visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Jumatano, 30 Julai 2014

ISRAEL YAENDELEA KUWAUA WAPALESTINA

Shambulizi Gaza laua watu 15 katika soko
Takriban watu 15 wameuwa na wengine 160 kujeruhiwa vibaya katika shambulizi kali la angani lililotekelezwa na Israeli kwenye soko moja huko Gaza .
Kwa mjibu wa viongozi wa Kipalestina mlipuko mkubwa ulilipua soko moja la Shejaiya la kuuza matunda na mboga ambalo kwa kawaida huwa na idadi kubwa ya watu, mashariki mwa Gaza.
Msemaji wa wizara ya afya Nchini Palestina amesema kuwa idadi kubwa ya wapalestina waliouwawa ama kujeruhiwa walikuwa wakiendesha shughuli za ununuzi wa bidhaa.
Msemaji wa kundi la Hamas, linalothibiti maeneo hayo Sami Abu Zuhri amekatalia mbali muafaka wa amani na kutaja kuwa hauna maana.
Wanahabari wanasema kuwa haijafahamika bayana iwapo wapalestina walikuwa wakijua kuwa watashambuliwa.
Shambulizi Gaza laua watu 15
Walioshuhudia wanasema kuwa, waliona moshi mkubwa ukifuka kutoka eneo hilo huku magari ya kutoa huduma ya kwanza yakionekana yakiingia na kutoka mahalipa tukio.
Aidha inasemekana kuwa mmoja wa waandishi habari ameuwawa katika shambulio hilo.
Wakati huo huo, majeshi wa nchi kavu ya Israel yamesema yatasitisha mapigano kwa muda wa masaa manne, lakini kauli hiyo haitotumika katika maeneo ambako wanajeshi wake wanaendeleza operesheni.
BBC

ISRAEL YAENDELEA KUWAUA WAPALESTINA

Shambulizi Gaza laua watu 15 katika soko
Takriban watu 15 wameuwa na wengine 160 kujeruhiwa vibaya katika shambulizi kali la angani lililotekelezwa na Israeli kwenye soko moja huko Gaza .
Kwa mjibu wa viongozi wa Kipalestina mlipuko mkubwa ulilipua soko moja la Shejaiya la kuuza matunda na mboga ambalo kwa kawaida huwa na idadi kubwa ya watu, mashariki mwa Gaza.
Msemaji wa wizara ya afya Nchini Palestina amesema kuwa idadi kubwa ya wapalestina waliouwawa ama kujeruhiwa walikuwa wakiendesha shughuli za ununuzi wa bidhaa.
Msemaji wa kundi la Hamas, linalothibiti maeneo hayo Sami Abu Zuhri amekatalia mbali muafaka wa amani na kutaja kuwa hauna maana.
Wanahabari wanasema kuwa haijafahamika bayana iwapo wapalestina walikuwa wakijua kuwa watashambuliwa.
Shambulizi Gaza laua watu 15
Walioshuhudia wanasema kuwa, waliona moshi mkubwa ukifuka kutoka eneo hilo huku magari ya kutoa huduma ya kwanza yakionekana yakiingia na kutoka mahalipa tukio.
Aidha inasemekana kuwa mmoja wa waandishi habari ameuwawa katika shambulio hilo.
Wakati huo huo, majeshi wa nchi kavu ya Israel yamesema yatasitisha mapigano kwa muda wa masaa manne, lakini kauli hiyo haitotumika katika maeneo ambako wanajeshi wake wanaendeleza operesheni.
BBC

Jumamosi, 26 Julai 2014

MASKINI:MUNGU AMLAZE DR KAPOLI MAHALI PEMA

TANZIA!!!

Tumempoteza Mwalimu wetu Dr. Kapoli.

Hakika tutamkumbuka kwa changqmoto za kitaaluma alizokuwa akitupa tukiwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza SJMC-UDSM!
"Dr.KAPOLI AMEFARIKI DUNIA JANA KTK HOSPITAL YA TUMBI. TAARIFA HII NIMELETEWA NA MKE WAKE ASUBUHI SAA 2.00 ASUBUHI YA LEO 26.7.2014 MWL.ERNEST MRUTU"
"

HOSPITALI YA IMTU YAFUNGIWA BAADA YA SAKATA LA VIUNGO

Baadhi ya viungo vya miili vilivyokutwa
Oliver Oswald na Adam Malinda, Dar es Salaam
SERIKALI imeifungia Hospitali ya Chuo Kikuu cha Tiba na Teknolojia (IMTU) kilichopo Mbezi eneo la Interchiki kwa muda usiofahamika.
Hospitali hiyo imefungiwa kutokana na kukosa sifa, ambapo imebainika kuwa maabara pamoja na wauguzi wake hawana vigezo vya kutoa huduma za kitabibu.
Hatua ya kuifungia hospitali hiyo imekuja siku chache tangu chuo hicho kilipokumbwa na tuhuma nzito za kuhusika na utupaji wa viungo vya binadamu katika eneo la Bonde la Mto Mpiji, Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi jana, Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja, alisema Serikali imechukua uamuzi huo baada ya kugundua kasoro nyingi zinazoikabili hospitali hiyo.
Alisema katika ukaguzi uliofanywa na jopo la wataalamu kutoka wizarani kwa kushirikiana na uongozi wa Manispaa ya Kinondoni, ulibaini kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu za kuendesha huduma za kitabibu.
“Kweli nimepokea taarifa za kufungiwa kwa Hospitali ya IMTU kutoka katika jopo letu lililokwenda kufanya uchunguzi hospitalini pale ambao wana wajibu wa kutembelea hospitali zote zilizopo ndani ya halmashauri yao kila mara.
“Katika uchunguzi wao wamethibitisha kukuta mapungufu hayo pamoja na mengine ambayo wizara itayaweka wazi katika mkutano wake na waandishi wa habari kesho (leo),” alisema Mwamwaja.
Aliyataja baadhi ya mapungufu yaliyogunduliwa na jopo hilo kuwa ni pamoja na hospitali hiyo kutokuwa na maabara inayojitosheleza kwa shughuli mbalimbali za kujifunzia pamoja na baadhi ya wauguzi wake kukosa sifa ya kutoa huduma za kitabibu.
Katika uchunguzi wa awali uliofanywa na Jeshi la Polisi ilibainika kuwa Chuo Kikuu cha IMTU kilihusika na tuhuma za kutupa mabaki ya viungo vya miili ya binadamu vilivyookotwa Julai 22, mwaka huu katika Bonde la Mto Mpiji.
Katika tukio hilo jumla ya mifuko 85 yenye viungo vya binadamu vilivyokaushwa na kuchunwa ngozi viliokotwa, ambapo Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwatia nguvuni watumishi wanane kwa kuhusishwa na tukio hilo.
Viungo vilivyookotwa katika eneo hilo ni pamoja na mafuvu ya vichwa, sehemu ya kifua cha binadamu, miguu, mikono, moyo na mbavu.
Kwa upande wake Rais wa Serikali ya wanafunzi wa udaktari wa IMTU, Meekson Mambo, ameelezea kusikitishwa na uamuzi huo wa Serikali, akisema umewaathiri wanafunzi.
Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi jana muda mfupi kabla ya gazeti hili halijaenda mtamboni, Mambo alisema kufunga hospitali hiyo ni sawa na kufunga chuo kwa kuwa mafunzo ya vitendo hufanyika katika hospitali hiyo.
“Sisi tunaonewa katika sakata hili kwa kuwa waliofanya uzembe ni viongozi, hatuhusiki kwa namna yoyote na utupwaji wa mabaki ya miili hiyo iliyokutwa huko Mpiji. Kwa kweli uamuzi huu haukuzingatia athari tutakazozipata,” alisema.
Mambo alisisitiza kuwa Serikali inapaswa kuwa makini katika uamuzi inaoufanya, kwani wanafunzi wamebakiza muda mfupi kabla ya kuanza kwa mitihani ya kumaliza mafunzo.
Rais huyo alisema uamuzi huo wa Serikali haukuzingatia umuhimu wa wanachuo kupata haki ya masomo na mafunzo kwa njia ya vitendo, hivyo utawaathiri kisaikolojia.
“Tumebakiza muda mfupi, Agosti 4 mwezi ujao tunaanza mitihani, kama hospitali imefungwa hatima yetu ya mitihani itakuwaje, hii ni kujenga mazingira ya kufanya vibaya katika mitihani yetu,” alisema.
Hata hivyo, Mambo alishauri waliohusika na sakata hilo wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria ili kulinda heshima ya taaluma bila kuathiri wasio husika hasa wanafunzi waliopo chuoni hapo.
Mtanzania

Ijumaa, 25 Julai 2014

HATIMAE MTOTO ALIEIBWA CHANGANYIKENI APATIKANA.

HATIMAYE kinara wa wizi wa watoto jijini Dar es Salaam, Amir Juma, amekamatwa na Jeshi la Polisi akiwa mkoani Tanga.
Juma anadaiwa kumuiba mtoto, Merlin Repyson (4) katika eneo la Changanyikeni siku nane zilizopita.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe, alikiri kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo akiwa wilayani Korogwe

Jumatano, 23 Julai 2014

UNYAMA

CHUO Kikuu cha Kimataifa Matibabu na Teknolojia (IMTU) kilichopo Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam ndicho kinahusika na tukio la kinyama la kuichuna, kuikatakata, kuikausha na kisha kuitupa miili ya binadamu kwenye Bonde la Mbweni Mpiji, lililopo Manispaa ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo awali gazeti hili lilizipata na kuthibitishwa na polisi pamoja na uongozi wa chuo hicho ni kwamba, chuo hicho ndicho kinahusika na sakata hilo na kwamba tayari baadhi ya viongozi wa chuo wameshakamatwa na Jeshi la Polisi.
Jana gazeti hili liliandika taarifa iliyoelezea tukio hilo kubainika baada ya akina mama wanaofanya kazi ya kuponda kokoto kwenye eneo hilo kufungua baadhi ya mifuko hiyo iliyokuwa imetupwa na watu wasiojulikana.
Mashuhuda wa tukio hilo walilieleza gazeti hili kwamba, viungo hivyo vya binadamu vilitupwa Julai 20, mwaka huu, lakini hakuna aliyegundua kutokana na kukaushwa na kupulizwa dawa iliyovizuia kutoa harufu.
UONGOZI WA CHUO WAKIRI
Ofisa Rasilimali watu wa Chuo hicho, Michael Lazaro, alikiri chuo chao kuhusika kwenye tukio hilo, lakini alishindwa kufafanua kwa kina ni kwanini walifanya hivyo, ambapo alisema kitengo cha maabara kinachohusika na uchunguzi na utafiti wa viungo vya binadamu ndicho kinahusika moja kwa moja na tukio hilo.
Lazaro alisema kwa mujibu wa taratibu za chuo, mabaki ya tafiti na chunguzi hizo huwa yanachomwa kwenye tanuru maalumu la kuchomea kemikali, lililopo Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambapo anashindwa kufahamu ni kwanini kitengo hicho kilikwenda kutupa taka hizo porini bila kutoa taarifa za kwanini hawakupeleka mabaki hayo Muhimbili.
Alipoulizwa ni wapi wanatoa miili hiyo, Lazaro alisema mtu pekee ambaye angeweza kutoa ufafanuzi wa kina wa wapi inatoka miili hiyo ni Mkuu wa kitengo hicho, anayefahamika kwa jina la Dimesh Kumaar, ambaye anashikiliwa na polisi.
Alipotakiwa kutupeleka kwa Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Prabhakar Rao ili kuelezea sakata hilo, Lazaro alisema bosi wake huyo ni mgeni nchini, lakini pia naye ni mmoja wa viongozi wa chuo waliokamatwa na Jeshi la Polisi.
MADUDU YA CHUO YAIBULIWA
Baada ya tukio hilo, kumeibuka madudu mengi yanayokihusisha chuo hicho na sakata la kutupa viungo vya binadamu, ambapo mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho alisema uongozi wa chuo hicho umekuwa na matatizo na kwamba sakata kama hilo liliwahi kutokea miaka ya nyuma, ambapo kuna mwanafunzi wa chuo hicho alionekana akiwa na mkono wa binadamu mtaani kitendo ambacho hakiruhusiwi.
Mtoa habari wetu alisema kuwa muhula wa kwanza wa masomo ulimaliza kutumia miili hiyo mwezi Machi mwaka huu na uongozi ulitakiwa kuiteketeza, lakini walishindwa kutokana na kifaa cha kuteketeza mabaki hayo kuharibika, ambapo waliomba msaada Muhimbili, huko nako waliambiwa kifaa kimeharibika.
Katika kuhakikisha wanaviteketeza inadaiwa waliomba msaada kwenye maeneo mbalimbali, ambapo walitakiwa kutoa fedha ili kazi hiyo ikamilike, lakini walishindwa kutoa fedha badala yake wakaamua kwenda kuitupa bondeni.
Alisema kuwa hatua hiyo ilifikiwa ili kuwahadaa wajumbe waliokuwa kwenye msafara wa Umoja wa Vyuo vya Madaktari Afrika, ambao kama wangekutana na mabaki hayo ni wazi wangepoteza sifa.
MUHIMBILI WAZUNGUMZA
Kwa upande wake Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminieli Eligaesha, alikiri kuharibika kwa mtambo wa kuteketeza mabaki hayo hata hivyo alikanusha uvumi wa kwamba viungo hivyo vimetoka hospitalini hapo.
Eligaesha alisema kifaa hicho kimeharibika tangu mwezi Februari mwaka huu na kwamba waliagiza kifaa kingine kutoka nje ya nchi ambacho baada ya kuunganishwa kifaa kingine kiliharibika.
“Kawaida huwa tunaagiza vifaa vya mitambo yetu kutoka nje ya nchi, lakini tulipounganisha kuna kifaa kingine kiliharibika na ndiyo maana hadi sasa ndugu waandishi mmeshuhudia mafundi wakiendelea kuutengeneza mtambo huo na kwa mujibu wao utakuwa tayari hivi karibuni,” alifafanua Eligaesha.
JESHI LA POLISI LAUNDA JOPO LA UCHUNGUZI
Kwa upande mwingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limeunda jopo la upelelezi la watu saba linaloongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ACP Japhari Mohamed.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, alisema jopo hilo limeshaanza uchunguzi mara baada ya kupata taarifa hizo kwa kushirikiana na Daktari wa Jeshi la Polisi ambaye anahusika na uchunguzi wa miili ya binadamu pamoja na madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Kova alisema uchunguzi wa awali ulibaini kuwa kwa mara ya mwisho viungo hivyo vilikuwa katika maabara ya Chuo Kikuu cha Madaktari cha International Medical and Technological University (IMTU) kilichopo jijini Dar es Salaam ambacho pia hufanya mafunzo ya udaktari kwa vitendo.
Alisema jeshi hilo tayari linawashikilia watu wanane kwa mahojiano kutokana na utupwaji wa viungo hivyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, alisema viungo hivyo vilipatikana jana katika eneo hilo vikiwa katika mifuko mieusi ya plastiki ipatayo 85.
Alisema kati ya watu wanane waliokamatwa wengine ni madaktari pamoja na wale waliohusika katika utekelezaji wa tukio hilo na wamewahoji na kukiri kuhusika.
“Miongoni mwa maswali tutakayoendelea kuwahoji ni pamoja na sababu ya wingi wa viungo hivyo na kwanini walienda kuvitupa katika eneo lile la wazi ambalo watu wengi hupita.
“Ili kufanikisha upelelezi wetu, tutamshirikisha Mkemia Mkuu wa Serikali ili aweze kufanya uchunguzi wa kina ikiwamo kubaini viungo hivyo ni vya muda gani kwa kutumia vinasaba (DNA), pia itabainika kuwa ni vya watu wangapi.
“Baada ya uchunguzi kukamilika jalada hilo litapelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili hatua za kisheria zaidi zichukuliwe dhidi ya wahusika pamoja na kujua kuwa ni sheria gani zimevunjwa katika kulinda viungo vya binadamu,” alisema Kova.
MAITI ZINAVYOPATIKANA
Wataalamu wa afya wameeleza namna miili hiyo inavyopatikana na kutunzwa kwa ajili ya mafunzo.
Wamesema kuwa miili hiyo hupatikana kutokana na maiti ambazo zimekaa kwa kati ya miezi sita mpaka mwaka bila kutambuliwa na ndugu zao.
Walisema miili hiyo hutoka katika nchi mbalimbali na kwamba nchi moja ikiwa na shehena ya maiti hutafuta nchi nyingine iliyo mbali ili kubadilishana miili hiyo.
“Kwa mfano Tanzania inaweza kubadilishana miili hii na nchi nyingine iliyo Afrika Magharibi, vinapofika vyuoni huwekwa kwenye maabara maalumu, jambo hili hufanyika kwa umakini sana, haijawahi kutokea mtu aliyeenda kusomea fani ya tiba akakutana na mwili wa ndugu yake ama rafiki yake,” alisema Dk. Samwel Shita.
Dk. Shita ambaye ni mtaalamu wa tiba, anasema miili hiyo hujulikana kitaalamu kama cadaver na hutumiwa na wanafunzi wa vyuo vya tiba, lengo likiwa ni kuifanyia upasuaji ili kujifunza maumbile ya mwili mzima wa binadamu.
Anasema kuwa miili hiyo inaweza kuwa ni ile iliyokosa ndugu wa kuizika na pia baadhi ya watu hujitolea na kuandika kimaandishi kuwa pindi wakifariki miili yao itumike kwa ajili ya mafunzo.
Anasema baada ya kukamilika kwa zoezi hilo hupendekeza namna ya kuhifadhiwa kwake, maiti hizo huhifadhiwa kwa kipindi cha miezi sita mpaka mwaka mmoja kisha kukabidhiwa kwa wataalamu wa afya ambao huzitunza na kuziwekea dawa maalumu ili zisiharibike wala kuguswa na bakteria wa aina yoyote.
Dawa hiyo inajulikana kama 2-phenoxethanol maarufu kama fomulani. Anasema kuwa dawa hii huingizwa katika mshipa mkubwa wa paja na kisha huenea sehemu yote ya mwili kupitia mfumo wa mishipa ya damu.
Anasema kuwa dawa hiyo huweza kuutunza mwili huo kwa muda mrefu na kuwa hakuna vijidudu vinavyoweza kuugusa na hata ukiwekwa sehemu ya wazi hakuna ndege wala mnyama atakayeweza kuugusa.
“Si kunguru, bakteria au fangasi au kiumbe chochote kinachoweza kuugusa au kuishi kwenye mwili uliowekwa dawa hii,” alisema Dk. Shita.
Alisema kuwa dawa hiyo inatambulika kama moja ya kemikali zinazoweza kusababisha saratani kama mtu atakumbana nayo kwa muda mrefu.
Dawa hii huweza kuwa na harufu kali na inayokera, ina ukakasi na pia huwa rahisi kuwa kama mvuke ambao mtu akiuvuta hupata shida kupumua.
Baada ya mwili huu kutengenezwa, huifadhiwa katika vyombo maalumu vilivyojaa dawa ya maji ya fomulani mpaka pale itakapohitajika.
Dk. Shita anaeleza kuwa mwili wa binadamu umefunikwa kwa ngozi ambayo huwa ni ngumu, hivyo hulazimu watu wanaojifunzia miili hiyo kutenganisha ngozi kwa kuichuna ili kuweza kuona sehemu za mwanzo ambazo huwa na tishu laini kama kitambaa na sehemu hizo huitwa farcia.
Pia huweza kuonyesha mishipa ya damu kwa juu, mishipa ya fahamu ilivyogawanyika katika tishu, misuli ya mwili pamoja na viungo vingine.
Anasema kuwa ni vigumu kuzifikia sehemu hizo bila kuchuna ngozi.
Anasema kuwa dawa ya fomulani husababisha athari mbalimbali katika mfumo wa hewa, mfumo wa fahamu na ngozi.
Alisema kuwa dawa hiyo ndiyo inayonyima kiumbe chochote kuweza kuishi.
Wakati Dk. Shita akieleza namna miili hiyo inavyopatikana na kutunzwa, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Tiba cha Bugando, Dk. Rodrick Kabangila, anasema hata kama miili hiyo ilitumika kwa ajili ya kufundishia wanafunzi wa tiba, kuitupa porini kunaonyesha namna mamlaka zinazosimamia fani hiyo zilivyoshindwa kufanya kazi.
“Mimi nilivyoona hiyo shehena nilikuwa na mambo mawili ya kujiuliza, kwanza niliona yawezekana yametoka hospitali ama kwenye vyuo vya tiba ambapo wanafunzi hutumia kujifunzia.
Lakini ukiangalia hata kama imetoka kwenye vyuo huwa kuna namna ya kuihifadhi kazi yake ikiisha. Nilivyoona zile ngozi zilivyokuwa nyingi nikasema ni vigumu zikawa zimetoka hospitali kwa sababu kule huwa wanachukua ngozi kidogo tu kwa sababu ya kuziweka kwenye sehemu nyingine ya mwili,” alisema Dk. Kabangila.
Alisema kuwa tangu miaka ya 1970 madaktari wamekuwa wakifundishwa na hakuna tukio kama hili, hivyo yawezekana kilichofanyika ni hujuma ama waliopewa kuteketeza mzigo huo walitaka kwenda kuuza.
“Yawezekana watu walikula hela ama ni mtu alikuwa amepatana na mtu mwingine ampelekee huo mzigo wakashindwa kuelewana bei ndiyo wakaenda kuutupa huko,” alisema.
Alisema kuwa katika kufundisha wanafunzi wa udaktari, ni suala la kawaida kuchuna ngozi ya sehemu moja ili kujua mishipa ya damu imepita wapi, ikoje, misuli imepita wapi na ikoje.
Habari hii imeandaliwa na Asifiwe George, Veronica Romwald, Deonidas Mukebezi na Jonas Mushi
MTANZANIA

Jumanne, 22 Julai 2014

WATU NANE MASHAKANI SAKATA LA VIUNGO VYA BINADAMU


Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam linawashikilia watu wanane wanaoshukiwa kuhusika na sakata la kutupwa kwa mifuko zaidi ya 85 iliyokuwa na mabaki ya viungo mbalimbali vya binadamu kama vile vichwa,miguu,mikono,mioyo mapafu,vifua na mifupa mbalimbali iliyogundulika katika eneo la mbweni mpiji jijini Dar es salaam hapo tar 21/7/2014.

Watu hao ambao ni pamoja na madaktari wa hospitali ambayo pia ni chuo cha udaktari IMTU kilichopo jijini Dar es salaam wanashikiliwa na jeshi hilo baada ya uchunguzi wa awali ambao umebaini kuwa mifuko hiyo ilitoka katika hospitali hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari,kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova alisema kuwa viungo hivyo havikuwa na uvundo wala harufu yoyote na vilionekana kuwa vimekaushwa na kukakamaa.Kova alisema pia kuwa katika eneo hilo vilionekana vifaa vinavyotumika hospitari kama vile mipira ya kuvaa mikononi(gloves) nguo maalum(apron) na mifuko miwili iliyotunika pamoja na karatasi mbili zenye maswali na majibu.

"Viungo hivyo vilichukuliwa na kupelekwa muhimbili kwa uchunguzi zaidi na jopo la wapelelezi wakiongozwa na mkuu wa upelelezi kanda maalum ACP Japhar Mohamed walianza upelelezi mala moja kwakushirikiana na daktari wa jeshi la polisi anayehusika na uchunguzi wa miili ya binadamu(forensic Doctor) ambaye alishilikiana na madaktari wengine kutoka hospitali ya taifa Muhimbili"Alisema Kova

Kamanda Kova aliongeza kuwa baada ya uchunguzi ilibainika kuwa viungo hivyo kwa mala ya mwisho vilikuwa katika maabara ya chuo kikuu cha madaktari IMTU ambacho pia hufanya mafunzo ya udaktari kwa vitendo.

Kamanda Kova alisema kuwa uchunguzi zaidi unaendelea na jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua za kisheria mtu yoyote ambae atagundulika kuhusika na tukio hilo na kuwataka wananchi watulie wakati polisi ikiendelea na uchunguzi