visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumanne, 23 Septemba 2014

MKUU WA MKOA ARUSHA AWA MGENI RASMI MKUTANO MKUBWA WA UTALII

Mkutano mkubwa unaohusu mambo yate ya utalii unafanyika jijini Arusha na kuhudhuriwa na washiriki kutoka nchi mbalimbali duniani ukiwa na lengo la kukuza na kuendeleza utalii.

Mkutano huo ambao umeandaliwa na kampuni ya MPINGO TOURISM SUMMIT na mgeni rasmi akiwa ni mkuu wa mkoa wa Arusha mheshimiwa Magesa Mulungu unahusu mambo yote ya utalii,changamoto na faida kutokana na fulsa za utalii zilizopo Tanzania hususani jijini Arusha.

Wawakilishi wanaohudhuria katika mkutano huo wanatoka katika nchi mbalimbali duniani ikiwa ni pamoja na Austraria,South Africa,Marekani,Zimbabwe,United Kingdom,Netherland pamoja na kutoka makampuni mbalimbali ya utalii ambayo yalishiriki kupata fulsa hizo.

Akizungumza wakati wa mkutano huo,mkurugenzi bwana Bakiri Angalia ambae ni CEO Grobal Skills aliwashukuru washiriki wote kwa kuchangia mada kama ambavyo ilikuwa ikiwasilishwa kutoka kwa wasemaji.

Mkutano huo uliofunguliwa september 22 unatarajiwa kumalizika september 23 jijini arusha na washiriki wanamatumaini makubwa kuwa tasnia ya utalii itapiga hatua kubwa sana kutokana na maazimio ya mkutano huo.

Chanzo:mshiriki mwanahabari mshiriki kutoka Arusha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni