visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumamosi, 20 Septemba 2014

SIERALEONE WATII AGIZO LA SERIKALI LA KUTOKUTOKA MAJUMBANI MWAO

Mitaa ya Siera Leone
Raia wa Sierra Leone wamesalia majumbani mwao kwa siku ya pili mfululizo wakati ambapo taifa hilo linatekeleza agizo la kutotoka nje la masaa 72 ili kujaribu kusitisha ueneaji wa ugonjwa wa Ebola.
Mwandishi wa BBC katika mji mkuu wa Freetown anasema kuwa barabara nyingi za miji ambazo zimekuwa zikijaa watu hazina watu kwa sasa.
Mwandishi wetu anasema kuwa kituo cha oparesheni za dharura kilipokea zaidi ya simu 900 katika siku ya kwanza ya agizo hilo,kupitia kuwaripoti wagonjwa ama kutaka miili ya wafu kuchukuliwa.
Amesema kuwa kuna vituo viwili pekee katika taifa hilo na kwamba kituo kimoja katika eneo la Kenema kimejaa wagonjwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni