visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Alhamisi, 29 Mei 2014

ZITO ATUHUMIWA Inaendelea kutoka uk 1

Mbilinyi alizihusisha Sh12.2 milioni za Hifadhi ya Taifa ya Saadan na maandalizi ya filamu fupi ya kuhamamisha shughuli za utalii wa hifadhi kwa kuwatumia wasanii kutoka mkoani Kigoma na kusisitiza kuwa wana nakala ya mkataba huo.
Alisema ofisi ya kampuni ya Gombe Advisors zipo jengo moja na zilipo ofisi za Kampuni ya Leka Dutigite na kusisitiza kuwa nyaraka walizo nazo zinaonyesha kuwa Zitto na Raphael Ongangi ndiyo wakurugenzi, huku Zitto akitajwa kuwa mchumi katika kampuni hiyo.
“Zitto siyo mchumi kama ambavyo zinaeleza nyakara za usajili wa kampuni hiyo. Ni mbunge na kiongozi na kwa mujibu wa sheria viongozi wanatakiwa kuwa waadilifu, wenye huruma, utulivu na umakini,” alisema Mbilinyi.
Aliongeza: “Kwa kadri ya ufahamu wa Kambi Rasmi ya Upinzani ya Bunge lako tukufu, Zitto hajawahi kutangaza masilahi aliyonayo kwenye mikataba ya Gombe Advisors na Leka Dutigite.”
Alisema Zitto kwa kampuni hizo mbili amefanya biashara na mashirika yanayosimamiwa na kamati yake na kulipwa fedha za umma.
“Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kutoa maelezo kwa kuwa suala hili linahusu mbunge na mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusika na usimamizi wa fedha za umma,” alisema.
Alifafanua kuwa Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge nayo ifanye uchunguzi wake juu ya madai ya masharti ya Katiba ya Nchi, Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na Kanuni za Bunge juu ya maadili ya kiongozi wa umma, yakiwamo yanayohusu utangazaji wa masilahi.
Zitto ajibu mapigo
Hata hivyo, Zitto mwenyewe alipohojiwa jana, alijibu kwa ujumbe mfupi wa maandishi (sms) akisema amesikitishwa na kitendo cha kuingizwa katika siasa za majitaka katika kipindi hiki akimuuguza mama yake.
“Kampuni ya Leka Dutigile inamilikiwa na wasanii na Gombe Advisors ni kampuni isiyofanya faida na haina masilahi yoyote ya kiabiashara,” alisema.
“Wasanii wa Kigoma wamefanya kazi na Tanapa na NSSF kazi ambazo zipo na zinajulikana,” alisema Zitto aliyekuwa naibu kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni kabla ya kuondolewa.
“Kwa namna yoyote, hii ni ishara ya kukosa ubinadamu maana waliyoyasema wanajua sina faida yeyote ya kifedha, leo wala kesho na Leka Dugitile na Gombe Advisors,” alisisitiza Zitto.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni