visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumapili, 25 Mei 2014

HATIMAE JAYZEE AGOMA KUHUDHULIA HARUSI YA KANYE WEST ILIYOFANYIKA JANA

Hatimaye Rapa maarufu wa muziki wa nchini Marekani Kanye West na mwanadada anayemake headlines kila kukicha Kim Kardashian wamefunga pingu za maisha na kuwa mume na mke huko Florence nchini Italia. Wapenzi hao walisafiri kwa nyakati tofauti kutoka jijini Paris nchini Ufaransa ambako waliungana na familia zao katika ile Pre Wedding Party.
Taarifa zinadai kuwa wanandoa hao wapya walipanga kufunga ndoa hiyo huko Chateau de Versailles lakini sheria za Ufaransa hazikuwaruhusu kufanya hivyo kutokana na hata mmoja wao kutokuwa na uraia wa nchi hiyo.
Cha kushangaza ni kwamba si Jay Z wala Mke wake Beyonce aliyehudhuria katika harusi hiyo na kuishia kutuma salamu za pongezi licha ya kuwepo kwa uvumi kuwa Jay Z atakuwa msimamizi wake kutokana na ukaribu na urafiki mkubwa waliokuwa nao.
Tza

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni