visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumapili, 21 Septemba 2014

MR,BLUE ATAJA ANAEPENDA KUFANYA NAE MZIKI KATI YA DIAMOND NA ALLY KIBA

Kihistoria, Diamond na Alikiba ni wadogo zake Mr Blue. Wakati Mr Blue anatamba na ngoma zake ikiwemo Mapozi, hakuna aliyekuwa akiwafahau wawili hao.
Na kuna wakati Blue aliwahi kusimulia namna alivyokerwa na tabia ya Diamond ya kutembea na ex wake akiwe Wema na Najma. Hata Hivyo rapper huyo wa Pesa, amesema anawakubali wote Alikiba na Diamond na wote ni washkaji.
“Unajua mie wale wote washkaji zangu nawala sina tatizo nao kwahiyo nipo tayari kufanya kazi na yeyote yule ambaye atakuwa tayari si unajua hii kazi na kazi mkishirikiana pamoja ndo inakuwa nzuri zaidi,” Blue ameiambia Bongo5.
Akizungumzia kuhusu video, rapper huyo amesema anatarajia kutoa video mbili kwa pamoja.”Nimeshaulizwa sana kuhusu natoa video lini. Jibu sasa lipo tayari kwa mashabiki wangu. Nitaachia video mbili hivi karibuni na hizo video nimefanya zote na Adam Juma. Video ya Pesa ipo tayari na namalizia kushoot video ya Mapenzi pia kwahiyo muda wowote nitaziachia.”
Kwa upande mwingine Kabasyer amesema kama akitaka kurudi shule basi atasomea tu muziki na utayarishaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni