visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Ijumaa, 18 Aprili 2014

IJUMAA KUU ILA DAA......

Juma Khamis (kwa msaada wa maandiko)
Leo ni Siku ya Ijumaa Kuu, ambapo wakristo duniani kote wanaungana wenzao, kukumbuka mateso aliyoyapata Yesu Kristo, wakati aliposulubiwa msalabani huko Jerusalem, yapata miaka 2, 000 iliyopita
Kumbukumbu hii, inaadhimishwa kwa ibada ya Ijumaa Kuu iliyojaa historia ya mateso ya Yesu Kristu.
Tendo la Yesu kufa msalabani linaonesha jinsi Yesu Kristu alivyokubali kubeba makosa ya wakiristu ikiwa ni fidia ya maisha kwa Mungu.
Hata hivyo, kufa msalabani hakuna maana kuwa Yesu alikuwa na dhambi.
Maandiko ya kikiristu (biblia) yanabainisha kuwa Yesu alikubali kuzibeba dhambi za wafuasi wake katika mwili wake juu ya msalaba, ili wapate kufa wakiwa hawana dhambi na kuishi kwa ajili ya uadilifu.
Kwa kadiri ya mafundisho ya Kanisa Katoliki, dhambi ni matendo yoyote ya makusudi ambayo mtu anayotenda kwa kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu, yaani kuvunja amri 10 za Mungu.
Ili dhambi iitwe dhambi ni lazima itendwe kwa makusudi, yaani na mtu mwenye akili timamu.
Ijumaa kuu inaadhimishwa wakati dunia leo ikiwa imegubikwa na matendo mengi ya dhambi, huku matendo mazuri ya kumtukuza Mungu yakipungua na matendo mabaya ya kishetani yakitawala nafsi za watu na kusababisha watu waishi katika ulimwengu wa kutupiana mpira.
Serikali kwa upande inalaumu madhehebu ya dini, vivyo hivyo madhehebu ya dini yanailaumu serikali kwamba imekuwa laini mno kuruhusu na kuachia kila kitu, hata yale yanayokiuka maadili ya jamii
Kwa upande mwingine wazazi wanalaumu kuwa watoto wa siku hizi hawana heshima, watoto nao wanalaumu wazazi kuwa wao wamelegea katika suala la malezi, yaani wazazi wamekuwa huria mno katika suala la malezi na hawaishi na kutenda kulingana na umri wao.
Mfano mdogo tu, baba wa miaka 60 leo anafikishwa mahakamani kwa kulawiti mtoto wa miaka 12.
Pia kuna kutupiana mpira kati ya masikini na matajiri, kwamba maskini wanalalamika kuwa matajiri ndio chanzo cha uozo wote katika jamii, watu maarufu kujihusisha dawa ya kulevya na athari zake zinawakumba watoto wa maskini.
Pia mvutano mwingine ni kati ya nchi maskini na tajiri, Afrika inazilaumu nchi za Magharibi kuwa zinaua maadili ya Kiafrika kwa kusambaza utamaduni wake mchafu.
Lakini cha kujiuliza, hakuna sera zinazopaswa kuwekwa na nchi kama hizo kuzuia uingiaji wa tamaduni hizo?.
Kwa mfano, angalia suala la ndoa za mashoga, kuna nchi za Kiafrika zimeruhusu kufungisha ndoa za mashoga.
Ndio tendo la ushoga lilikuwepo lakini halikuwa limewekewa sheria ya kuliruhusu mpaka kwenye nyumba za ibada lifanyiwe ibada na kurasimishwa rasmi kuwa huyu mwanamume ni mke wangu na mimi mwanamume mwenziwe ni mume wake.
Sikuu ya Ijumaa kuu inafuatiwa na Pasaka ambayo historia yake imeanza mbali.
Siku hii ndio aliyofufukua Yesu Kiristu baada ya kusulubiwa msalabani.
Kabla ya kuja kwa dini ya Kikiristu, watu walikuwa na dini mbali mbali lakini baada ya kuanza, watu walianza kupuuza utamaduni wa kuabudu miungu na taratibu za watu wa mataifa mbali mbali, walianza kusherehekea sikukuu ya Pasaka, kama ishara ya kukubali utamaduni mpya.
Utamaduni mpya ulihimiza watu waache kuabudu miungu na kumfuata Yesu Kristo kama mfalme na mwokozi wa watu wote duniani.
Jina la Pasaka limetokana na neno la Kiebrania lenye maana ya pasaka.
Jina hilo lina maana ya kupita juu, kukaa juu au mlinzi kama ilivyoandikwa katika Biblia.
Sherehe za Pasaka ya Kikristo ni chimbuko la sherehe ya Pasaka ya Kiyahudi.
Kwa Kiswahili majina ya sherehe za Kikristo na Kiyahudi, hazitofautiani kwa kuwa tukio la kusulubiwa na kufufuka kwa Yesu Kristo lilitokea wakati wa sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi mwaka wa 30 kabla ya Kristo.
Kwa mujibu wa historia ya dini ya Kikristo, wakristo wa kwanza walikuwa Wayahudi.
Awali Wayahudi hao walikuwa wakisherehekea sikukuu ya Kiyahudi pamoja na kumbukumbu ya kufufuka kwa Yesu Kristo.
Hata hivyo, Wayahudi waliojikita kwenye dini ya Kikristo, waliamua kutenganisha sherehe hizo na kufuata kalenda tofauti, kwa lengo la kuimarisha dini ya Kikristo.
Pasaka ya Kiyahudi ni miongoni mwa sikukuu muhimu na yenye mtazamo wa kipekee kwa Wayahudi, kwani inatumika kukumbuka jinsi Wanaisraeli walivyofanikiwa kuwa huru, baada ya
Pasaka ya Kikristo inashabihiana sana na Pasaka ya Kiyahudi kutokana na historia ya Pasaka hizo mbili.
Kwa mujibu wa maandiko Musa alitumwa na Mungu kuwaondoa Wanaisraeli katika hali ya utumwa katika nchi ya Misri kisha kuwaongoza kwenda nchi ya ahadi.
Hata hivyo, mfalme wa Misri mwenye cheo cha Farao alikaidi amri ya Mungu na kuendelea kuwashikilia Wanaisraeli.
Kama ilivyo kwa Wayahudi, Pasaka ya wakristo inahesabiwa kuwa sikukuu muhimu kabisa katika ukiristo.
Tarehe ya Pasaka inafuata mwandamo wa mwezi, hivyo sikukuu hiyo haina tarehe maalumu katika kalenda ya kawaida.
Lengo la siku hii ni kuhimiza umoja aliokuwa nao Yesu Kristu kwani maandiko yanasema kabla Yesu Kristo hajasulubiwa msalabani alifanya karamu na kula pamoja na wanafunzi wake ili kuhimiza umoja na ushirikiano baina yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni