visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Alhamisi, 22 Mei 2014

BILIONEA ANAEMILIKI UTAJILI WA $8.8 BILION AAMLIWA KUTOA TALAKA YA $4.5 BILION KWA MKEWE.

Mahakama nchini Uswisi imeamuru Dmitry Rybolovlev, mmiliki wa klabu maarufu ya Ufaransa, AS Monaco kumlipa zaidi ya dola za kimarekani 4.5 bilioni mke wake wa zamani Elena Rybolovleva katika kile kinasemwa kwamba ni moja ya talaka au usuluhishi wa ndoa ghali wa kihistoria duniani.
Mwenendo wa kesi hiyo ya ndoa ilianza mapena mwaka 2008 wakati mke wake huyo wa zamani alidai kiasi cha dola za kimarekani 5.77 bilioni kutoka mwa tajiri huyo wa kirusi. Wote wa umri wa miaka 47 na walikaa kwenye ndoa miaka 24.
Katika hukumu hiyo ya mahakama mke huyo wa zamani wa bilionea wa kirusi alipewa vitu vyenye thamani paundi 146 milioni katika eneo la Gstaad. Mwanamama huyo alipewa pia majumba mawili katika jiji la Colony, sehemu ambayo wanandoa hao wa zamani walikuwa wakiishi na binti zao wawili na kuhakikishia kupewa ulinzi wa binti zao Anna mwenye umri wa miaka 13 na Ekaterina mwenye miaka 14 ambaye ni binti maarufu kwenye jamii.
Wanandoa hao walikutana kama wanafunzi katika chuo kikuu cha Perm nchini Urusi, na wakafunga ndoa mwaka 1987. Walikuwa mahakama kwa muda wa miaka sita katika vita kali vya kimahakama ambapo bilionea Rybolovlev aliweka upinzani mkali kuhusu mali zake ghali mno katika majiji ya Marekani na mali ya thamani paundi 100 milioni katika kisiwa cha Skorpios nchini Ugiriki.
Rybolovlev pia anamiliki nyumba Hawaii ambayo alinunua kutoka kwa muigizaji Will Smith, na ghorofa lenye urefu wa mita 6,744 katika jiji la Manhattan. Mwaka 2008, pia alinunua ghorofa kutoka kwa Donald Trump yenye urefu wa mita 33,000 kwenda juu la sq ft Maison L’ Amitie kwa dola za kimarekani 95 milioni.
Katika jarida la Forbes orodha ya mwaka 2014, Dmitry Rybolovlev alikuwa nafasi ya 147 kati ya mabilionea duniani na thamani halisi ya utajiri wake ni dola bilioni 8.8.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni