visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatatu, 30 Desemba 2013

WATANZANIA TUHAMASISHE WATALII WA NNJE KWA KUFANYA UTALII WA NDANI

Ukimuuliza mtanzania wa kawaida leo kama anamfahamu mnyama aina ya mamba atakwambia alimuona kwenye luninga tu na wala hajawahi kumuona moja kwa moja.

Sio kwamba wanyama hao na wengine hawapatikani Tanzania isipokuwa watanzania tumekuwa na utaratibu wa kutokutembelea vivutio vilivyoko kwenye nchi yetu wenyewe na wakati huo huo tukilalamika kuwa serikali haifanyi jitihada za kutosha kuvutia watalii wengi zaidi kutoka nchi za nje na hatimae kuiingizia serikali pesa za kutosha.

Zamani tulikuwa tunatoa sababu mbalimbali kuwa viingilio katika vivuto vya watalii ni vikubwa sana kiasi kwamba tunashindwa kumudu ghalama zake,lakini kwa sasa hatuna sababu yoyote ya kutoa kwa kuwa gharama hizo ziko chini sana na wakati mwingine mtanzania anaweza kutembelea maeneo hayo hata bule.

Hapa najaribu tu kuwaonesha mamba wanaopatikana mji wa Bagamoyo mkoa wa pwani ambao wangekuwa sababu tosha kwa wakazi wa maeneo ya karibu kama Dar es salaam na maeneo ya pembezoni kutembelea eneo hilo na kupata historia zaidi ya mji huo;

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni