visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Alhamisi, 19 Juni 2014

HEMEDI PHD KUMUOA MENEJA WAKE

Muigizaji na muimbaji mwenye mikogo inayozidi bilioni za Dr Dre, Hemedy PHD amesema baada ya ‘kuchafua sana’ sasa ameamua kutulia na msichana mmoja ambaye anatarajia kufunga naye ndoa mwezi November mwaka huu.
“Nimeshachafua sana, yaani more than sana,”alikiri Hemedy kupitia XXL ya Clouds FM.“Ikafika hatua mpaka nikaona kwamba hii lazima iishe yaani kwasababu umri unaenda mama yangu anategemea vingi kutoka kwangu[...] kwahiyo mwisho wa siku nikapata msichana ambaye nikaona she is the right person for me, anaendana na mimi anakubaliana na ninachokifanya”.
Hemedy amesema licha ya kuwa hakuwa amejiandaa kwa ndoa hivi karibuni lakini ameitaja sababu ya kuamua kufunga ndoa mwezi November.
“kitu ambacho alichokuwa anataka zaidi ni mtoto na kama ilivyo kikawaida mtoto hawezi kuzaliwa nje ya ndoa, kwahiyo I was like boo siko tayari mimi ni star lazima nifanye kitu kikubwa kwenye yangu harusi yangu akasema as long as dini inaruhusu tufunge ndoa ya kihalali ambayo kidini haina gharama, so hiyo ndoa inakaribia kufungwa halafu tutapanga kuja kuparty, kwahiyo Novemba Inshallah nitakuwa mume wa mtu”.
Huyu ndiye mke mtarajiwa wa Hemedy aitwaye Muna aka Momo
Hemedy amemtambulisha rasmi mpenzi wake huyo kwa jina la Muna au Momo ambaye anadai amekuwa nae katika uhusiano nae nyuma ya pazia kwa mwaka mmoja na nusu na miezi 9 toka amtambulishe.
Ameongeza kuwa mke wake mtarajiwa ndiye meneja wake kikazi na…,
“Kitu kingine ambacho watu walikuwa hawakifahamu mke wangu mtarajiwa ndio meneja wangu right now ndio anammanage Hemedy from bed to stage”.
Hemedy ameongeza kuwa kwa sasa anapenda afahamike kama Hemedy aka Pappi na sio PHD sababu maana halisi ya PHD inafanana na tabia aliyokuwa nayo ya ‘kuchafua’ ambayo ameamua kuipa mgongo.
“The name PHD kidogo inaelekea ukingoni kwasababu maana halisi ya PHD ni jina flani ambalo kiukweli haliko…kuanzia sasa ningependa kutambulika kama Pappi”.Alisema Pappi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni