visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumapili, 25 Mei 2014

MATOKEO YA UCHAGUZI YANAONESHA KUWA BILIONEA PETRO PEROSHENKO ANAONGOZA NA ATAKUWA NDIE RAIS MPYA UKRAIN

Matokeo yanayotokana na maoni ya wapigaji kura yanaonesha kuwa biliyoneya anayetengeneza chakileti, Petro Poroshenko, ameshinda katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa rais wa Ukraine.
Inakisiwa amepata asili-mia 56 ya kura.
Matokeo rasmi hayatotangazwa hadi Jumatatu.
Bwana Poroshenko alisema azma yake ni "kumaliza vita na kuleta amani", na alisema Ukraine daima haitokubali Urusi "kulikalia" jimbo la Crimea.
Waziri Mkuu wa Urusi, Dmitri Medvedev, alizuru Crimea wakati upigaji kura unaendelea, hatua ambayo serikali ya Kiev imesema ni uchokozi wa kusudi.
Upigaji kura ulisonga mbele ingawa vituo vya kupigia kura havikufunguliwa katika miji ya Mashariki ya Donetsk na Luhansk.
Bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni