visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatatu, 21 Aprili 2014

ETI LUSEKELO HATAKI HEBU MUONE HAPA!

Dar/ Moshi:Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo, Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mchakato wa Katiba kwa lengo la kunusuru amani ya Taifa.
Lusekelo alisema siyo lazima Katiba Mpya ipatikane mikononi mwa Rais Kikwete kwa kuwa hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kubwa, hivyo inaweza kuendelezwa na Rais atakayefuatia mwaka 2015.
Akizungumza jana katika ibada ya Pasaka, Lusekelo alisema hali inayoendelea kwa sasa inajenga hofu na kuwachanganya Watanzania kutokana na hofu ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Alisema Bunge la Katiba kwa sasa limekuwa mfano wa klabu ya pombe za kienyeji kutokana na vurugu alizodai kuchangiwa na wajumbe wa CCM.
“Hakuna majadiliano ya kujenga hoja na badala yake tunasikia matusi tu yanarushwa... uamuzi wa Profesa Ibrahim Lipumba kutoka nje ulikuwa ni sahihi. Hata mimi iwapo ningekuwa mjumbe, ningekuwa wa kwanza kutoka,” alisema Lusekelo na kuongeza:
“Kwa hiyo ni vyema mchakato ukasitishwa kwa hatua iliyofikia ili Taifa litulie na wananchi wajiandae kwa Uchaguzi Mkuu ujao.”
Iwapo mchakato huo hautasitishwa, alipendekeza busara zitumike kuunda jopo la watu kutoka Usalama wa Taifa na wataalamu wa masuala ya kiuchumi ili kujadili hoja tata ya muundo wa Serikali.
Alisema wachumi wanaweza kutafsiri hali ya uendeshaji wa uchumi wa nchi endapo serikali tatu zitapitishwa huku watu wa usalama wakitafsiri usalama wa nchi endapo muundo wa serikali mbili utakufa.
“Watu wa usalama wanaifahamu nchi hata kwa miaka 30 ijayo, wanajua usalama wa taifa hili utakuwaje, kwa hivyo wakikaa na wachumi wanaweza kuja na mapendekezo mapya tufanyeje,” alisema Lusekelo.
Lusekelo alisema: “Rais alikuwa na nia njema kabisa baada ya kuruhusu mchakato huu uanze, lakini kabla ya kuunda Tume inaonekana hakuwa amezungumza na chama chake juu ya mchakato wa Katiba, kwani kama angekuwa amewashirikisha yote haya yasingejitokeza.
“Tume aliyoiteua ilikuwa na watu makini sana kuanzia Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Mkuu mstaafu Augustino Ramadhani na wenzake, ni wasomi wa sheria kwa hivyo walikaa na kuchambua mpaka wakaona muundo wa serikali tatu ndiyo unafaa.”
Alisema tatizo kubwa linalojitokeza ni pamoja na wajumbe wa CCM kulazimisha muundo wa serikali mbili ikiwa ni tofauti na uchambuzi uliofanywa na Tume hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni