visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumanne, 3 Juni 2014

DHAHABU YA LOLIONDO inaendelea.........ktoka uk 1

Wajitokeza kuomba vitalu
Magayane alisema kutokana na kuthibitika uwepo wa dhahabu katika eneo hilo ofisi yake imepokea maombi 14 ya kuchimba.
Alisema walioomba wote ni Watanzania na hakuna kampuni ya kutoka nje ya nchi.
Kuhusu taratibu za utoaji wa leseni alisema: “Nitakwenda Ngorongoro hivi karibuni na kuonana na viongozi wa Serikali kwanza kujua umiliki wa ardhi hiyo kabla ya kutoa leseni.”
Taarifa hiyo ya wataalamu wa Serikali imetolewa takriban miezi matatu tangu wachimbaji wadogo walipogundua madini hayo huku Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali akipinga taarifa za uwepo wa madini hayo.
Lali ambaye alikuwa hajafika Samunge tangu uchimbaji ulipoanza wiki iliyopita, aliibuka na kupinga taarifa za watu kuongezeka Samunge kuchimba dhahabu.
MWANANCHI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni