visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Ijumaa, 10 Oktoba 2014

VITAMBULISHO VYA TAIFA VYAGEUKA KERO TANZANIA

Shughuli ya upatikanaji wa vitambulisho vya uraia nchini Tanzania imegeuka kuwa kero kwa wananchi badala ya faraja waliyoisubiri kwa hamu.
Kumekuwa na msongamano wa watu katika maeneo mbali mbali wanaoitwa kupokea vitambulisho vyao bila mafanikio.
Kwa Zaidi ya miaka miwili sasa tangu vitambulisho hivyo vianze kuandaliwa na hatimaye kutolewa, kumekuwa na changamoto upande wa uhakiki taarifa na uhaba wa vifaa walivyopewa NIDA na serikali ya Tanzania kama vitendea kazi.
Vifaa vilivyotarajiwa kwa zoezi zima la usajili na utoaji wa vitambulisho nchini Tanzania ni elfu tano lakini kwa sasa vilivyopo ni miatano tu kwa nchi nzima yenye mikoa Zaidi ya 26.
Msongamano wa raia wa Tanzania mbele ya kituo cha kupokea kadi za utambulisho wa raia,bila kujali mwanamke ama mwanaume mzee au kijana ,mjamzito ama mzazi wote mchapalo pasi na tafrija, macho mlangoni kusubiria nani atatoka wa kwanza kwenye kadhia ya kukaribiana kwa saa moja hadi saa mbili,mradi kitambulisho kitoke na maisha yaendelee.
Credit:BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni