visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumapili, 10 Agosti 2014

MAAJABU YA MUAROBAINI

Maajabu Tiba ya Muarobaini
Ndugu msomaji, Unaujua muarobaini...?
Wengi wetu watasema wanaujua lakini hawajui maana ya kuitwa muarobaini mti huo kwa kuwa mti huu ulipandwa nchini kwa amri ya kila nyumba kuwa na miti hii japo miwili huku wenye maeneo ya biashara wakihimizwa kuupanda mti huu kwa masharti kuwa asiyepanda basi atanyang’anywa leseni!
Si maneno ya mtu mwingine bali Kanali Yusuph Makamba ambaye aliwahi kuwa mkuu wa mkoa huu wa Dar Es Salaam enzi hizo za mwanajeshi huyu alipopata wazo la kuleta mbegu hii toka nchini India na kuupandikiza kijeshi-jeshi maana anatujua fika watanzania kwa ubishi usio na maana hata kwa maslahi yetu wenyewe.
Leo hii hasa vipindi hivi vya jua kali utakuta watu wote wapo chini ya muarobaini wakipata oksijeni nyiiingi tu toka kwenye mti huo jeuri bila kumbukumbu kuwa ulipandwa kwa viboko! Lakini, Angalau dozi ya malaria sasa inagusa mitaa ya shilingi elfu kumi na zaidi huku watanzania bado wanashindwa kutegua kitendawili cha mwanajeshi huyu mstaafu. Yeye amemaliza kazi:
Alikoutoa huo mti nchini India, unaitwa village Pharmacy na mlipomuuliza huu ni mti gani aliwajibu kuwa huu ni muarobaini na alijua mtalishika hili jina hadi mtakaposhindwa kumudu gharama za mahospitalini basi kila mtu atajua mwarobaini ni nini kwa kuwa utatibu maradhi yote yatakayotusumbua watanzania na kutunusuru na gharama hizi kubwa za madawa ya kemikali mahospitalini.
Nasikitika kuwa inawezekana siku tutakapolijua hili pengine mtaalamu huyu toka jeshi la Tanzania anaweza akawa kaburini na tukabaki na historia yetu ya kutangaza wema wa mtu baada ya kifo chake…
Muarobaini ukikamuliwa juisi yake umethibitishwa na vyuo vikuu vya tiba duniani kuwa una uwezo wa kukinga maambukizi ya HIV nap engine kutibu kabisa ugonjwa wa UKIMWI ambao husababishwa na virusi vya HIV.
Muarobaini una uwezo mkubwa wa kuzuia aleji na kutibu pia aleji za aina tofauti kama juisi yake itapakwa mwilini na hata kama utainywa pia.
Muarobaini huko Marekani na India umeonyesha uwezo mkubwa wa kuzuia nyani dume kutoa mbegu za uzazi kwa majike na kugundulika kuwa juisi ya muarobaini inamfaa mwanaume anayetaka kupanga uzazi bila kwenda hospitali kwa vipimo, ushauri na kufanyiwa upasuaji mdogo kukinga uzalishaji wa mimba (Vasectomy)
Muarobaini pia ni kiboko kwa wanawake wasio na mpango wa kushika mimba vilevile. Muarobaini kama utakamuliwa juisi yake na kupakwa kwenye via vya uzazi vya mwanamke , basi juisi hiyo itamsaidia mwanamke kutopata mimba zisizotarajiwa.
Muarobaini una uwezo mkubwa wa kupambana na kansa na hata kinga ya mwili pia. Tindikali ziitwazo Polysaccharides na limonoids zilizomo katika magamba, majani na mizizi huboresha kinga ya mwili haraka mno ili kupambana na maradhi kama kansa na mengineyo bila uharibifu wa mwili kama zilivyo dawa kemikali za mahospitalini.
Muarobaini hutibu kisukari kwa haraka sana. Majani matatu tu ya muarobaini ni dozi tosha kwa mgonjwa wa kisukari na akizidisha zaidi ya matatu basi anaweza kurudi hospitali na kuwaomba tena waganga waitafute sukari kwenye damu yake kwa tochi! Maana muarobaini utaikomba sukari yote kwenye damu hivyo usijiongezee dozi kijinga.
Muarobaini hushambulia wadudu wote wanaoshambulia ngozi ya binadamu kwa usahihi kabisa. Muarobaini hutibu mapunye, mba, ukurutu, upele na magonjwa kadhaa ya ngozi bila madhara yoyote.
Muarobaini hutibu magonjwa ya moyo. Huifanya damu kuwa nyepesi itembee kwa mwendo sahihi na kuyafanya mapigo ya moyo kuwa tulivu kwa wenye maradhi ya moyo.
Mafua. Ujerumani ambako ni nchi ya baridi kwa kipindi kirefu cha majira ya mwaka watu hufa kwa mafua tu! Tafiti walizofanya zinasema juisi ya muarobaini hukata mafua haraka zaidi ya dawa yoyote ya hospitalini huku ikikuhakikishia usalama bila madhara.
Muarobaini unaua fangasi. Inawezekana una fangasi miguuni, kwenye maungio ya siri kama mapajani, kwapani, sehemu za siri n.k. tumia juisi ya muarobaini ujipake sehemu zilizoathirika kupambana na fangasi hao bila madhara.
Muarobaini pia ni dawa ya kufukuza wadudu bila madhara ya kemikali. Jaribu kulala chini ya muarobaini lakini angalia pawe na majani yake hapo chini halafu utaona hakuna usumbufu wa mbu wala nzi maana mwarobaini hufukuza wadudu aina kadhaa akiwemo mbu!
Wakala wa kulinda mazingira Marekani imeupitisha muarobaini kama kinga bora ya kuhifadhia mazao dhidi ya wadudu waharibifu huku ikidaiwa kwamba muarobaini hauna sumu mara 200 zaidi ya madawa ya kemikali na mazao yanakuwa salama kwa matumizi ya binadamu,ndege na wanyama kwa ujumla.
Muarobaini pia hutibu malaria. Mchanganyiko maalum wa majani ya muarobaini uitwao kwa kitaalam “irodin A” ni sumu ya kuzuia na kutibu malaria. Majaribio mengi yamefanyika hata hapa nchini na muarobaini umeonekana una nguvu ya kupambana na malaria hata hapa nchini Tanzania japo si mti wenye asili yetu.
Nilipoingia katika tiba asili, wataalamu wengi waliniambia kama nataka mafanikio ya haraka basi nianze na kutibu wagonjwa kwa muarobaini. Naapa kwa watanzania wote kuwa nilifanikiwa sana maana hakuna aliyerudi akasema hakupona ugonjwa wowote hivyo nina imani siku mwarobaini ukitumika kama India basi utaitwa National Pharmacy….
Na nina wasiwasi kuwa kama wadau wa afya wakichelewa kuwajulisha wenye nchi taarifa hii muhimu tena kwa vituo basi watakapogundua hili, matabibu wengi watakosa ajira maana hakuna atakayeenda tena hospitali: akatafute nini?
Maana hata urafiki kati ya matabibu na wenye nchi utapungua kwa kuwa watagundua kuwa walifichwa habari hizi ili wawe mitaji ya wadau wa afya ambao ni sisi! Binafsi nimeanzisha kozi ya kutengeneza vidonge vya muarobaini inayogharimu shilingi elfu sitini tu kwa wenye familia zenye msimamo na tiba asili ili kesho niweze kujitetea kuwa nilijitahidi kwa uwezo wangu kusambaza taarifa hizi kwa vitendo.
Je, wewe mdau wa tiba mwenzangu umechukua hatua gani? Nipigie tukutane ofisini siku ya jumatatu, jumatano na Ijumaa pale machinga Complex Ilala Dar Es Salaam tuyaongee kwa vituo. Ada ya mazungumzo ni shilingi elfu tano tu!
Asanteni kwa kunisoma na tuuenzi Muarobaini….
Tabibu John Haule
Machinga Complex, Kawawa road.
Room no. 35F, 36F and 37F
Kariakoo Dar Es Salaam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni