visit here again on mukebez.blogspot.com


CHANGE YOUR LIFE

CHANGE YOUR LIFE
Go to Amazon .com and get the copy of this book to make your life better.

Alhamisi, 3 Aprili 2014

MBINU SITA ZA KUISHI NA KUMHANDLE BOSS MKOROFI


Bila shaka ni ukweli usiopingika kuwa ili kazi iweze kufanywa vizuri,ni lazima anaefanya kazi hiyo aipende na aifanye kwa moyo wake wote.Pia ni kweli kuwa ofisi yako ndio mahali ambapo unakaa muda mrefu zaidi kuliko mahali pengine ukiondoa kitandani.Kwa bahati mbaya wafanyakazi wengi wamejikuta wakizichukia sehemu zao za kazi kutokana na aina ya mabosli walionao.Badala ya kufanya kazi kwa moyo,mtu anajikuta anafanya kazi kuepuka purukushani za bosi na kimsingi kazi hiyo haiwezi kufanywa kiufanisi ukilinganisha na kama mtu huyo anaeifanya angeifanya kwa moyo.Kuna mabosi wengi ambao hawajawahi kuwaamini wafanyakazi wao na mala nyingi maamuzi yao wanayafanya kwa hisia badala ya kufikilia.Mabosi hawa ni hataru sana kwani wanaweza kukufanya ukaharibu kazi yako na huwa ndio namba moja kukufukuza kazi.

Pamoja na ukweli wote huo bado unatakiwa kufanya kazi yako kiufanisi ili kuijenga profession yako.Kwahiyo ili kumuepuka bosi mkoarofi,anaefoka ovyo,na ambae anaendeshwa na hisia,hizi ni hatua sita unazoweza kuzitumia kuishi na mabosi wa aina hiyo.

1.ANDIKA KILA KITU AMBACHO KINAHUSIANA NA BOSI WAKO.
Hakikisha kila mnachojadiri au kufanya na bosi wako unakiweka kwenye maandishi ili kiwe kumbukumbu nzuri atakapokuwa anakushutumu vitu ambavyo utakuwa na uhakika kuwa ni maagizo yake.Mala nyingi mabosi wa aina hii huwa ni wasahaulifu kwa kuwa hawatumii sana akili zao bali hutumia hisia kufanya maamuzi.Kutokana na hilo hawakubali kirahisi utetezi wa mtu isipokuwa kama kuna ushahidi ambao unaonekana.Hakikisha wakati unaandika kumbukumbu zako hizo anakuwa hayupo ili kuepusha matatizo zaidi.

2.EPUKA KUKASIRIKA AU KUONESHA SURA YOYOTE YA KUKASIRIKA WAKATI BOSI WAKO AKIWA AMEPANIC.
Unapoona bosi wako amekasirika au anabwabwaja ovyo kuwa mtulivu na uoneshe tabia zako za kitaaluma(professional manner)ulizofundishwa shule.Tatizo ni kuwa watu wengi huwa wanasahau mambo ya taaluma na kufanya mambo kwa mazoea.Utakapokuwa mtulivu bosi wako atagundua kuwa anachokifanya ni utoto na anaweza kutulia.Pia epuka kujadiliana nae ishu ya kazi akiwa amekasirika kwa kuwa mnaweza kuharibi kazi.Mwambia hatuwezi kujadili ishu hii ukiwa katika hali hiyo.

3KUBALIANA NA SHUTUMA ZAKE KUMRIDHISHA.
Bado naongelea kuhusiana na kuwa professional.Ukitaka kumuweza bosi wa aina hii usipambane kwa kubishana nae,yaani usilipe neno kwa neno.Hii inamaana kuwa usikatae kile anachokiongea bali msikilize halafu umwambie kuwa unakubaliana na shutuma zake na utazifanyia kazi,lakini na wewe pia una matatizo ambayo anapaswa kuyasikiliza.Hii inaweza kumpunguza jazba kuliko ukikataa kila anachosema jambo ambalo linaweza kuleta matatizo zaidi,kumbuka yeye ndio bosi.

4.TAMBUA KUWA HUWEZI KUMBADILISHA BOSI WAKO KAMA NDIO TABIA YAKE KIBIOLOGIA ISIPOKUWA MPE TAARIFA.
Ukigundua kuwa ukorofi ndio tabia ya bosi wako na wala sio ya kuiga kiasi kwamba inaweza kubadilika,unapaswa kuishi kulingana na hali hiyo na mbinu mojawapo ni kuhakikisha kuwa unampa taarifa za matatizo yako at least awe anayafahamu ili asisingizie kuwa hayajui.

5.BAKI KUWA PROFESSIONAL NA USIBADILIKE KWA SABABU YA UKOROFI WWA BOSI.
Kuwa mtulivu na fanya mambo yote kulingana na taaluma yako inavyotaka.Hii haijalishi kuwa anakasirika au la kwa kuwa ukifanya kulingana na taaluma ni dhahili kuwa kazi itakuwa nzuri na sio vinginevyo na hakuna bosi aliewahi kumfukuza kazi mtu aliefanya kazi nzuri.

6.USIMPANDE KICHWANI BOSI WAKO KWA KUWA HII ITAZAA UADUI KATI YAKO NA BOSI WAKO.
Epuka kung'ang'ania jambo hata kama ni haki yako kwani hii itamfanya bosi wako akukasirikie maradufu na kujenga uadui kitu ambacho kitakufanya uione kazi chungu.

MWANAJESHI AWAUA WENZAKE 3 MAREKANI.

Wanajeshi wanne wamepigwa risasi na kuuawa katika kambi ya jeshi huko Fort Hood jimboni Texas.

Jenerali Mark Milley, amesema mwanajeshi mmoja ndiye aliyewafyetulia wenzake risasi hizo karibu na zahanati ya afya ya kijeshi ya Carl R Darnall iliyoko katika kambi hiyo ya Jeshi.

Watu watatu walifariki kabla ya mwanajeshi huyo kujipiga risasi na kujiua.

Wanajeshi wapato wanne wanatibiwa majeraha mabaya ya risasi.

Daktari mkuu wa zahanati hiyo Dakta Glen Couchman anaelezea majeraha wanayotibu.

''Wote walikuwa na majereha mbalimbali ya risasi kwenye vifua shingo na tumbo''.

Waziri wa usalama Chuck Hagel amesema kuwa uchunguzi tayari umeshaanza kubaini chanzo cha kisa hicho cha pili kuikumba kambi hii.

''ninajua kuwa mtangulizi wangu Leon Pannetta aliwahi kusema kuwa tukio kama hili mwaka wa 2009 litachungzwa .

Ni wazi lazima kuna kitu kinachoendelea ambacho hakifai.

Lazima tutatue shida hii .''

Rais Obama amehuzunishwa sana na tukio hilo ambalo anasema limetokea katika kambi ambayo inapaswa kuwa salama .

Obama amesema ''amezungumza na maafisa wa FBI na idara ya mahakama kutafuta kwa kina kiini cha makabiliano haya ilikuhakikisha kambi zetu zimekuwa salama.

Hii siyo mara ya kwanza kwa kituo hicho kikubwa cha majeshi ya Marekani Fort Hood kushuhudia ufyetulianaji wa risasi .

Mwaka 2009 wakati dakatari wa magonjwa ya kiakili wa jeshi la Marekani meja Nidal Hasan alipowapiga risasi na kuwaua watu kumi na watatu.

Rais Obama amesema anafuatilia yanayotukia katika kambi hiyo kwa makini.

Jumatano, 2 Aprili 2014

DUNIA INAELEKEA KUBAYA


Ni jambo la kushangaza sana na mtu unaweza kujiuliza ni kitu gani kilichowakumba watangazaji hawa mpaka kuamua kutangaza kipindi wakiwa bila nguo.Kama ni maswala ya utandawazi,tunakoelekea ni kubaya sana kwani hata watazamaji hawakuonekana kustuka na badala yake walikuwa wakiwapigia makofi watangazaji hao baada ya kuvua nguo zao
Huu ni ushetani na vizazi vijavyo vitakuwa kama wanyama kutokana na uhuru wa hali ya juu unaohubiriwa siku hizi

TAZAMA PICHA ZA NYUMBA SABA(7) GHARI ZAIDI DUNIANI




to live.
7. The Penthouse, One Hyde Park, London - $220,000,000



6.The Steeple Times $222000000


5. Fairfield, Sagaponack, NY - $248,000,000


4. The White House - $320,364,354


3. Villa Leopolda, French Riviera - $506,000,000



2. Antilla Mumbai - $1,000,000,000

Wikimedia Commons


1. Buckingham Palace - $1,560,000,000



KATIKA MAGAAZETI YA LEO NIMEIPENDA HII







UTAJIRI wa komediani maarufu Bongo, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ ni kufuru! Tena unatisha na sasa anaonekana kuwa miongoni mwa wasanii wanaomiliki fedha na mali nyingi Bongo.

Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ akiwa mbele ya usafiri na mjengo wake.


HABARI MEZANI
Awali, habari kuhusu utajiri wa Masanja ilitua mezani mwa gazeti hili kama kidokezo, hapo mwandishi wetu akaingia mzigoni na kuanza kuchunguza kwa kina mali anazomiliki msanii huyo na kugundua kuwa ni kati ya mastaa mabilionea Bongo.

“Masanja sio yule tena. Ana mpunga (fedha) mrefu sana. Hakuna msanii wa maigizo Bongo anayeweza kumfikia kwa sasa. Hao wengine ni mbwembwe tu, lakini pesa imelala kwa Masanja,” kilipasha chanzo chetu.

Kikaongeza: “Kwanza ana ghorofa lipo Tabata, hapo ndipo anapoishi. Pia ana magari kibao ya kifahari, mashamba ya mpunga na Kampuni ya OK Security inayolinda sehemu mbalimbali zikiwemo taasisi nyeti nchini.

Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ akiwa kwenye pozi na miongoni mwa magari yake.

“Ni msanii gani mwenye kampuni kubwa kama ya Masanja? Wengi wanaishia kudai wanatayarisha filamu ambazo hata matunda yake hayaonekani.”

RISASI MZIGONI
Mdogomdogo, Risasi Mchanganyiko likajitupa mtaani kuchimba kuhusu madai hayo ambayo awali liliyatilia shaka kama si wasiwasi.

Uchunguzi wetu ulibaini ukweli wa mali za msanii huyo na mambo mengine mengi yanayoingia kama vyanzo vya mapato yake.

MAGARI SITA
Ilibainika kuwa, Masanja anamiliki magari sita, yakiwemo ya kifahari. Baadhi ya magari hayo ni Toyota Land Cruiser V8, Nissan Hardboad na Toyota Verossa.

NYUMBA TATU BONGO
Pia, mkali huyo wa kuvunja mbavu, anamiliki nyumba tatu za maana jijini Dar es Salaam, moja ni ghorofa ipo Tabata, nyingine Kigamboni na nyingine haifahamiki eneo rasmi ilipo.
Hata hivyo, imebainika kuwa mbali na mijengo yake hiyo iliyopo jijini Dar, nyumbani kwao Mbarali, Mbeya ana mjengo wa maana.

MASHAMBA KIBAO
Msanii huyo hayupo nyuma kwenye kilimo, ana mashamba kadhaa Kigamboni jijini Dar es Salaam lakini linalotia fora ni lile lililopo Mbarali lenye ukubwa wa hekari 50 ambalo analima mpunga.

NI MSANII WAMAIGIZO TAJIRI ZAIDI?
Kwa utajiri huo, ipo minong’ono kuwa, nyota huyo anaweza kuwa kwenye namba za juu za wasanii wa maigizo wenye mkwanja mrefu.
Wengine wanaotajwa kwenye orodha ya waigizaji matajiri Bongo ni Husna Posh ‘Dotnata’, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ na Amri Athumani ‘Mzee Majuto’.
MATAJIRI BONGO FLEVA
Katika muziki wa Bongo Fleva, wasanii wanaoaminika wana utajiri mkubwa zaidi ni Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Joseph Haule ‘Profesa Jay’.
Wasanii hao wanamiliki mijengo ya maana, achilia mbali magari ya kifahari na miradi kadhaa.

MASWALI KUHUSU MASANJA
Utajiri wa Masanja umeonekana kuibuka ghafla huku vyanzo vyake vya kumwingizia kipato vikijulikana ni sanaa ya uigizaji, muziki na huduma ya uchungaji.
Je, kwa uigizaji tu katika Kundi la Orijino Komedi ‘OK’ ndiko alikopata mkwanja huo na kuanzisha miradi hiyo mikubwa?

Kama ndiyo, kwa nini memba wenzake ndani ya kundi hilo hawana maendeleo makubwa kama yeye?
Kazi nyingine ya Masanja ni muziki wa Injili ambapo kwa sasa albamu yake ya Hakuna Jipya iko sokoni. Je, albamu hiyo na shoo anazofanya zinaweza kuwa chanzo cha utajiri huo?

Lakini pia Masanja ni mchungaji ambaye anahudumu katika Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) ‘Mito ya Baraka’ lilicho chini ya Askofu Bruno Mwakiborwa. Je, mshahara anaoupata kutokana na huduma hiyo unaweza kuwa chanzo cha mapato yake?

Risasi Mchanganyiko halikutaka kupasua kichwa, juzi lilimsaka Masanja kwa simu na kumhoji juu ya mali zake ambapo kwanza alithibitisha kweli anamiliki mali hizo na nyingine ambazo hakupenda kuzitaja.

“Ni kweli nina nyumba tatu hapa mjini, kampuni ya ulinzi na mashamba ya mpunga eka 50 nyumbani Mbarali, Mbeya. Kuhusu magari pia ni kweli kabisa. Mimi ni mtumishi sitakiwi kusema uongo,” alisema Masanja.

RISASI: Lakini mbona utajiri wako umekuwa wa haraka sana mtumishi, vipi vyanzo vya mapato yako?
MASANJA: Orijino Komedi ndiyo chanzo cha vyote... pale ndipo kwenye koki.

RISASI: Kuchekesha tu kaka? Au kwenye muziki wa Injili pia kunalipa?
MASANJA: Injili na uchungaji ninaotumika kanisani ni huduma kaka, sitegemei mapato kutoka huko. Nipo kwa ajili ya kulisha kondoo wa Bwana.

RISASI: Wasanii wenzako wa Orijino Komedi wanachukuaje mafanikio yako?
MASANJA: Wanafurahia, wananiunga mkono maana ni sehemu ya mafanikio yao pia. Sisi tunaishi kama ndugu. Kwa hiyo kuna baadhi ya aidia ni zao, hivyo wanajivunia sana mafanikio yangu.
Tuituitui! Simu ikakatika! Risasi likaenda mtamboni.

Habari kwa hisani ya Grobal publishers.

HISTORIA YA TAJIRI NAMBA MOJA AFRICA ALIKO DANGOTE #THE HISTORY OF THE RICHEST PERSON IN AFRICA ALIKO DANGOTE#


Aliko Dangote alizaliwa Nigeria mwaka 1957,april,10.Historia ya utajiri katika familia yake ilianzia kwa babu yake ambae alikuwa na mashamba makubwa ya peanut ambazo zilikuwa zikisafirishwa kwenda ulaya na kufanikiwa kupata utajiri mkubwa.

Jumanne, 18 Machi 2014

WALICHOKIFANYA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA NI UTOVU WA NIDHAMU.


Siku ya jumatatu ya tarehe 17 march 2014 jaji mstaafu mzee Joseph Sinde Walioba alitaka kuwasilisha rasimu ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania tayari kwa kujadiliwa hoja moja baada ya nyingine lakini kwa bahati mbaya alishindwa kutokana na wajumbe wa bunge maalum kufanya fujo kwa kugonga meza na hivyo kutokuwepo na kusikilizana bungeni hapo.

Sina haja ya kurudia kusimulia sababu zilizotolewa na wabunge hao kutetea kitendo chao hicho cha kuzuia Mzee Walioba asiwasilishe rasimu hiyo kwani ni hoja ambazo hata mtoto mdogo atakwambia kuwa hazina mashiko.

Nasema hoja hizo hazina mashiko kwasababu lengo kuu la wajumbe hao kuwepo Dodoma sio hotuba ya Rais au chochote wanachokisema, isipokuwa swala lililowapeleka hapo ni Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo Rasimu yake ndio mzee Warioba alitaka kuiwasilisha ili ijadiliwe.

Kutokana na matukio mbalimbali yanayoendeelea kujitokeza bungeni ambayo mengine hata watoto wadogo wanashangaa kuona kuwa hata watu wazima wanafanya matendo hayo,wananchi wanafika mbali na kudiriki kusema kuwa hizo ni mbinu za kutaka siku ziongezeke na wabunge hao waendelee kuwepo bungeni hapo na kuendelea kula posho zinazotokana na kodi ya wananchi walala hoi wa nchi hii.

Ni dhahiri shahiri kuwa wabunge hawa wanajua wanachokifanya bungeni,ikiwa na maana kuwa wanajua lengo la kufanya vitendo hivyo,na kama watasema hawajui wanachkifanya basi hoja hiyo itakuwa inakwenda mbali zaidi, kwa sababu kuwaweka watu ambao hawajui wanachokifanya halafu tunategemea watoke bungeni pale wakiwa na katiba ambayo itatuongoza wananchi zaidi ya milioni arobaini tena kwa zaidi ya miaka hamsini litakuwa ni jambo la kushangaza kidogo.

Wabunge hawa wanapaswa kufahamu kuwa hichi wanachokifanya sasa kitawaathiri na wao wenyewe pamoja na watoto wao vizazi kwa vizazi vijavyo kwa hiyo bado wana muda wa kujirekebisha na kuongeza umakini katika mambo ya msingi kama hayo.