visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Ijumaa, 26 Septemba 2014

KIPIMO CHA SKETI NI MBINO MOJAWAPO YA KUJUA UKO KATIKA HATARI YA CANCER

Baadhi ya watafiti wana sahuku ikiwa vipimo vya sketi vitamtahadharisha mwanamke kuhusu tisho la Saratani
Utafiti unaonyesha kuwa wanawake wanaonenepa maishani bila ya kuwa waangalifu wanajiweka katika hatari ya kupata Saratani.
Watafiti kutoka chuo Kikuu cha London wanasema kwamba wanawake walio kati ya umri wa miaka 24-28 ambao huendelea kunenepa kila baada ya miaka 10, wako katika hatari zaidi ya kupata Saratani ya Matiti baada ya kupitisha umri wa kuzaa.
Sasa je ni nini ishara ya mwanamke kunenepa? Watafiti wanasema vipimo vya sketi yake vinaweza kukusaidia kujua ikiwa uko katika hatari ya kpatwa Saratni ya Matiti au la.
Kila unapogundua kuwa sketi yako inaendelea kuwa ndogo kiunoni, basi inakubidi ujue kuwa mwili wako unaongekeza kwa unene. Na pia ni rahisi kwa wanawake kukumbuka kipimo cha sketi kuliko kitu kingine chochote.
Kwa hilo watafaiti wanasema mwanampe anapaswa kutahadhari kila sketi yake inapoendelea kuwa ndogo kwake maana kwamba amenenepa zaidi. Ikiwa ukubwa wake unazidi kwa kipimo cha sketi mbili katika kipindi kimoja basi mwanamke anakuwa katika hatari ya kupatwa na Saratani hata zaidi.
'Mfumo wa maisha'
Tisho hili linawakabili zaidi wanawake waliopitisha umri wa kupata watoto
Akizungumzia utafiti huo, Simon Vincet kutoka shirika la kupambana na saratani ya Matiti la Breakthrough Breast Cancer, alisema kuwa saratani ya Matiti miongoni mwa wanwake inaweza kupunguka ikiwa watu watabadilisha mfumo wa maisha kwa kujiuzia kunenepa kupita kiasi na kufanya mazoezi sana.
Utafiti huu unaangazia njia rahisi sana kwa wanawake kuwa waangalifu kuhusu unene wa miili yao.
Kuangalia kipimo cha sketi kati ya wanawake walio kati ya miaka 24 na 28 wenye miaki katikati ya 20 na zaidi wanaweza kuwa na njia rahisi ya kufuatilia uzito wa miili ya Unene wa kupita kiasi unajulikana kwa sababu ni hatari kubwa inayochangia katika ugonjwa wa saratani , hususan mafuta ya yaliyoko tumboni.
Prof Usha Menon wa shirika lakupambana na satratani ya matiti, ndiye aliyeongoza utafiti huo na kuambia BBC kuwa "Kama kipimo cha sketi kinaweza kuthibitishwa na wengine kama kigezo cha wanawake watu wazima kuapa Saratani, basi hii itakuw anjia nzuri na rahisi ya mtu kuwa mwangalifu ili asinenepe kupita kiasi.
'Changamoto'
Unene kupita kiasi ni moja ya mambo yanayohatarisha afya ya wanawake waliopitisha umri wa kuzaa
Watafiti hao walisema utafiti wao ulikuwa na changamoto kadhaa kwamba uliangazia zaidi wanawake kukumbuka vipimo vya sketi zao tangu tangu wawe na umri wa miaka 20
Lakini ikiwa matokeo ya utafiti huo yatathibitishwa, itakuwa njia rahisi kwa wanawake kuelewa hatari zinazowakabili hasa wanapoendelea kunenepa.
Tom Stansfeld kutoka shirika la utafiti wa Saratani nchini Uingereza,anasema utafiti huo unaweza kuaminika lakini unazingatia zaidi wanawake kukumbuka vipimo vya sketi walizovalia miaka ya zamani.
Utafiti unasema kuwa baadhi ya mambo muhimu ambayo mwanamke anaweza kufanya kupunguza tisho la kuugua Saratani ya Matiti , hasa baada ya kupitisha miaka yake ya kuzaa ni pamoja na kufanya mazoezi , kula vizuri na kupunguza ulevi.
Kupunguza unene ni njia moja wapo ya kupunguza tisho la kupata Saratani baada ya kupitisha miaka ya kuzaa na kuangalia vipimo vya sketi za wanawake kuwahamasisha wanawake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni