visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 21 Mei 2014

ANGALIA FID Q ALIVYOMUONYA DYNA KUACHA KUTUMIA MIKOROGO KATIKA MISTARI YAKE

Fid Q na Dayna na Fid Q ameingia hasa utata wa kwenye line zake kadhaa kwenye wimbo wa Sina Muda wa Jcb ambazo zimeonekana kumhusu moja kwa moja Dayna.
Fid Q ameonekana kama anamfokea Dayna kwa kutumia mkorogo unao badilisha ngozi yake na kuonekana mweupu kitu ambacho Fid Q amedai kuwa Dayna anaukimbia uafrika,Mistari ya Verse hiyo iko hivi.
“Hi Dayna, sikufichi ulikua unahusika/
au mtoto wa uswazi ‘ akijichubua ‘ haimaanishi anaukimbia uafrika?/
nisikize Dayna..please.. najua uko busy kiaina na hizi ni aina tu za uchizi au kama vipi bye DAYNA/
HUUH.. now back to you fools/
Soudy brown kamtafuta Fid Q ambapo alipoulizwa kuhusu hili majibu yake alidai kuwa katika ngoma hiyo hamzungumzii Dayna Msanii bali anamzungumzia Dayna msichana anayeishi nae kitaani maeneo ya Mikocheni kwa Nyerere.
Dayna huyo wa kiafrika alikua mweusi sasa hivi amejichubua ngozi yake na kuwa mweupe ambapo baadae Fid Q aliuchambua kiutaalam mstari huo na kusema kuwa wadada wanaofanya hivyo wanaua melanie.
Ambacho ni kitu muhimu sana kwenye ngozi na hupatikana zaidi kwenye ngozi nyeusi ya kiafrika chembechembe ambazo huilinda ngozi isiunguzwe na jua.
Majibu ya Dayna baada ya kupigiwa simu na Soudy Brown kutaka kujua kama ameshaisikia hiyo line ya Fid Q alichokijibu ni ameisikia na anamuheshimu Fid Q kwa wazo lake ila kwa wakati huu amepunguza kidogo kutumia mikorogo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni