visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumanne, 8 Julai 2014

SOMA

DONDOO 8 MUHIMU KWA WAZAZI NA WAZAZI WATARAJIWA

1. Kila wakati mwanao anapoenda kucheza na wenzake, hakikisha
unafuatilia kujua wanacheza nini, siku hizi hata watoto wanafundishana michezo michafu

2. Mkanye mtoto wako wa kike kuhusu kukubali kupakatwa hovyo,
bila kujali ni nani anampakata, hata kama ni mjomba wake.

3. Usiruhusu mtu yoyote amwite mwanao “Mchumba”, “Mke wangu” au “Mme wangu”.

4. Usivue nguo mbele ya mwanao pindi akifikisha miaka 2 au zaidi.
Jifunze kumwomba akupishe.

5. Kama mwanao ameonyesha kutopenda kwenda kwa mtu fulani
usimlazimishe, pia chunguza kwa ukaribu ili kujua sababu.

6. Inashauriwa kupitia kwanza mwenyewe movie yoyote kabla ya kuruhusu mwanao waiangalie.

7. Mfundishe mwanao thamani ya kuishi bila kufuata mkumbo.

8. Mwanao akilalamika kuhusu mtu fulani, usikae kimya fuatilia ujue sababu ni ipi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni