visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Ijumaa, 23 Mei 2014

MOURINHO AKEBEHI UBINGWA WA ARSENAL

Miezi kadhaa iliyopita kocha wa Chelsea Jose Mourinho alimpa jina la “Special in Failure” mpinzani wake Arsene Wenger ambaye ni kocha wa klabu ya Arsenal.
Moja ya sababu kuu ya Mourinho kumpa jina hilo Wenger ni kutokana na kushindwa kwake kuiongoza Arsenal kushinda ubingwa kwa kipindi cha takribani miaka 9.
Lakini mapema wiki iliyopita, Wenger aliiongoza Arsenal kushinda ubingwa wa FA Cup, na wakati huo Mourinho alikuwa akijiandaa na safari ya kwenda barani Africa kwa ajili ya kufanya kazi za ubalozi wake wa shirika la chakula duniani WFP.
Mourinho alialikwa na kituo cha Channel 4 kwa ajili ya Interview kuzungumzia mambo mambo mbalimbali juu ya safari yake ya Africa, lakini pia mambo yanayohusiana na soka, na moja kati ya swali aliloulizwa lilikuwa juu ya kufikiria kubadilisha mtazamo wake juu ya Wenger kuhusu kuwa bingwa wa kufeli: Mourinho alijibu – “Katika miaka 9 iliyopita Arsenal wameshinda kombe moja tu la FA Cup……….mmmmh huu utakuwa muda mzuri kwao.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni