visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumanne, 23 Septemba 2014

MASHAMBULIZI YA MAREKANI YAANZA NCHINI SYRIA

Majeshi ya Marekani yameanza rasmi mashambulizi ya anga nchini Syria yakilenga kundi la kigaidi la ISIS (Islamic State of Iraq and Syria).
Makao Makuu ya Ulinzi ya Marekani yameeleza kuwa wanafanya mashambulizi ya mchanganyiko kwa kutumia mabomu, wapiganaji wa ardhini pamoja na majeshi ya Anga kutoka nchi za Mashariki ya Kati zinazowaunga mkono.
Lakini habari za mashambulizi yaliyoanza zilitolewa na raia wa Syria aliyetweet kuhusu kile anachokisikia katika mji aliopo wa Raqqa ambako kuna makao makuu ya kundi hilo.
Mtu huyo anaetumia jina la Abdulkader Hariri aliandika kuwa milipuko mikubwa imelenga makao makuu ya ISIS na kwamba anga lote limejaa ndege za kivita na drones.
Baadae Agency ya wanaharakati nchini Syria ilipost video fupi inayoonesha kwa mbali mashambulizi ya Marekani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni