visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatatu, 20 Januari 2014

KATA YA MAGOMENI YARINDIMA KWA KAMPENI

Ikiwa umebaki mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mdogo wa madiwani kufanyika katika sehemu mbalimbali hapa nchini,wanasiasa wa vyama mbalimbali wamekuwa wakipigana vikumbo kufanya kampeni katika kata ya Magomeni wilayani Bagamoyo mala baada ya uzinduzi wa kampeni hizo siku ya jumamosi.

Baadhi ya wanasiasa waliofika kupigania kata hiyo ni pamoja na wale wa CIVIC UNITED FRONT(CUF) Wakiongozwa na kiongozi wao ambae ni katibu wa chama hicho taifa maalim Seif Sharif Hamad,Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakiongozwa na katibu wao mwenezi bwana Nape Nnauye pamoja na wale wa Chama Cha Demoklasia na maendelea(CHADEMA).

Kata hiyo ya Magomeni inafanya uchaguzi wake mala baada ya aliekuwa diwani wa kata hiyo kuiaga dunia ghafla mwishoni mwa mwaka jana na hivyo nafasi yake ya udiwani kubaki wazi.

Nao wananchi waliohudhuria kampeni hiyo walisema kuwa wanahudhuria kwa wingi katika kampeni hizo ili kusikiliza sera za wagombea na hatimae kuchagua diwani wao kulingana na sera zake na sio chama chake.

Walisema wanasiasa wa sasa wamekuwa na tabia ya kuwadanganya wananchi wakati wa kampeni lakini mwisho wa siku hawatekelezi ahadi zao.

NAPE NNAUYE AKIONGEA NENOWANANCHI WAKISIKILIZA KWA MAKINI
MAMBO YAMEPAMBA MOTO
WANANCHI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZAMSIFANYE MAKOSA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni