the authority and ignore another side which is media. Example in section number 54 which deals with the authority to make rules dealing with prohibited articles state that the authority may make rules for preventing the sending and delivery of articles prohibited under this Act and detaining disposing of or destroying any such postal article sent or tendered by for transmission by post.

The Act affects sponsorship and advertisement and hence reduce the finance capacity to the media. This is because all advertisement done by the media is under special supervision in accordance to the terms and conditions. The section which deals with this issue is section 109 which deals with advertising and sponsorship. The section state that without derogating from the generality of power of the authority to make rules pertaining the advertising and sponsorship of such rules it may include the following provisions;
(a)Prohibiting, restricting or regulating advertisement of specified goods, products, services, activities,prohibiting,restricting or regulating specified forms and methods of advertising and sponsorship.
(b)Prohibiting,restricting,or otherwise regulating political advertising. All these and the remainder of section 109 give the evidence that sponsorship and advertising is not done but under special conditions and terms to be followed and instead it might cause problem to the media pertaining the license.

Also the Act protect the president from being published negatively and reduce one of the important function of mass media which is Acting as a gate keeper. One of the sections which gives such power to the president is section number 59 which is about power of the president in emergency or in the national or public interest. The section state that (1) the president may on occurrence of any event which gives rise to an emergence or in the interest of national or public security authorize the authority to (a) suspend the public postal license of postal licensee and take temporary possession of any post office under the control of any such licensee.(b)Withdraw either totally or partially the use of any postal service from any person or class of person or from the public at large.

That is on one side of the impact, on the other side the act have some positive impact whereby it helps the media to be responsible and stand to the ethics. In order to avoid any possibility of suspension and withdraw of the license, media owners are making sure that there is not any indecent posted or transmitted to their media.

It helps also to control the market and media competition due to the fact that it reduces number if media owners hence avoiding too much media in the market. By doing that it helps the owners to maintaining the existing and avoid banklupse.

In conclusion the Act requires any one who makes an offence to be punished by paying the amount of money which has not specified. This punishment seem to give the chance for the media to make some offence by having confidence that if anything bad happens they are just paying the money and the case is finished. This can be seen in section number 155 which deals with power of the authority to compound certain offence which state that, Where a person commit an offence under this Act, the director general may, at any time prior to the commencement of court proceeding;(a)compound the offence other than offences related to theft fraud, forgery and other similar offence and (b)order the person to pay a sum of money specified by the director general but not exceeding the amount of the fine prescribed by the offenses .

















PICHA MBALIMBALI ZA WAHUSIKA WA SHAMBULIO LA WASTE GATE/KENYA

WATOTO WA TANZANIA/(DOUBLE LL KIDS): JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI ZA MICHE

WATOTO WA TANZANIA/(DOUBLE LL KIDS): JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI ZA MICHE: MAHITAJI; (I)CAUSTIC SODA (II)MAFUTA YA NAZI,MISE,MBOSA AU MAWESE AU YA NYONYO (III)MAJI (IV)PAFYUM (V)HYDROGEN PEROXIDE (VI)CHUMVI ...

MBUNGE WA CHALINZE KUZIKWA IJUMAA.

Mazishi ya mbunge wa jimbo la Chalinze mh.Said Bwanamdogo aliefariki siku ya jumatano katika hospitari ya mifupa MOI jijini Dar es salaam yatafanyika siku ya ijumaa tar 23/01/2014.

Akithibitisha taarifa hizo mmoja wa ndugu wa karibu wa marehemu Bwanamdogo alisema kuwa ndugu wameamua maziko hayo yafanyike ijumaa kwa kuwa taratibu zote zitakuwa zimekamilika.

Viongozi kadhaa wanatarajiwa kuhudhuria katika mazishi hayo akiwemo mheshimiwa makamo wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine wa serikali.


Mheshimiwa Bwanamdogo atazikwa kijijini kwao miono siku hiyo ya ijumaa ambapo waombolezaji wakiwemo ndugu jamaa na marafiki wanatarajiwa kumsindikiza ndugu yao huyo mpendwa.Mungu ailaze roho ya marehemu mahari pema peponi.Amen

Jumatatu, 20 Januari 2014

KUMBE FROLA MVUNGI ALITAMANI DIAMOND NA WEMA WARUDIANE!!


Zikiwa zimepita wiki kadhaa tangu wasanii maarufu wa Tanzania Nasib Abdul maarufu kama Diamond na Wema Sepetu kurudiana,imebainika kuwa baadhi ya wasanii wa Tanzania walikuwa wakitamani uhusiano huo urudi na moja kati ya wasanii hao ni msanii Frola Mvungi.

Hilo lilibainika baada ya muandishi wa habari hii kuinyaka moja kati ya ujumbe wa maneno wa Frola Mvungi alioutuma katika mtandao wa instagram akiwaombea wasanii hao kwa Mungu waendeleze uhusiano huo.
"Mimi na mume wangu tunapendana sana,but still tunaipenda sana hii couple iendelee kuwepo Mungu awajalie mapenzi tele wafike malengo.All the best darling."ulisema ujumbe huo wa Frola.

Uhusiano wa wasanii hao wawili umeonekana kurudi kwa nguvu zaidi ya zamani na watu wengi ambao ni wapenzi wa wasanii hao wameonekana kufurahia uhusiano huo.

UMEME WAPANDISHA BEI ZA BIDHAA BAGAMOYO

Katika hali ambayo iliwasikitisha wananchi wengi mjini Bagamoyo,wafanyabiashara wameamua kupandisha bei za bidhaa mbalimbali zikiwemo zile za huduma za saloni na maduka ya kuuza bidhaa mbalimbali.

Wakizungumza na muandishi wa habari hii,wafanyabiashara hao wamesema kuwa wao sio wanaosababisha ugumu wa maisha kwa wateja bali shirika la umeme na serikali kwa ujumla ndio wa kulaumiwa kwa kupandisha bei ya umeme bila kuzingatia hali za watanzania wengi

"Sisi bwana hatuwezi kulaumiwa kwa hili,unapopandisha umeme maana yake ni kuwa matumizi pia yanapanda!tunatumia umeme kupooza maji pamoja na vinywaji vingine,na siku hizi kila siku umeme unaisha kwahiyo hakuna jinsi zaidi ya kupandisha bei ya bidhaa la sivyo ni hasara tupu"alisema mmoja wa wafanyabiashara anaefanya biashara ya kuuza maji.

Nae Joice mathew mfanyabiashara wa salon ya kike akizungumza na muandishi alikiri kupanda kwa bei ya huduma hiyo na kusema kuwa zamani alikuwa akitoa shilingi 20000/- anapata unit 18 lakini kwa sasa ni unit 13 tu na hivyo njia pekee ya kulitatua hilo ni kuongeza bei ya huduma.

Kwa upande wao wananchi wamesema hawawalaumu wafanyabiashara kwa kuwa hawawezi kufanya biashara kwa hasara,bali wao wanailaumu serikali kwa kuto kuwajari na hivyo kuzidi kuwaongezea ugumu wa maisha.

KATA YA MAGOMENI YARINDIMA KWA KAMPENI

Ikiwa umebaki mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mdogo wa madiwani kufanyika katika sehemu mbalimbali hapa nchini,wanasiasa wa vyama mbalimbali wamekuwa wakipigana vikumbo kufanya kampeni katika kata ya Magomeni wilayani Bagamoyo mala baada ya uzinduzi wa kampeni hizo siku ya jumamosi.

Baadhi ya wanasiasa waliofika kupigania kata hiyo ni pamoja na wale wa CIVIC UNITED FRONT(CUF) Wakiongozwa na kiongozi wao ambae ni katibu wa chama hicho taifa maalim Seif Sharif Hamad,Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakiongozwa na katibu wao mwenezi bwana Nape Nnauye pamoja na wale wa Chama Cha Demoklasia na maendelea(CHADEMA).

Kata hiyo ya Magomeni inafanya uchaguzi wake mala baada ya aliekuwa diwani wa kata hiyo kuiaga dunia ghafla mwishoni mwa mwaka jana na hivyo nafasi yake ya udiwani kubaki wazi.

Nao wananchi waliohudhuria kampeni hiyo walisema kuwa wanahudhuria kwa wingi katika kampeni hizo ili kusikiliza sera za wagombea na hatimae kuchagua diwani wao kulingana na sera zake na sio chama chake.

Walisema wanasiasa wa sasa wamekuwa na tabia ya kuwadanganya wananchi wakati wa kampeni lakini mwisho wa siku hawatekelezi ahadi zao.

NAPE NNAUYE AKIONGEA NENOWANANCHI WAKISIKILIZA KWA MAKINI
MAMBO YAMEPAMBA MOTO
WANANCHI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZAMSIFANYE MAKOSA